Tanesco kutangaza kiama kwa wadeni na wahujumu ni mbwembwe?

Twilumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2010
Posts
12,576
Reaction score
14,522
Nimesikiliza taarifa ya habari Clouds Fm, Afisa uhusiano wa Tanesco Babra Masoud ametangaza kwamba wote wanaoihujumu Tanesco kwa kuiibia umeme wajisarimishe ndani ya wiki 2 na kwamba kwa wale wenye mademi wakalipe ndani ya muda huo yaani wiki 2 na kwamba kuna sheria ambayo inawaruhusu wao kupiga mnada nyumba ya mteja ikiwa watakuwa wamelimbikiza deni!

Swali:

kama hiyo sheria ilikuwepo nini walichokuwa wanasubiri maana sijawahi kusikia wamemwajibisha hata mteja mmoja hasa wateja sugu zikiwepo taasisi za serikali na mashirika mengine!

My take:

Wanaleta Propaganda na zaidi hakuna kipya chenye mlengo kulikwamua shirika hilo kutoka kwenye dimbwi la tope la utendaji wa mbovu na wa kimazoea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…