Hapa naomba ufafanuzi kidogo maana naona Sasa hivi tuliokuwa kwenye matumizi madogo yani wale tuliokuwa tunanunua umeme wa elfu 9 units km 73 hivi kwa mwezi Sasa mmetuhamishia matumizi makubwa..shida ni Nini?Hakuna mabadiliko yeyote yaliyotokea kwenye tarif bali ni utekelezaji wa miongozo iliyopo toka mwaka 2016.Wateja wote wanawekwa kwenye makundi yanayoendana na matumizi yao
Kigezo cha kuendelea kuwa kundi la tarif 4 ni wastani wa matumizi yasiyozidi unit 75 kwa miezi mitatu mfulululizo, nyumba iwe ya makazi na iwe kijijini.Hapa naomba ufafanuzi kidogo maana naona Sasa hivi tuliokuwa kwenye matumizi madogo yani wale tuliokuwa tunanunua umeme wa elfu 9 units km 73 hivi kwa mwezi Sasa mmetuhamishia matumizi makubwa..shida ni Nini?
Eneo gani haswa? Wilaya na namba ya simu tafadhaliUmeme unakatika hovyo mno,tofauti wa wakati wa JPM.
Tanesco wanakera.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili swala la tarrif 4 lazima nyumba iwe kijijini mmechemka sio wote wanao kaa eneo la mji ni matajili, mnatugawa bila sababu, na sidhani kama ni sababu ya msingiKigezo cha kuendelea kuwa kundi la tarif 4 ni wastani wa matumizi yasiyozidi unit 75 kwa miezi mitatu mfulululizo, nyumba iwe ya makazi na iwe kijijini.
Ufafanuzi zaidiHili swala la tarrif 4 lazima nyumba iwe kijijini mmechemka sio wote wanao kaa eneo la mji ni matajili, mnatugawa bila sababu, na sidhani kama ni sababu ya msingi
Ingekuwa vyema utupie hapa walaka rasmi wote tuuoneUfafanuzi zaidi
Lalamiko la aina yako lilitolewa ufafanuzi na Mahakama kuu ya Tanzania kupitia lalamiko la mteja wetu hivyo lipo kisheria kupitia hukumu husika
Mnapata mwanga mbadala@TANESCO mnashindwa kutambua kwamba, mwenge unapopita sehemu au mkoa wowote ule ni kama Rais wa Tanzania kapita eneo hilo?
Tanesco katika mkoa wa Mwanza, ukiacha tabia hii ya siku ya Leo kukata umeme bila taarifa tena ukizingatia mwenge unakagua miradi ya maendeleo ni dharu kwa niaba ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ni kitendo cha kudharau mamlaka hiyo.
Jitahidini mnapopigiwa simu muwahi kufika eneo la tukio na kutatua tatizo mapema iwezekanavyoUfafanuzi zaidi
Lalamiko la aina yako lilitolewa ufafanuzi na Mahakama kuu ya Tanzania kupitia lalamiko la mteja wetu hivyo lipo kisheria kupitia hukumu husika
Tunakuomba radhi sana mpendwa mteja wetu, tafadhali tujulishe kama umeshapata huduma au bado, eneo gani? Wilaya namba ya simu na namba ya taarifaJitahidini mnapopigiwa simu muwahi kufika eneo la tukio na kutatua tatizo mapema iwezekanavyo
Jana katika mtaa wangu tulikua na hitilafu ya umeme kua mdogo tangu asubuhi tumetoa taarifa mara3 na usiku ndo wamerekebisha
Sasa ukiangalia hasara tuliyoipata hapo sio kidogo kazi za watu kudorora na vitu kwa friji kuharibika. Jirekebisheni kwakweli. Sio tabia nzuri hii
Hii nchi bhana!Tunakuomba radhi sana mpendwa mteja wetu, tafadhali tujulishe kama umeshapata huduma au bado, eneo gani? Wilaya namba ya simu na namba ya taarifa
Nawadai Unit Zangu Umeme WA TSH. 20,000 mlinipa Token Feki Tokea Mwezi WA 5! Nimetoa taarifa Tanesco ila mpaka Leo Kimyaaa, huo umeme ni mwingi mno kusamehe, sio haki.Tunakuomba radhi sana mpendwa mteja wetu, tafadhali tujulishe kama umeshapata huduma au bado, eneo gani? Wilaya namba ya simu na namba ya taarifa
TANESCO wilaya ya Mwanga, Kata ya Lenbeni, Mtaa wa Kisangara kijiji cha Chanjale leo ni siku ya nane kuna nyumba zaidi ya 10 hazina umeme, sababu meter zimegoma kusoma umeme unaonunuliwa, Kila wakipigiwa simu wanadai watakuja mchana .SABABU ZINAZOWEZA KUSABABISHA KUKATIKA KWA UMEME
1. Utangulizi
Kwa muda mrefu kumekuwa na uelewa kutoka kwa wateja wetu kuwa kila umeme unapokatika TANESCO WAMEKATA. Nimeona ni vyema tukatoa
Maelezo kwa ufupi ili wateja wetu waelewe sababu za kiufundi na zisizo za kiufundi, zilizo ndani ya uwezo wa TANESCO na zisizo ndani ya uwezo wa TANESCO.
