Tanesco yafilisika!!!


teh teh bora life tu bana..halina faida..Engineer toka lini anweza kuwa na business mind..ye anawaza kusimika nguzo na kilovott za umeme sio kukkaa ofisini ...acha life tutumie vibatari
 
Nini kufilisika bora ife kabisa tuanze moja maana Hili Litanesco sioni hata faida yake umeme wenyewe mgao kila kukicha..aaggrrrr

Bora huo mgao , umeme umerudi wameua ka friji kangu ambako imechukua 5 years kukanunua!!:A S angry:
 
teh teh bora life tu bana..halina faida..Engineer toka lini anweza kuwa na business mind..ye anawaza kusimika nguzo na kilovott za umeme sio kukkaa ofisini ...acha life tutumie vibatari

Du taratibu kaka!!! yaani Engineers hawana business mind? :A S angry:
 
... guy is a good CEO na Tanesco wengi wanamlilia.
Mkuu, ulitegemea wafanyakazi wa TANESCO watamponda? Kipimo cha kukubalika ni kauli za wafanyakazi wa TANESCO? Hukuona Chenge et al walivyopokelewa kwa maandamano majimboni mwao baada ya 'kujiuzulu'? Unadhani mafisadi ni wajinga kiasi kwamba watakuwa wanakula peke yao tu bila kugawa mkate kwa wachache wanaowazunguka?
 
Km TANESCO haikopesheki inamaana serikali haipokesheki maana ni Taasisi ya Serikali. Otherwise ni blah blah. Tuwe makini na hoja zetu.

kwani ule mkopo wa usd 250ml wa serikali stanbic walikopeshwa?
 

Na je Tanesco kubreak even walifanya ufisadi au waliwaambia waliwakopesha na kuwaazima vitu kuwa wayafute madeni yao, na zile gharama za uendeshaji pia walipata bure kwa kuhonga. Sikubaliani na fallacy argument yako I am sorry inaweza kuwork katika siasa ila sio katika uendeshaji wa shirika ni fani ya watu mkuu.
 
Kama utakuwa ulisoma Creactive Accounting vizuri utaelewa,ukweli ni kwamba haya mashirika ya umma(public utility companies),huwa yana utaratibu wa kufanya ujanja katika kutengenea hesabu zao na kuhakikisha kuwa wanadisclose loss katika Financial statement zao bila kuathiri rules na regulations za financial standards..
Na hii yote ni kwa sababu watakapo wasilisha maombi kwa ajili ya kuongeza bei ya service zao(unit za umeme,maji na kadharika),ionekane kana kwamba wanajiendesha kwa loss na kuruhusiwa kuongeza viwango vyao....
Pia hasara zingine wanzozipata pia ni pamoja na serikali kuingilia utendaji wa haya makampuni ya umma kwa ajili ya kutekeleza sera za vyama tawala,kwa mfano chama fulani kimeahidi kupeleka umme kijiji fulani kwa ajili ya kujipatia kura kwa wananchi halafu ichoicho chama kikashinda lazima kitalazimisha umeme upelekwe,sasa hapo ndo hasara inapotokea.....Gharama ya kuupeleka umeme ni kubwa kuliko wato watauweka umeme piaa tutegemee kuwa mapato yatakuwa madogo,we fikiria unapeleka umeme kilomita zaidi ya 100 kwenye kiji na watu wenye uwezo wa kuweka umeme ni wachache kuna nini!!!
 

Tatizo la TANESCO sio kupandisha bei bali kuhakikisha kuwa wote wanaotumia huduma ya umeme wanalipia. TANESCO inachojua ni kukusanya bill kwa walala hoi matajiri na mifisadi na mikampuni yao hailipi bill na wao wamekaa wametoa macho. Uislam umeiangiusha TANESCO. Nchii kila inapoongozwa na mwislam ni shida tupu
 

Sasa unadhani tatizo la madeni sugu limesababishwa na Idrissa? Mbona alipowadai walilipa wengi kama sio wote na MaCEO waliopita walikuwa wanagoma kulipa yeye alifanya nini? Kwahivyo problem sio Idrissa problem ni kwamba wengi wenu humu mnamchukia Idrissa kwakuwa muislamu tu nothing else mnamhusisha ambazo hauhusiki nazo kutokana na chuki zenu dhidi ya uislamu. Likewise, chuki na kulewa kwenu kwa kuuchukia uislamu unawafanya mpaka msione mazuri aliyoyafanya Idrissa. Haya sasa kachaguliwa mwenzenu shirika linamfia mkononi sijui mtasema nini?
 

Kaka problem ya Creative Accounting ipo mpaka katika ulimwengu ulioendelea. Ila creative accounting ina mabaya na mazuri yake na hii inasababishwa na kwamba accounting practices and principles zilizowekwa zina weakness na wahasibu, na maceo wanatumia hizo loopholes kujustify their actions. But saa zengine tupime jambo kwa uzito wake. Shirika linaelemewa na mzigo wa gharama za uendeshaji lakini mnataka mapato yake yabakie constant inawezekana vp? Mbona bei ya mafuta Ewura imeshindwa kuizuia mpaka sasa mafuta yanauzwa sehemu nyengine 2,000. Mbona Sumatra imeruhusu nauli za daladala zipande lakini gharama ya umeme ibakie hapo hapo kama vile gharama na supply ya vipuri vya umeme ni inelastic please!!!!! Wacha life tu shirika, Tanesco, ATCL na mengineyo kwasababu tatizo siasa imetawala kila mahali
 
Mimi binafsi nimeongea kwa mara nyingi na wafanyakazi wa TANESCO wa level mbali mbali (ma engineer, hesabu ...). Hii inatokana na kazi yangu ninayofanya ambayo nakuwa karibu nao.

