TANESCO: Mabwawa ya kufua umeme yamekauka

TANESCO: Mabwawa ya kufua umeme yamekauka

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
"....Kihansi, Hale na Bwawa la Mungu yote yamekumbwa na uhaba wa maji hali inayopelekea mchana kutozalisha umeme ili kujaza maji ili usiku uzalishaji ufanyike."

TANESCO.


=======

Mamlaka ya Hali ya Hewa hivi karibuni ilitoa taarifa juu ya mabadiliko ya tabia ya nchi yanayoleta athari nyingi ikiwemo upungufu wa vipindi vya mvua unaopelekea hali ya ukame na kuongezeka kwa joto nchini. Hali ambayo imeendelea kujitokeza nchini na katika maeneo mbalimbali ulimwenguni.

Mnamo mwaka jana tayari Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) lilishaanza mikakati ya kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo mseto vya nishati. Mpaka sasa mradi wa kituo cha ubungo namba 3 chenye uwezo wa megawati 112 kinachozalisha umeme kwa gesi umekamilika. Mradi wa kinyerezi 1 extension ambao utaingiza jumla ya megawati 185 katika gridi ya taifa unatarajia kukamilika hivi karibuni. Mradi wa umeme unaotokana na nguvu za jua mkoani Shinyanga, Kishapu ukitarajiwa kukamilika ndani ya mwaka 2023 ukiingiza megawati 50 kati ya 150.

Pamoja na hayo Shirika limeendelea na mikakati ya kuhakikisha tunaongeza vyanzo vingine vya uzalishaji umeme kwa kutumia vyanzo vya nishati jadidifu ambapo hivi karibuni tumeingia makubaliano na kampuni ya Masdar yenye makao yake Abudhabi Jijini Dubai. Ushirikiano huu unalenga kuwezesha miradi mbalimbali ya umeme jadidifu utakaofikia megawati 2000.

Ni dhahiri kwamba, kama mipango hii isingeanza kutekelezwa pengine hali ya kupatikana kwa umeme ingekuwa mbaya zaidi tofauti na ilivyo sasa. Hata hivyo, ni maeneo kadhaa tu katika baadhi ya mikoa ambayo yataathirika katika nyakati tofauti na tutaendelea kuwataarifu wateja wetu kadiri miradi hii itakapoanza kuingiza umeme katika gridi.

Shirika linawaomba radhi wateja wake kwa usumbufu unaoweza kujitokeza na linawahakikishia kuwa litaendelea kutoa taarifa mbalimbali za hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme.
 

Attachments

hata kama maji yangekuepo bado mgao ungekuepo,imefika wakati wananchi atuanimi serikali na mambo yake.
 
uku nilipo toka jana usiku umeme hakuna unarud chap unakatika yan ni mateso
 
Yule madevu awashe tu magenereta yake hatuna uwezo wa kumzuia sisi,wapo juu ya sheria
 
Kwa hiyo pamoja na kuwa na gesi lukuki bado nishati ni tatizo kwetu, Urusi gesi ndo inamtoa hadi inampa kiburi duniani........sisi ndo daily kulialia shida ya umeme. Tunazidiwa na nchi za ulaya ambazo zinategemea gesi kutoka urusi kuzalisha umeme. Ngozi nyeusi tuna shida kubwa sana namna tunavyotumia akili kufikiri.​
 
"....Kihansi, Hale na Bwawa la Mungu yote yamekumbwa na uhaba wa maji hali inayopelekea mchana kutozalisha umeme ili kujaza maji ili usiku uzalishaji ufanyike."

TANESCO.


=======

Mamlaka ya Hali ya Hewa hivi karibuni ilitoa taarifa juu ya mabadiliko ya tabia ya nchi yanayoleta athari nyingi ikiwemo upungufu wa vipindi vya mvua unaopelekea hali ya ukame na kuongezeka kwa joto nchini. Hali ambayo imeendelea kujitokeza nchini na katika maeneo mbalimbali ulimwenguni.

Mnamo mwaka jana tayari Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) lilishaanza mikakati ya kuzalisha umeme kwa kutumia vyanzo mseto vya nishati. Mpaka sasa mradi wa kituo cha ubungo namba 3 chenye uwezo wa megawati 112 kinachozalisha umeme kwa gesi umekamilika. Mradi wa kinyerezi 1 extension ambao utaingiza jumla ya megawati 185 katika gridi ya taifa unatarajia kukamilika hivi karibuni. Mradi wa umeme unaotokana na nguvu za jua mkoani Shinyanga, Kishapu ukitarajiwa kukamilika ndani ya mwaka 2023 ukiingiza megawati 50 kati ya 150.

