TANESCO mnanigombanisha na TRA. Siwezi kulipa kodi kabisa wakati kutwa nzima umeme hakuna

TANESCO mnanigombanisha na TRA. Siwezi kulipa kodi kabisa wakati kutwa nzima umeme hakuna

polokwane

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2018
Posts
3,361
Reaction score
5,842
Naona kama mama nae anaenjoy tuu wala haoni kama hili ni tatizo kwake anakula tu good time na machawa wake huko DUBAI.

Yani tunashinda mchana bila umeme, usiku ndio umeme unarudi hakafu asubuhi unakatika tena, mambo gani haya! nani unamuhudumia huo usiku huo.

😜😜😜😜😜😜😜Ila hata UNIT za LUKU zimekaa safari hii sijanunua umeme muda mrefu kweli yani hadi nimemiss na nahisi nimesha sahau hata jinsi ya kununua umeme wenyewe maana tangu nilivyo weka hauishi maana hautumiki kabisaaaa.
 
Ivi TRA nao kuna haja ya kuiunganisha na tanesco, yaani Kwa kazi zinazohitaji umeme kama kinyozi mapato yachukuliwe tu kipindi umeme upo
Tanesco wakichukua umeme na mapato hamna
Yaan hili linchi sijui lina viongozi wa aina gani , hawawajibiki kabisaa , waziri wa nishati hajatia muongozo wowote kwenye swala la umeme kukatika katika hivi ,mwanzo walisema maji sasa sahizi maji mengi tu sijui wanasema nini maana hatujawahi kumaliza saa 24 umeme upo.
 
Naona kama mama nae anaenjoy tuu wala haoni kama hili ni tatizo kwake anakula tu good time na machawa wake huko DUBAI,

Nasema hivi niione pua ya ofisa wa TRA hapa kwangu eti anafuatilia mapato yani huyo
namkata pua yake wallah
halafu naipika roast na kachumbari na pilipili kwa mbaaali na ugali wa mtama pemben na kikombe cha mtundi , na sina utani katika hili na panga nimesha linoa kabisa linameremeta kwa makali yake🗡️🗡️⚔️😜

Yani tunashinda mchana bila umeme ,usiku ndio umeme unarudi hakafu
asubuhi unakatika tena, mambo gani haya! nani unamuhudumia huo usiku huo

😜😜😜😜😜😜😜Ila hata UNIT za LUKU zimekaa safari hii sijanunua umeme muda mrefu kweli yani hadi nimemiss na nahisi nimesha sahau hata jinsi ya kununua umeme wenyewe maana tangu nilivyo weka hauishi maana hautumiki kabisaaaa
Pamoja na mafuriko yote haya bado mabwawa ya kuzalisha umeme hayajaa maji. Kweli chama chakavu mna usanii sana kwenye mambo ya msingi. Ndio yale yale ya kuipa Twiga Stars 200M na kununua magoli kwa 10M wakati Katesh Manyara hamna dawa na miundombinu ya kuzuia mafuriko. Hii ni futuhi!
 
“Ipo siku mtanikumbuka, sio kwa mabaya yangu; bali mazuri yangu” JPM.

Inabidi upate changamoto ujue tofauti ya jambo jema na baya.

Miaka mitano ya umeme wa uhakika halafu muhusika wa usimamizi wanasiasa uchwara walikuwa wanadai anaua biashara na uchumi.

Halafu hawa wanaouwa biashara na tuzo wanapewa na mafisadi,

Nchii kufuata mkumbo wa wanasiasa kwa hoja zao za majungu utajikuta pabaya sana, wakati wanufaika ni wengine kabisa.

