Kituo ndio kina gharama hizo na sio mitambo. Katika tenda dokumenti bei haitajwi kwani wanaomba kusupply hutaja bei zao na mnunuzi huchagua amba bei ya chini na mtambo bora au mtambo bora na bei ikawa juu. Umenipata? Hiyo 120m usd ni gharama za mradi mzima!
Hii kampuni ya Noor Oil ina uhusiano wowote na huyu Al Noor hapo chini aliyeshughulikia suala la gesi ya Songo Songo kabla JK hajakabidhiwa mikoba ya suala hilo pale Wizara ya Nishati?
In Africas Winds of Change: Memoirs of an International Tanzanian, the former Minister responsible for Energy, Al Noor Kassum, documents how we ended up at the mercy of Dowans. I take the liberty to say so because it is a documentary of how we forfeited, nay, suspended an initiative that could provide us with a total capacity of 2,100 MW, 21 times more than the 100 MW from Dowans.
That initiative is what came to be known as the Stieglers Gorge Power Project. The gorge is located on the Rufiji River. According to Kassum, in 1979 they proposed to use it to generate electricity. To that end Halfslund/Norplan of Norway were consulted to prepare a feasibility study for the project.
It is this study, financed by the Norwegian government, that showed the said grand capacity then thus spaced over four phases: At the end of Phase I (1990-95) the capacity would be 300 MW; at the end of Phase II (1995-2005) it would be 900 MW; at the end of Phases III and IV (2005-15) it would be 2,1000 MW. Thus, the capacity could be stepped up as demand increased over time. This would also spread the total cost over a longer period.
Interestingly, these consultants estimated that the investment cost for all these phases would be USD 1,382 million - a mere two times the cost of Dowans plant in non real terms. They also noted that it could meet all of Tanzanias projected power needs at least until 2010. Yes, indeed, until next year.
Unfortunately, laments Kassum, we were unable to obtain financing for the project. Instead, he further laments, the Mtera Dam was built for half the cost of Stieglers Gorge project but supplied only 10 percent of the power that the other project would have made available.
His in hindsight lamentations doesnt end there. Tanesco, he laments nostalgically, spent almost the same amount that the Stieglers Gorge project would have cost on constructing many small power-generation plants that used fuel to produce electricity. So, after all, we didnt start thinking small now.
Later, Kassum winds up his regrets, Mwalimu Nyerere told me it had been a mistake not to go ahead with the Stieglers Gorge project. Had the money spent on those power stations be used on the Stieglers Gorge project, electricity could have been supplied through cables to the whole country and we would not have the frequent power shortages that continue to plague Tanzania today.
Full of hope, Kassum sums up by saying the good news is that the current Government has announced its intention to revive the Stieglers Gorge project. That was 2007. Today, two years later, in 2009, the scanty information we can gather from the meeting between Dr. Idris Rashidi and Hon. Zitto Kabwes teams is that Stieglers Gorge project among other projects have been delayed due to lack of funds etc.
Piga chini Waziri na uongozi wote wa Tanesco..........damn!
Nikweli serikali inapaswa kuwajibika..na sasa ni zamu ya Rais kuwajibika. sio waziri mkuu tena....tatizo la nchi hii kwasasa ni maamuzi mazito hayafanyiki.kwasababu Rais anataka apendwe na kila tabaka matokeo yake kila tabaka linamlaumu....wengine watailaumu tanesco, lakini tulio karibu tunajua kuwa tatizo sio tanesco, sio kweli kwamba tanesco hawana mikakati, tanesco mikakati wanayo, tatizo ni serikali haitekelezi mikakati ya kitaalamu ya tanesco na hatimaye inabidi kila wakati tanesco walazimike kuchukua hatua za dharula....ni kwasababu mikakati ya muda mrefu haitekelezwi na serikali..
