TANESCO, mmefuta ile bei nafuu kwa watumiaji umeme mdogo?

TANESCO, mmefuta ile bei nafuu kwa watumiaji umeme mdogo?

Ghiti Milimo

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2011
Posts
4,748
Reaction score
7,061
Wadau, salaam!

Mi nipo kanda ya ziwa. Nina kiduka, ambacho kinafanya shughuri za ki fedha, yaani, wakala wa Benki mbali mbali, na pia, makampuni ya simu. Pamoja na wateja wa kutoa na kuweka fedha, wapo wa kununua Luku, pamoja na kulipia maji.

Sasa, toka mwezi huu wa Septemba uanze, nimekuwa nikiwasikia wateja wa kununua umeme wanalalamika, kuwa hawapati umeme kwa fedha waliyokuwa wakinunulia miaka yote, yaani kwa wale waliokuwa wamepata punguzo, kwa kuelezwa kuwa serikali imewawekea ruzuku.

Mabadiliko hayo, binafsi nilikuwa sijui, jana Jumapili, ndiyo nilipata nafasi ya kukaa hapo shughurini kwangu, ndipo nilipojithibitishia kuwa, kwa sasa bei ile haipo, kwani watu wote, niliokuwa nafahamu wapo kwenye ile punguzo, kila waliponunua, hawakaupata unit walizokuwa wanapata.

Sasa Wakuu, kuna tanzazo lililotolewa na Serikali, au TANESCO kwa mabadiliko hayo? Kama lipo, naomba nami nilisome, ili nami niwawekee wateja, ili maswali kwa sisi tunaowauzia yapungue!
 
Hukunaga umeme mdogo. Umeme ni ule ule tatizo nikuendekeza siasa kwenye facts
 
Ukitegemea Majibu Sahihi JF Nikupe Pole
JF saivi Inakuongezea Unyonge Kuliko Ulio kuwa nao Hapo Awali
Humu Kila Mmoja Ni Tajiri Anakazi Yupo Vizuri
Anajiona Kila Kitu kwake Poa
Kumbe ndio Ma Kanchukila Wakufa Mtu!
Hawa Ndio Wenye ID Kumi kumi Tangaza Njia Nzuri Ya Kupata MB
Uone utakavyo Fuata Inbox Kwa Id tofauti!
 
Ukitegemea Majibu Sahihi JF Nikupe Pole
JF saivi Inakuongezea Unyonge Kuliko Ulio kuwa nao Hapo Awali
Humu Kila Mmoja Ni Tajiri Anakazi Yupo Vizuri
Anajiona Kila Kitu kwake Poa
Kumbe ndio Ma Kanchukila Wakufa Mtu!
Hawa Ndio Wenye ID Kumi kumi Tangaza Njia Nzuri Ya Kupata MB
Uone utakavyo Fuata Inbox Kwa Id tofauti!
Aloo kunywa soda utalipa hapo hii ni sahihi.sana!
 
Ukitegemea Majibu Sahihi JF Nikupe Pole
JF saivi Inakuongezea Unyonge Kuliko Ulio kuwa nao Hapo Awali
Humu Kila Mmoja Ni Tajiri Anakazi Yupo Vizuri
Anajiona Kila Kitu kwake Poa
Kumbe ndio Ma Kanchukila Wakufa Mtu!
Hawa Ndio Wenye ID Kumi kumi Tangaza Njia Nzuri Ya Kupata MB
Uone utakavyo Fuata Inbox Kwa Id tofauti!
Hapa napafahamu sana! Nasubiri jibu kutoka kwa TANESCO wenyewe! Na inawezekana halikutoka tangazo lolote!
 
Back
Top Bottom