RIP Magufuli
 
Naona kama mama nae anaenjoy tuu wala haoni kama hili ni tatizo kwake anakula tu good time na machawa wake huko DUBAI,

Nasema hivi niione pua ya ofisa wa TRA hapa kwangu eti anafuatilia mapato , yani huyo namkata namkata pua yake , wallah naipika rost nakachumbari na pilipili iwa mbaaali , na sina utani katika hili na panga nimesha linoa kabisa linameremeta kwa makali yake[emoji2787][emoji2787][emoji3538][emoji12]

Yani tunashinda mchana bila umeme ,usiku ndio umeme unarudi hakafu
asubuhi unakatika tena, mambo gani haya! nani unamuhudumia huo usiku huo

[emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12]Ila hata UNIT za LUKU zimekaa safari hii sijanunua umeme muda mrefu kweli yani hadi nimemiss na nahisi nimesha sahau hata jinsi ya kununua umeme wenyewe maana tangu nilivyo weka hauishi maana hautumiki kabisaaaa
Bas bora uendelee kukatika hili tusinunue luku lakini mjomba kua na subira ngoja mwaka wa uchaguzi ufike umeme hauto katika mwisho mwaka huu kukatika katika kwa umeme kuanzia mwaka wa kesho umeme Oya Oya kwasababu kuku wa mgeni karibu anafika yani uchaguzi
 
Naona kama mama nae anaenjoy tuu wala haoni kama hili ni tatizo kwake anakula tu good time na machawa wake huko DUBAI.

Yani tunashinda mchana bila umeme, usiku ndio umeme unarudi hakafu asubuhi unakatika tena, mambo gani haya! nani unamuhudumia huo usiku huo.

😜😜😜😜😜😜😜Ila hata UNIT za LUKU zimekaa safari hii sijanunua umeme muda mrefu kweli yani hadi nimemiss na nahisi nimesha sahau hata jinsi ya kununua umeme wenyewe maana tangu nilivyo weka hauishi maana hautumiki kabisaaaa.
Lipa kodi ili tupate umeme.
 
Kwamba hutofanyaje? Penda usipende utalipa tuuuu. Hata ukikatwa mwaka mzima,itajulikana ulikuwa umelala lakini utalipa tuuuu
 
“Ipo siku mtanikumbuka, sio kwa mabaya yangu; bali mazuri yangu” JPM.

Inabidi upate changamoto ujue tofauti ya jambo jema na baya.

Miaka mitano ya umeme wa uhakika halafu muhusika wa usimamizi wanasiasa uchwara walikuwa wanadai anaua biashara na uchumi.

Halafu hawa wanaouwa biashara na tuzo wanapewa na mafisadi,

Nchii kufuata mkumbo wa wanasiasa kwa hoja zao za majungu utajikuta pabaya sana, wakati wanufaika ni wengine kabisa.

RIP Magufuli
Unakosea ku - generalize mambo.

Si kwamba Hayati JPM alikuwa mbaya totally. Alikuwa na uzuri wake kwa kiasi kikubwa sana. Lakini pia alikuwa na ubaya (udhaifu) wake mkubwa pia.

Mathalani, kwenye eneo hili la umeme alikuwa mzuri. Lakini huwezi kujenga uchumi wa nchi kwa kuangalia na kutilia mkazo push factor moja tu ya kiuchumi..

Lakini, ni kweli pia alikuwa anapiga vita sana watu wenye fedha (matajiri) kwa dhana kwamba ni wezi na mafisadi..

Na kwa kutumia dhana hii (ya kudhani tu), wasaidizi wake serikalini wakautumia mwanya huu kumuonea na kumnyang'anya fedha yeyote na sio kwamba ziende serikalini kama mapato bali ziliingia kwenye mifuko binafsi ya viongozi hawa. Huu ndiyo tuliuita ujambazi au wizi wa kidola....

Liko eneo jingine ambalo Hayati Rais JPM alivurunda sana - Eneo la ujenzi wa demokrasia huru, na ya ushindani wa haki...

Nadhani ni kwa sababu ya asili yake ya ubinafsi mkubwa na ulafi wa madaraka aliokuwa nao tangu akiwa mbunge kule Chato na hivyo kufanya kuwa kiongozi mwoga na asiyejiamini.. Kiongozi mwenye sifa na tabia hizi siku zote akipewa madaraka makubwa, huishia kuwa dikteta tu. Ndivyo alivyokuwa huyu ndugu yako...

