Tanesco wamenipa ajira hewa, wanasheria mnasemaje juu ya hili?

Wa kusoma

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2011
Posts
3,454
Reaction score
2,975
Wanajamvi nina kijana wangu alifanya interview ya kazi TANESCO, kama kawaida majibu yanafuata bgaadae. Baada ya wiki mbili kijana wangu alitumiwa barua iliyosainiwa na meneja wa Tanesco ikimpa hongera zake amefaulu interview na kumwaarifu kuwa asubiri pindi taratibu za ajira zitakapokamilika ataitwa akasaini mkataba.
Hiyo ilikuwa ni June, sasa mpaka leo hawa jamaa wako kimya na huyu kijana nikimwambia afanye application sehemu nyingine anakataa eti tayari ana baru ya TANESCO kwamba tayari ni mfanyakazi wao. Naombeni wadau sheria inasemaje juu ya jambo hilo? mwanangu asikae tu anasubiri ajira kumbe hakuna.
 
Du! Mfanayakzi wao wakati haja sign mkataba wa ajira!!!!
 
umepiga simu? wanasemaje? atakuwa amepotea kwenye mchakato somehow.
 
Du! Mfanayakzi wao wakati haja sign mkataba wa ajira!!!!

Ngoja tuone wanasheria watusaidie hasa masuala ya mikataba japo nafahamu kumtangazia mtu direct offer ni sawa na kuingia nae contract hata kama hujaanguka signature moja kwa moja na anaweza akademand damages kwa offer hii aliyopewa na TANESCO japo inabidi awe na proof kuwa kweli walikuwa ni TANESCO na sio makanjanja tu wa mjini........somebody can prove wrong haka ka elementary sheria nilikokasoma
 
Ukiona hivyo kazi imeshauzwa kwa mtu mwingine.
 
Alifanya interview Tanesco makao makuu ya mkoa Iringa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…