2. Sababu za TANESCO Kukata Umeme
TANESCO itakata tu umeme endapo kuna sababu zifuatazo BILA kuwataarifu wateja:-
a) Kuna mali inaungua (Mf. nyumba, kiwanda au mtambo)
b) Kuna mtu kanaswa na umeme.
c) Dharura emergencies (imeelezwa hapo chini namba 4)
3. TANESCO itakata umeme baada ya kuwataarifu wateja - Planned Interruptions endapo:-
a) Kuna matengenezo Kinga yaliyopangwa kufanyika ili kuimarisha miundombinu Planned Preventive Maintanance (Mf. Kubadili nguzo zilizooza, kubadili waya chakavu, kubadili transfoma ili kuongeza uwezo wa umeme nk)
b) Matengenezo ya kila mara Routine Maintanance (Mf. Kukata miti inayogusa line za umeme, kukagua vikombe na vifaa vingine kwenye line)
c) Kumuunga mteja mkubwa kwenye line ya msongo mkubwa wa umeme 11kV au 33kV
4. SABABU zinazoweza kusababisha umeme kukatika kwa dharura Emergency cases nyingi ni Unplanned Interruptions
a) Za kiasilia Natural Calamities (Mf. Radi kupiga transfoma, mvua au upepo mkali kuangusha nguzo, kukata waya, miti au minazi au matawi ya miti kuangukia line, mafuriko, wanyama kama komba, nyani, nyoka, kunguru kunasa kwenye mifumo ya umeme nk.
b) Hujuma za kibinadamu Sarbotage
(Mf. Transfoma kuibiwa mafuta, kuibwa nyaya za umeme, nguzo kuchomwa moto na kuanguka, nguzo kubwa kuibiwa vyuma na kuanguka, magari kugonga nguzo za umeme na kuanguka, malori marefu kwenda juu kukata waya za umeme, wateja kukata miti ikaangukia kwenye line nk.
Hizi ni baadhi tu ya sababu za msingi zinazoweza kusababisha umeme Kukatika. Hivyo ieleweke kuwa sio kila KUKATIKA KWA UMEME -TANESCO wamekata ni suala pana linalohitaji kujua sababu. Wakati mwingine kwa maelezo hayo hapo juu, Umeme unakatika hata TANESCO inabidi kufuatilia mifumo ili kujua sababu za kukatika.
5. Hitimisho
Tunajua jukumu la TANESCO ni kuhakikisha wateja wanapata umeme wa uhakika, pia ni ukweli kuwa mifumo mingi ya TANESCO ni ya muda mrefu hivyo inahitaji ukaratabati wa mara kwa mara na uwekezaji mkubwa ambao sote tumeona jitihada zinazofanywa na Serikali ili TANZANIA iwe na umeme wa uhakika.
Tunaomba umma uelewe sababu hizi na kuwa kama viongozi tunaamini hakuna mfanyakazi wa TANESCO anaweza kulihujumu Shirika kwa kukata umeme bila sababu au kukata umeme bila kufuata maagizo na utaratibu wa kukata line uliowekwa. Sio kila mfanyakazi au fundi anaweza kukata umeme. Upo utaratibu tena wakati mwingine wa kimaandishi unaompa fundi ruhusa, kabla ya kukata umeme. Kama yupo na anafahamika ( Kama baadhi ya wateja wetu wanavyotuhumu) tunaomba ushirikiano wenu ili tuweze kumshughulikia kwa taratibu za kisheria na tutakuwa tumelisaidia Shirika na serikali kwa ujumla.
TANESCO
Tunayaangaza Maisha Yako
[emoji120][emoji120][emoji120]
Nyinyi tanesco Hamna ofa za unit Kama Watoa huduma za simu wanavyofanya!!! Au kwa kuwa Hamna hushindani wa kibiashara????Nyumba ipo eneo gani haswa Tanga? Ni ni makazi au biashara?
Ndugu mpendwa Mteja wetuSisi Mkoa wa Njombe leo siku ya pili mfululizo umeme unakatwa saa9am unarudi saa18pm hakuna cha Tangazo la kukata umeme wala nini
Kero tupu
Ndugu mpendwa Mteja wetuTANESCO wilaya ya Mwanga, Kata ya Lenbeni, Mtaa wa Kisangara kijiji cha Chanjale leo ni siku ya nane kuna nyumba zaidi ya 10 hazina umeme, sababu meter zimegoma kusoma umeme unaonunuliwa, Kila wakipigiwa simu wanadai watakuja mchana .
Miongoni mwa waathirika ni Taasisi za Shule na Vyuo.
Je mnalizungumziaje hili?
Mimi naomba namba ya Manager wa Mkoa tu maana sio kwa mateso haya.
Vyakula kwenye fridge vinaoza,
Wengine wanashindwa kupika kwa kutumia majiko ya umeme
Kupiga pass nguo kunashindika
Monthly subscription za TV na internet majumbani zinaisha
Tunaingia hasara.
Write your reply
Taarifa kama hizo siwezi tuma hapa public labda kama PM.Je unalalamikia eneo gani haswa?Wilaya gani na namba yako ya simu kwa hatua zaidi
Jm
Tumeangalia hatukuona tuma tafadhaliTaarifa kama hizo siwezi tuma hapa public labda kama PM.
Lakini still PM hua hamujibu jumbe.
Njombe mjini hakuna umeme wanakata asubuhi na kurudisha jioni tangu jana Mpaka hapa ninavyoandika hapa hakuna umeme.Ndugu mpendwa Mteja wetu
Tafadhali tusaidia taarifa kamili ili tuweze kufanyia kazi taarifa zako
Jina
Eneo
Wilaya
Namba ya simu
Tatizo
Toka lini
Ahsante sana
TANESCO Huduma kwa Wateja, JM