Mimi binafsi, mwanzoni mwa utawala wake kati ya 2015 hadi 2017 nilikuwa nampenda sana pamoja na mapungufu yake by then....

Lakini nilikuja kumdharau na kumuona kumbe ni kiongozi mmoja mjinga na mpumbavu aliyepindukia pale serikali yake ilipofanya jaribio la kumuua mwanasiasa machchari na mkosoaji mkubwa wa utawala wake pamoja chama kinachoongoza serikali hata sasa CCM ndugu Tundu Antipasi Mughway Lissu wa CHADEMA..

Watu huuliza Kuna uthibitisho gani kuwa Rais na serikali yake walihusika?

Daima hili swali huwa linatoka kwa wajinga na wapumbavu pekee wasioweza kutumia vyema vichwa vyao vyenye akili kufikiri na kuchakata mambo...

Ushahidi kuwa Hayati Rais JPM na serikali yake wanahusika ni wao wenyewe (serikali) kwa kutumia mamlaka za uchunguzi kushindwa kujisafisha na tuhuma hizi kwa serikali kufanya uchunguzi makini na wa wazi kwa kila mtu wa tukio hilo baya kabisa kwa mwanasiasa na mbunge wa kaliba ya Tundu Lissu kupigwa risasi zaidi ya 35 mchana kweupe ktk maeneo ya viongozi tena akitoka kazini...

Yaani hakuna uchunguzi wowote mpaka sasa kwa visingizio lukuki visivyo na vichwa wala miguu...!!

Ktk mazingira haya, ni nani mwenye akili timamu anaweza kuwa na shaka na uhusika wa Rais na serikali yake..?

Honestly, mimi, tangu wakati huo hajawahi kuwa moyoni mwangu regardless alifanya nini..!
 
Unakosea ku - generalize mambo.

Si kwamba Hayati JPM alikuwa mbaya totally. Alikuwa na uzuri wake kwa kiasi kikubwa sana. Lakini pia alikuwa na ubaya (udhaifu) wake mkubwa pia.

Mathalani, kwenye eneo hili la umeme alikuwa mzuri. Lakini huwezi kujenga uchumi wa nchi kwa kuangalia na kutilia mkazo push factor moja tu ya kiuchumi..

Lakini, ni kweli pia alikuwa anapiga vita sana watu wenye fedha (matajiri) kwa dhana kwamba ni wezi na mafisadi..

Na kwa kutumia dhana hii (ya kudhani tu), wasaidizi wake serikalini wakautumia mwanya huu kumuonea na kumnyang'anya fedha yeyote na sio kwamba ziende serikalini kama mapato bali ziliingia kwenye mifuko binafsi ya viongozi hawa. Huu ndiyo tuliuita ujambazi au wizi wa kidola....

Liko eneo jingine ambalo Hayati Rais JPM alivurunda sana - Eneo la ujenzi wa demokrasia huru, na ya ushindani wa haki...

Nadhani ni kwa sababu ya asili yake ya ubinafsi mkubwa na ulafi wa madaraka aliokuwa nao tangu akiwa mbunge kule Chato na hivyo kufanya kuwa kiongozi mwoga na asiyejiamini.. Kiongozi mwenye sifa na tabia hizi siku zote akipewa madaraka makubwa, huishia kuwa dikteta tu. Ndivyo alivyokuwa huyu ndugu yako...

Mimi binafsi, mwanzoni mwa utawala wake kati ya 2015 hadi 2017 nilikuwa nampenda sana pamoja na mapungufu yake by then....

Lakini nilikuja kumdharau na kumuona kumbe ni kiongozi mmoja mjinga na mpumbavu aliyepindukia pale serikali yake ilipofanya jaribio la kumuua mwanasiasa machchari na mkosoaji mkubwa wa utawala wake pamoja chama kinachoongoza serikali hata sasa CCM ndugu Tundu Antipasi Mughway Lissu wa CHADEMA..

