TANESCO yatangaza maboresho ya Mita za LUKU, soma ujue jinsi ya kuingiza Token upya kuanzia Juni 1, 2024

TANESCO yatangaza maboresho ya Mita za LUKU, soma ujue jinsi ya kuingiza Token upya kuanzia Juni 1, 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760




MABORESHO YA MITA ZA LUKU KWA WATEJA WA TANESCO KANDA YA ZIWA NA KANDA YA MAGHARIBI

Jumatatu, 27 Mei 2024
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa mikoa ya Mwanza, Kagera, Mara, Geita, Simiyu, Tabora, Katavi na Shinyanga kuwa zoezi la maboresho ya mfumo wa LUKU litaanza kufanyika katika mikoa hiyo kuanzia tarehe 01 Juni 2024.

Lengo la mabadiliko haya ni kuendana na viwango vya mifumo ya LUKU vya kimataifa na kuongeza ufanisi wa mita za LUKU.

Mteja anaponunua umeme atapokea tarakimu kwenye makundi matatu, kila kundi likiwa na tarakimu ishirini. Mteja ataingiza tarakimu za kila kundi kwa mfuatano unaosomeka kwenye risiti ya malipo au ujumbe mfupi wa simu (sms). Makundi mawili ya tarakimu yatakuwa kwa ajili ya maboresho na kundi moja la umeme ulionunuliwa.

Zoezi hili ni bure na litafanyika mara moja tu kwa mteja, baada ya kufanya hivyo mteja atakuwa amefanya mabadiliko hayo na ataendelea kupata kundi moja la tarakimu ishirini kila anapofanya manunuzi ya umeme.

Baada ya mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi zoezi litaendelea kwa mikoa mingine nchini kwa awamu tofauti, kadri Shirika litakavyotangaza kwa umma na mwisho wa zoezi hili nchini ni tarehe 24 Novemba 2024.

Kwa taarifa zaidi wateja wanaweza kuwasiliana nasi kupitia namba ya huduma kwa wateja 0748 550 000, namba za huduma kwa wateja kwa mikoa husika, namba ya WhatsApp 0748 550 000 au mitandao yetu ya kijamii.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA
TANESCO- MAKAO MAKUU
DODOMA
 
TANESCO waseme tu Ukweli, kuwa wanabadili Tariffs. Hapa tutegemee ongezeko la ulaji wa umeme kwa kupokea units pungufu.

Vinginevyo watuambue huo mfumo wa kimataifa wanataka tu archive Nini speciasificaly kama watanzania?
 
Unaingiza makundi yote matatu ndiyo unagonga ENTER/OK au kila kundi na OK yake?
 

MABORESHO YA MITA ZA LUKU KWA WATEJA WA TANESCO KANDA YA ZIWA NA KANDA YA MAGHARIBI

Jumatatu, 27 Mei 2024
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu wateja wake wa mikoa ya Mwanza, Kagera, Mara, Geita, Simiyu, Tabora, Katavi na Shinyanga kuwa zoezi la maboresho ya mfumo wa LUKU litaanza kufanyika katika mikoa hiyo kuanzia tarehe 01 Juni 2024.

Lengo la mabadiliko haya ni kuendana na viwango vya mifumo ya LUKU vya kimataifa na kuongeza ufanisi wa mita za LUKU.

Mteja anaponunua umeme atapokea tarakimu kwenye makundi matatu, kila kundi likiwa na tarakimu ishirini. Mteja ataingiza tarakimu za kila kundi kwa mfuatano unaosomeka kwenye risiti ya malipo au ujumbe mfupi wa simu (sms). Makundi mawili ya tarakimu yatakuwa kwa ajili ya maboresho na kundi moja la umeme ulionunuliwa.

Zoezi hili ni bure na litafanyika mara moja tu kwa mteja, baada ya kufanya hivyo mteja atakuwa amefanya mabadiliko hayo na ataendelea kupata kundi moja la tarakimu ishirini kila anapofanya manunuzi ya umeme.

Baada ya mikoa ya Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi zoezi litaendelea kwa mikoa mingine nchini kwa awamu tofauti, kadri Shirika litakavyotangaza kwa umma na mwisho wa zoezi hili nchini ni tarehe 24 Novemba 2024.

Kwa taarifa zaidi wateja wanaweza kuwasiliana nasi kupitia namba ya huduma kwa wateja 0748 550 000, namba za huduma kwa wateja kwa mikoa husika, namba ya WhatsApp 0748 550 000 au mitandao yetu ya kijamii.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA
TANESCO- MAKAO MAKUU
DODOMA
Acheni usumbufu kwa wayeja nyinyi viumbe, na huo umeme wenu unaokata kata hovyo.
 
TANESCO waseme tu Ukweli, kuwa wanabadili Tariffs. Hapa tutegemee ongezeko la ulaji wa umeme kwa kupokea units pungufu.

Vinginevyo watuambue huo mfumo wa kimataifa wanataka tu archive Nini speciasificaly kama watanzania?
Achieve na siyo archive
 
Kwakweli apa tujiandae kupigwa....
Mnatuambia Umeme upo mwingi Sana mpaka mna plan ya kuuza nje ya nchi, so kwanini wasipunguze bei za units Watanganyika waweze kuenjoy Umeme kwa gharama ndogo...?
 
Mbona mlolongo mrefu hivyo?? Tarakim 60? Zilizopo zenyewe nilikuwa naona tabu kuziingiza sasa hizi 60 itakuwaje?
 
Tanesco wametoa maaelezo pungufu na kuwaacha watanzania hewani maana Hakuna anayejua haya maboresho yana athari gani au faida gani kwa mlaji.
Tutulie dawa ituingie..
 
Back
Top Bottom