Kwa jinsi hii siasa zetu zitaangamiza taifa letu.kwamba majuzi tulikataa kununua mitambo yenye mashaka kuwa ni ya watu wezi...dowans, leo nchi nzima imeingia giza...:
1.Wapo wanaosema atakumbukwa zitto kuhusu hili sio zitto peke yake, hata Ndesamburo alionya hili ndani ya tanzania daima j,pili wakati huo....Engineer stella manyanya alionya hatari ya siasa zetu katika hili alipohojiwa na gazeti la majira wakati huo...sijapata nukuu zao kwa haraka tu....lakini wabunge hawa waliweka msimamo wa kutaka nkununuliwa mitambo yenye uwezo tuweze kukabiliana na tatizo la umeme bila kujali mitambi hiyo ni ya nani....Blair ana msemo wa "change evil money into gud use"....
lakini nakumbuka wakati wa mjadala wa dowans, kuna wabunge walisema mitambo yenye uwezo wa zaidi ya ile ya dowans ingeweza kupatikana ndani ya wiki mbili tena kwa bei nafuu mara dufu kuliko hiyo ile ya dowans....sijui kama serikali au tanesco walipata msaada huo kutoka kwa wabunge,au wabunge hao waliweza kupeleka mapendekezo hayo serikalini......au zilikuwa siasa zetu za bongo za kujadili hoja with respect to aliyeitoa badala ya tatizo lenyewe.....kazi ipo!
Mimi nashindwa kujua hivi sisi tuna wadudu gani kichwani kwetu?? Hivi baada ya haya madudu yote mpaka serikali kujiuzulu mpk leo kuna matatizo ya umeme?? Jamani ndugu zangu Taifa letu nani anweza kufanya kweli kwa ajili ya kizazi hiki, inatia uchungu sana
Nikweli serikali inapaswa kuwajibika..na sasa ni zamu ya Rais kuwajibika. sio waziri mkuu tena....tatizo la nchi hii kwasasa ni maamuzi mazito hayafanyiki.kwasababu Rais anataka apendwe na kila tabaka matokeo yake kila tabaka linamlaumu....wengine watailaumu tanesco, lakini tulio karibu tunajua kuwa tatizo sio tanesco, sio kweli kwamba tanesco hawana mikakati, tanesco mikakati wanayo, tatizo ni serikali haitekelezi mikakati ya kitaalamu ya tanesco na hatimaye inabidi kila wakati tanesco walazimike kuchukua hatua za dharula....ni kwasababu mikakati ya muda mrefu haitekelezwi na serikali..
Kwa kuongezea, kwa nini serikali imeingia kwenye mikataba na IPTL, RICHMOND etc. kwa mfano pesa za richmond za mkataba $172million ( three years contract) zingeweza kununua mitambo mipya 3 ya 100MW toka GE/ROLL ROYCE/ DRESSALAND/SIEMENS etc. bahati nzuri nafanya kazi kati ya hizo kampuni hapa Ohio, gharama ya mtambo (equipment only ya 100 MW ni 30-35million) ukiongeza installation cost , shipping etc ambayo ni 25-75% ya cost ya equipment. utaona kwamba mtambo mmoja ni kati ya 50-60 million mpaka kuwashwa. juzi juzi tu Tanesco wametangaza tender ya 100MW kwa gharama ya $120million, hizi pesa zingetosha kununua mitambo 2 ya 100MW. miezi kama miwili niliongea na classmate wangu tuliyekuwa naye Colombia university ambaye anafanya kazi roll-royce internation kaniambia kuna jamaa wanaitwa noor oil ya waharabu na wahindi wamepeleka bid ya hiyo tender kwa kutumia jina la roll royce kwa haraka haraka nikamwambia huyo classmate wangu kwamba mbona hawa jamaa ni wale wa richmond wanakuja kwa sura nyingine, kwa hiyo tunasubiri tender itoke kwa kweli safari hii tutatumia international lawyer kuwafikisha hawa noor na tanesco kwenye international court ya corruption. haiwezekani mtambo wa 100mw ambao gharama yake ni 50-60million wanunue kwa 120million.