Watu huuliza Kuna uthibitisho gani kuwa Rais na serikali yake walihusika?

Daima hili swali huwa linatoka kwa wajinga na wapumbavu pekee wasioweza kutumia vyema vichwa vyao vyenye akili kufikiri na kuchakata mambo...

Ushahidi kuwa Hayati Rais JPM na serikali yake wanahusika ni wao wenyewe (serikali) kwa kutumia mamlaka za uchunguzi kushindwa kujisafisha na tuhuma hizi kwa serikali kufanya uchunguzi makini na wa wazi kwa kila mtu wa tukio hilo baya kabisa kwa mwanasiasa na mbunge wa kaliba ya Tundu Lissu kupigwa risasi zaidi ya 35 mchana kweupe ktk maeneo ya viongozi tena akitoka kazini...

Yaani hakuna uchunguzi wowote mpaka sasa kwa visingizio lukuki visivyo na vichwa wala miguu...!!

Ktk mazingira haya, ni nani mwenye akili timamu anaweza kuwa na shaka na uhusika wa Rais na serikali yake..?

Honestly, mimi, tangu wakati huo hajawahi kuwa moyoni mwangu regardless alifanya nini..!
Hakuna binadamu mwenye chembe ya uungwana atakae support alichokipata Lissu.

But then Lissu hajui boundaries za siasa za ushindani na national interest issues.

Linapokuja swala la national interest wanasiasa wanatakiwa wafahamu hata kama hawakubaliani na mbinu za serikali; ukosoaji katika ya vita hiyo sio jambo la busara.

Sasa hivi Lissu ni kama diaspora ana muda mwingi wa kufuatilia siasa za EU nadhani anaona mipaka ya wenzake. Ingekuwa viongozi wa EU na US wapo free kuongelea swala la mgogoro wa GAZA hizo nchi zao serikali zisingekuwa na support kuachia kinachoendelea huko. Lakini kwakuwa ni moja ya national interests zao ku-support uwepo wa taifa la Israel uwezi kusikia viongozi wanakosoa kinachoendelea huko.

Same thing siku serikali moja huko ikitaka kuitandika nchi kama Tanzania kwa kitu wanachoita protection of their interest, either sababu zao ni legit or not, uwezi kusikia wanasiasa wa chama chochote huko wanapinga.

France ilipokataa kubariki air support kwenye invasion ya Libya; kilichofuata ni kutengwa kwa muda kiasi na baadhi ya nchi hasa US kwa kuwekawa ban ya baadhi imports zao.

Ni hivi wanasiasa wanatakiwa kuelewa mipaka yao kwenye maswala ya national interest ukishaonywa na serikali achana na jambo fulani wewe usikii basi kubali na potential consequences zake; uamini tafuta waathirika wanao jifanya kutoa siri za mbinu chafu zinazotumiwa na intelligence services kinyume na sheria uone huwa wanafanywa nini US, au kilichomkuta Dr Kelly mtaalamu wa nuclear U.K. aliekuwa aking’ang’ania hakuna ushahidi wa nuclear weapons in Iraq.

Kuelewa mipaka ya siasa na national interest ni jambo muhimu sana, vingine kawaida huwa kuna madhara ukikaidi popote duniani.
 
Yaan hili linchi sijui lina viongozi wa aina gani , hawawajibiki kabisaa , waziri wa nishati hajatia muongozo wowote kwenye swala la umeme kukatika katika hivi ,mwanzo walisema maji sasa sahizi maji mengi tu sijui wanasema nini maana hatujawahi kumaliza saa 24 umeme upo.
Wanasemsingizia mwendazake anzio tare 21 mpka leo eti mitambo haikufanyiwa maintenance
 
Kwamba hutofanyaje? Penda usipende utalipa tuuuu. Hata ukikatwa mwaka mzima,itajulikana ulikuwa umelala lakini utalipa tuuuu
Aisee nakuhakikishia nitakuwa mkwepa kodi namba mbilo baada ya Mo
 
Back
Top Bottom