Pamoja na hayo Shirika limeendelea na mikakati ya kuhakikisha tunaongeza vyanzo vingine vya uzalishaji umeme kwa kutumia vyanzo vya nishati jadidifu ambapo hivi karibuni tumeingia makubaliano na kampuni ya Masdar yenye makao yake Abudhabi Jijini Dubai. Ushirikiano huu unalenga kuwezesha miradi mbalimbali ya umeme jadidifu utakaofikia megawati 2000.

Ni dhahiri kwamba, kama mipango hii isingeanza kutekelezwa pengine hali ya kupatikana kwa umeme ingekuwa mbaya zaidi tofauti na ilivyo sasa. Hata hivyo, ni maeneo kadhaa tu katika baadhi ya mikoa ambayo yataathirika katika nyakati tofauti na tutaendelea kuwataarifu wateja wetu kadiri miradi hii itakapoanza kuingiza umeme katika gridi.

Shirika linawaomba radhi wateja wake kwa usumbufu unaoweza kujitokeza na linawahakikishia kuwa litaendelea kutoa taarifa mbalimbali za hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme.
Ufafanuzi wa madai ya kupungua kwa kina cha maji kwenye mabwawa ya kufua umeme

07 Septemba 2022

Ni kweli kumekuwepo uhaba wa mvua uliojitokeza kwenye maeneo mengi ya nchi yetu kwenye miezi ya hivi karibuni, uhaba huu umesababisha kuwepo kwa upungufu wa kina cha maji kwenye mabwawa ya kufua umeme kwa kutumia maji hivyo kuathiri hali ya uzalishaji wa umeme kwenye baadhi ya vyanzo vinavyotumia maji.

Aidha, ili kuhakikisha kuwa utoaji wa huduma ya umeme inaimarishwa nchini, Shirika limeshachukua hatua mbalimbali za muda mfupi na za muda mrefu kama ifuatavyo;

Mipango ya muda mfupi

[emoji625] Kuanzisha kituo cha kuzalisha umeme kwa njia ya Gesi asilia cha Ubungo III ambacho kimeshakamilika na kuingiza jumla ya Megawati 112 za umeme kwenye Gridi ya Taifa tangu mwanzoni mwa mwaka 2022.

[emoji625]Kuanzisha kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia Gesi asilia cha Kinyerezi I Extension kitakachozalisha jumla ya megawati 185.

Tayari megawati 45 zimeshaingizwa kwenye Gridi ya Taifa na megawati zilizobakia zitaingizwa kwenye Gridi ya Taifa hadi kufikia mwanzoni mwa mwaka ujao.

[emoji625]Mradi wa kufua umeme wa Rusumo kwa kutumia maji.
Mradi huu unaozihusisha nchi tatu (Tanzania, Rwanda na Burundi) utakapokamilika, unategemewa kufua jumla ya megawati 80 za umeme, ambapo kwa upande wa Tanzania, tutapata megawati 27 za umeme zitakazoingizwa kwenye Gridi ya Taifa.

[emoji625]Mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya jua wa Kishapu, Shinyanga.
Mradi huu unategemewa kuanza ujenzi wake Novemba 2022 na kukamilika Disemba 2023, utaingiza jumla ya megawati 150 za umeme kwenye Gridi ya Taifa.

[emoji625]Mradi wa kupeleka Gridi ya Taifa kwenye wilaya za mkoa wa Kigoma.
Tayari umeme wa Gridi ya Taifa umeshapelekwa kwenye wilaya ya Kibondo.
Serikali imeanza kuokoa jumla ya Tsh.9.44 bilioni kwa mwaka zilizokuwa zikitumika kununulia mafuta ya dizeli na kutengeneza mitambo (jenereta).
Mpango uliopo ni kuufikisha umme wa Gridi ya Taifa kwenye Wilaya ya Kasulu hadi Kigoma mjini kabla ya mwisho wa mwaka huu wa 2022 kufika.

Mipango ya muda mrefu

[emoji625]Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maji wa bwawa la Julius Nyerere (JNHPP).

[emoji625]Mradi huu umefikia asilimia 71 ya utekelezaji wake.
Mradi utakapokamilika mnamo mwezi Juni 2024, unategemewa kuingiza megawati 2115 za umeme kwenye Gridi ya Taifa.

