Tanesco kusoma mita kutokea makao makuu Dar ni wizi?

Tanesco kusoma mita kutokea makao makuu Dar ni wizi?

Jotu

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2012
Posts
444
Reaction score
311
Hivi karibuni Tanesco imeanzisha utaratibu mpya wa kusoma matumizi ya umeme katika mita kutokea makao makuu Dar. Mita mpya zilizowekwa huwa juu sana katika mlingoti wa umeme ambayo mtumiaji hawezi akajua ametumia umeme kiasi gani tofauti na zamani ambayo mtu angeweza soma kiasi alichotumia. Tanesco inachofanya ni kutuma kila mwisho wa mwezi bill ambayo mlaji huwezi kujua kama ni bill halali. maana yake huwezi kuague kabisa lako ni kulipa. Je mlaji anajuaje kuwa ametumia kiasi hicho? Nadhani tunaweza kuibiwa.
 
Ndio ni Wizi; USA pamoja na Techno development lakini bado wanatuma watu majumbani kusoma meter na kufananisha na za maofisini mwao

Kwani Jua ni kali kutuma wapima meter au hawataki kuwalipa Mishahara? Waiweke Mifukoni kama Wafanyakazi Hewa? na Kutoza Wananchi Umeme bei ya Juu?
 
Ndugu yangu hapa kuna utata mimi mwenyewe nimewekewa, nilienda kuomba kuapgrade kutoka single phase kwenda three phase. Kwa kusema ukweli nilicho experience toka nimewekewa hiyo mita gharama zimeshuka, kabla ya hapo nilkuwa nalipa wastani wa elfu themanini hadi laki moja lakini sasa nalipa elfu hamsini hadi sitini na matumizi ni yale yale sasa sijui ni kwangu tuu. Na mimi kilichonifanya niupgrade nilikuwa naexperience low voltage. Labda wenzangu mnaexperience gani na hizi mita za mlingotini mimi naona imenipa advantage.
 
Back
Top Bottom