Kwa kweli walimsifia Idriss kwa uendeshaji wake na kama alivyosema Mdondoaji nilishasikia hiyo ya shirika kubreak even kwa mfanya kazi mmoja aliniambia hiyo.

Na iliyonisukuma niamini zaidi ni kwamba hao walioniambia hivyo siyo wa dini moja tu na wala sio wa kabila moja tu.

Tatizo ni kwamba siasa na majungu ndivyo vinavyotawala kwenye maamuzi na sio muelekeo wa shirika kibiashara. Idriss alikuwa jeuri na aliweza kusimama kidete kwenye maamuzi anayoyaamini na hii ndiyo ilimletea matatizo na hao mabosi wakubwa.

Tusisahau kwamba na sisi wengine tunaoiba umeme tunachangia kuliua shirika halafu tuko mstari wa mbele kunyooshea vidole mafisadi.

I have no data to confirm my analysis though!
 
Tatizo lako ume-base kwenye udini, hakuna mafanikio ya kujivunia toka kwa Idrisa labda kama una takwimu tutakuelewa ila kwa taarifa yako shirika lilifilisika mapema kabla Idrisa hajaachia ngazi, mkopo wa zaidi ya usd 200mil wakati wa Idrisa ulitumika kinyume na malengo yaliyokusudiwa pia matumizi makubwa ya mkurugenzi (ukarabati wa nyumba, ununuzi wa magari na generator kubwa 25kva kwa matumizi ya nyumbani) yamechangia kulifilisi shirika, usifikiri taarifa hii ya kufilisika ni kwa miezi michache ya uongozi wa mkurugenzi mpya.

Zinduka mwanangu wapo waislamu ni watendaji wazuri, pia wapo wakristo hata wapagani watendaji wazuri lengo hapa ni tija wala si udini.
 
tehe TWIGA MNYONGE chali! kampuni inaendeshwa na wana siasa mnadhania itaishi kweli. mie naona tunachezea muda tu na resources bora waTanzania wapate ajira pale walipwe mishahara siku zinakwenda. kuna mama mmoja alikuwa bosi wa ma receptionist pale tanesco makao makuu siku hizi namsikia eti meneja wa hiyo tanesco sijui morogoro dah nimasema tutafika secretary anakuwa meneja tena wa tanesco hahahahaaaa twigaaaaaaaaaa.
 

unsubstantiated argument mie nimekupa one example when Tanesco ila break even isipokuwa wakati wa mzee Kasambala? Tatizo ni udini unawasumbua watu wanaomchukia Idriss I beg to differ my friend. Kama ulivyosema kuna watendaji wazuri wakristo na waislamu na mmoja katika watendaji wazuri ni huyu mzee.

Bitikongowe amesema hapo tatizo jamaa labda ana principles zake ambazo sio wote wanaozipendelea lakini mie naweza kuitazama vile vile kwa upande mwengine kama isingelikuwa principles je wadaiwa sugu wangelipa? Sometimes it is better to be bold so that message iwafikie walengwa.
 
Mimi naomba niongee kwa ushaidi,kwani haifai kuzungumza kupitia magazeti..............Ukweli ni kwamba,wakati Idrisa Rashidi anakabidhiwa kuongoza hili shirika lilikuwa na hasara ya bil 25, na mpaka anaondoka madarakani alifanikiwa kupunguza hasara mpaka kufikia bilion 5 (round figure).
Na hii yote imetokana na juhudi zake binafsi pamoja na taaluma yake kama mchumi,wakati kwa kipindi cha nyuma shirika lilikuwa likiongozwa na Wakurungenzi ambao wenye taaluma ya Engineering....kiufupi IDRISSA alijitahidi sana kuliweka shirika katika hali nzuri ukiondoa binadamu hawezi kuwa makini 100% matatizo madogomadogo yapo kama binadamu..
 
Hivi shirika kama hili litafilisikaje wakati kuna wateja maelfu kwa maelfu hata kufungiwa umeme bado na wanalia sana?
 
Hivi shirika kama hili litafilisikaje wakati kuna wateja maelfu kwa maelfu hata kufungiwa umeme bado na wanalia sana?

Swali zuri sana hilo but jiulize jibu utalipata wapi? Chunguza utendaji wa Tanesco na mfumo wa Tanesco ndio utaona haliweza kukwamuka kiutendaji. Idrissa aliliona hilo ndio maana akawa anajaribu kulibadilisha liwe linajiendesha kibiashara na kifaida zaidi lakini mfupa umemshinda je mtu mwengine atauweza?
 
Wacha lifilie mbali,na yaje makampuni mengine kama ilivyo kampuni za simu ,ukiritimba uliota matende kwenye hilo shirika,bora tujue hatuna shirika kuliko kudanganyana,
 
wrong...

  1. kabla ya bei ungeangalia efficiency ya shirika
  2. ungeangali procurement function ya tanesco halafu uniambie
  3. ungeangali na kutafakari kama lile shirika lingekua binafsi kama wangefeli
  4. ungejaribu kujifunza infuence ya government na hasa vilele vitoto viwili (viwaziri) kwenye kurudisha nyuma tanesco
  5. ungecheki admin approach
  6. ungeangalia possibility ya decentralization
  7. ungehoji kwa nini tanesco ina siasa sana na kila kiongozi ana kamdomo pale wakati maji wali-decentralize

Ukimaliza ndo uje na hilo lako la bei

nyie ndio unidirectional ambao unadhani dawa ya joto ni kuvua shati tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…