Sheria ya Umeme ya mwaka 2007 (tuliipitisha bungeni 2008) inaruhusu makampuni ya binafsi kuzalisha umeme na kusambaza umeme (upande wa kuzalisha tayari IPTL na Songas wanashiriki).
Tatizo la umeme wa Tanzania ni Transmission. Uwezo wetu wa kusambaza umeme ni mdogo sana na tuna gridi moja tu. Uwekezaji katika gridi hauwezi kuwa kwa sekta binafsi (serikali ilitika kuliberalise transmission pia, nakumbuka mimi na mzee cheyo tulikataa kata kata na tukafanikiwa). Serikali ilipaswa kuwa imejenga gridi mpya ya North-West gridi ili kusafirisha umeme kwenda kanda ya Ziwa mikoa ya Kigoma, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Kagera na Mara. Mahitaji ya umeme wa mikoa hii kwa sasa kama migodi yote ikipata umeme wa gridi ni 240MW. Kwa sasa ni mgodi mmoja tu wa Bulyanhulu ndio unapata umeme wa gridi na usio na uhakika. Hii inapelekea serikali kupaata hasara mbili.Uwekezaji wa transmission line ni uwekezaji mkubwa sana lakini unawezekana. Zinahitajika kama 700m usd kujenga grid hii mpya. Hapa serikali ndipo inapotakiwa kufanya kazi sawasawa.
- TANESCO wanakosa soko la uhakika la zaidi ya 120 MW ambapo wangeweza kuingiza zaidi ya 120bn usd kwa mwaka na hivyo kupata fedha za kusambaza umeme vijijini na mijini. Pia hii inakosesha uchumi faida ya backward linkages kati ya sekta ya nishati na sekta ya madini (backward linkage is such that a sector that gets a lot of inputs from within the country will have strong backward linkages relative to sectors that import most of their inputs from oversees). Madhara haya tunayaona hapa chini kwenye hasara ya pili;
- Serikali inatoa misamaha ya kodi ya mafuta kwa kampuni za madini ili zizalishe umeme wake wenyewe (importing inputs). Kwa mujibu wa ripoti ya Bomani Tanzania ilisamehe jumla ya 191bn Tshs katika kipindi cha 2005/06 - 2007/08. Hii pia ina madhara katika urari wa biashara na hata thamani ya shilingi ya Tanzania pale uzalishaji unapokuwa unaongezeka katika sekta ya madini.
Lakini kuna hatua za dharura zilizotakiwa kufanywa. Mojawapo ni kuwa na mtambo wa 60MW Mwanza ambao utapunguza mzigo kwenye gridi. Zabuni zilitangazwa na TANESCO toka mwezi Aprili na wazabuni kujitokeza lakini mtambo huu utaweza kufungwa na kuanza kazi mwaka 2011. Hii inatokana na taratibu za ujenzi wa mitambo kwenye viwanda. Baada ya kupata mzabuni, itabidi kuanza sasa ujenzi wa mitambo nk.
Kwa mwono wangu, matatizo ya sasa ya mgawo hayatachukua muda mrefu sana kwani mvua zitanyesha na mitambo kurekebishwa. Hata hivyo bado tutakuwa na tatizo kubwa la kanda ya Ziwa maana hata mabwawa yazalishe at 100%, kama gridi imezidiwa haitaweza kusafirisha umeme kwenda huko. Mtambo wa 60MW Mwanza ndipo unapopata umuhimu wake kwa sasa.
Kuwalaumu TANESCO sidhani kama ni sawa. Hili ni Shirika ambalo limeharibiwa sana na mikataba mibovu ambayo sio TANESCO wenyewe waliingia. Hili ni Shirika ambalo NetGroup Solution waliliingiza kaburini na ndio kwanza limetoka.