[emoji625]Kwa hatua hizi Shirika ilizozichuka zimesaidia kuimarisha hali ya upatikanaji umeme nchini na iwapo jitihada hizi zisingechukuliwa, basi ya upatikanaji umeme nchini kwa sasa ingekuwa ipo vibaya zaidi.
 
Lile Bwawa la Nyerere ni hasara kwa taifa na tutajuta lijenga
 
Kipindi cha Magufuli kulikuwa hakuna hii migao ya mara Kwa mara, kwanini imeanza upya Kwa kasi
 
Na zile pesa mnazoziteketeza pale kwenye bwawa la Nyerere kiukweli mmefeli.

Lile bwawa ni hasara kwa Taifa
 
JNHPP ikikamilia huo mwaka 2025 mna uhakika kutakuwa na maji ya kutosha kuzalisha hizo megawati 2115??
Ufafanuzi wa madai ya kupungua kwa kina cha maji kwenye mabwawa ya kufua umeme

07 Septemba 2022


Ni kweli kumekuwepo uhaba wa mvua uliojitokeza kwenye maeneo mengi ya nchi yetu kwenye miezi ya hivi karibuni, uhaba huu umesababisha kuwepo kwa upungufu wa kina cha maji kwenye mabwawa ya kufua umeme kwa kutumia maji hivyo kuathiri hali ya uzalishaji wa umeme kwenye baadhi ya vyanzo vinavyotumia maji.

Aidha, ili kuhakikisha kuwa utoaji wa huduma ya umeme inaimarishwa nchini, Shirika limeshachukua hatua mbalimbali za muda mfupi na za muda mrefu kama ifuatavyo;

Mipango ya muda mfupi

[emoji625] Kuanzisha kituo cha kuzalisha umeme kwa njia ya Gesi asilia cha Ubungo III ambacho kimeshakamilika na kuingiza jumla ya Megawati 112 za umeme kwenye Gridi ya Taifa tangu mwanzoni mwa mwaka 2022.

[emoji625]Kuanzisha kituo cha kuzalisha umeme kwa kutumia Gesi asilia cha Kinyerezi I Extension kitakachozalisha jumla ya megawati 185.

Tayari megawati 45 zimeshaingizwa kwenye Gridi ya Taifa na megawati zilizobakia zitaingizwa kwenye Gridi ya Taifa hadi kufikia mwanzoni mwa mwaka ujao.

[emoji625]Mradi wa kufua umeme wa Rusumo kwa kutumia maji.
Mradi huu unaozihusisha nchi tatu (Tanzania, Rwanda na Burundi) utakapokamilika, unategemewa kufua jumla ya megawati 80 za umeme, ambapo kwa upande wa Tanzania, tutapata megawati 27 za umeme zitakazoingizwa kwenye Gridi ya Taifa.

[emoji625]Mradi wa kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya jua wa Kishapu, Shinyanga.
Mradi huu unategemewa kuanza ujenzi wake Novemba 2022 na kukamilika Disemba 2023, utaingiza jumla ya megawati 150 za umeme kwenye Gridi ya Taifa.

[emoji625]Mradi wa kupeleka Gridi ya Taifa kwenye wilaya za mkoa wa Kigoma.
Tayari umeme wa Gridi ya Taifa umeshapelekwa kwenye wilaya ya Kibondo.
Serikali imeanza kuokoa jumla ya Tsh.9.44 bilioni kwa mwaka zilizokuwa zikitumika kununulia mafuta ya dizeli na kutengeneza mitambo (jenereta).
Mpango uliopo ni kuufikisha umme wa Gridi ya Taifa kwenye Wilaya ya Kasulu hadi Kigoma mjini kabla ya mwisho wa mwaka huu wa 2022 kufika.

Mipango ya muda mrefu

[emoji625]Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maji wa bwawa la Julius Nyerere (JNHPP).

[emoji625]Mradi huu umefikia asilimia 71 ya utekelezaji wake.
Mradi utakapokamilika mnamo mwezi Juni 2024, unategemewa kuingiza megawati 2115 za umeme kwenye Gridi ya Taifa.

[emoji625]Kwa hatua hizi Shirika ilizozichuka zimesaidia kuimarisha hali ya upatikanaji umeme nchini na iwapo jitihada hizi zisingechukuliwa, basi ya upatikanaji umeme nchini kwa sasa ingekuwa ipo vibaya zaidi.
 
Wahuni Tulijua Lazima Watupige Chap Chap, Mpaka Tunaona Mauzauza
 
Back
Top Bottom