TANESCO wamejitahidi sana kwa kadiri ya uwezo wao kushugulikia suala hili kwani wao wenyewe wanajua kuwa wanapaswa kufanya kazi kwa bidii kwani wanatakiwa kubreak even mwaka 2010 ili waweze kuanza kulipa mkopo waliochukua katika taasisi za fedha. Hivyo migawo hii inawaumiza na ninajua wanaumia.
Tatizo ni commitment ya serikali katika suala hili. TANESCO waliomba 312bn kwenye bajeti ili kushughulikia masuala haya ya umeme hawakupewa kitu. Tuzingatie kuwa tuna nakisi ya 155MW za umeme kutokana na IPTL kusimama kuzalisha mpaka kesi iishe na kesi bado haijaisha.
Suala la umeme lapaswa kuangaliwa katika mapana sana. Ni kweli kuwa asilimia 12 tu ya nyumba ndio zina umeme, lakini umeme sio kwa jili ya kuwasha nyumbani tu. Umeme kwenye uzalishaji wa uchumi ni muhimu sana ili walaji wa kawaida waweze kufidiwa kwa kupata umeme wa gharama nafuu.
Ninaamini kabisa kuwa kama tukiamua kuisaidia TANESCO tunaweza kulifanya Shirika hili 'champion' wa nchi yetu. Potential zote zipo. Dhamira hakuna.
Mimi nimesoma kwa makini maoni yote yaliyotolewa katika thread hii kuhusu tatizo hili la umeme. Kama nilivyotabiri katika mjadala huu ulipojitokeza awali kuhusu athari za wanasiasa kuingilia maamuzi ya kitaalamu ya kununua mitambo ya Dowans, nilisema kuwa utapotokea mgao wa umeme, ni wale wale waliopinga ushauri ule wa busara ndio hao hao watakuwa wakwanza kulaumu. Sasa naona watu wale wale wanatoa hoja zile zile walizozitoa wakati ule.
Mimi nilimuunga sana mkono Zitto kwa uamuzi wake wa kuunga mkono ununuzi wa mitambo ya Dowans. Hivi sasa kaja tena na maelezo mazuri ya hali halisi ilivyo kuhusu nishati ya umeme badala tu ya kuilaumu Tanesco. Kama wananchi kweli wanataka Tanesco ifanye kazi yake sawasawa, basi Serikali iipe kazi mbili. Moja ya kuzalisha umeme na ya pili ya kutengeneza noti ili kila wanapotaka kununua mitambo au kujenga grid mpya basi wanazalisha noti za kiasi cha mahitaji yao. Hapo wakishindwa na mimi nitawalaumu.
Nitafurhi sana sasa katika hali hii tuliyofikia kumsikia Mh. Mwakyembe akitoa tena maoni yake kuwa ni bora nchi iingie gizani kuliko kununua mitambo ya Dowans. Ila safari hii kauli yake hiyo, ai back na tathmini ya faida na hasara zake kwa uchumi wa nchi kama alivyofanya Mh. Zitto. Asibane kimya tu au kuja na lawama zisizo na msingi za kuilaumu Tanesco.
Mimi nimesoma kwa makini maoni yote yaliyotolewa katika thread hii kuhusu tatizo hili la umeme. Kama nilivyotabiri katika mjadala huu ulipojitokeza awali kuhusu athari za wanasiasa kuingilia maamuzi ya kitaalamu ya kununua mitambo ya Dowans, nilisema kuwa utapotokea mgao wa umeme, ni wale wale waliopinga ushauri ule wa busara ndio hao hao watakuwa wakwanza kulaumu. Sasa naona watu wale wale wanatoa hoja zile zile walizozitoa wakati ule.
Mimi nilimuunga sana mkono Zitto kwa uamuzi wake wa kuunga mkono ununuzi wa mitambo ya Dowans. Hivi sasa kaja tena na maelezo mazuri ya hali halisi ilivyo kuhusu nishati ya umeme badala tu ya kuilaumu Tanesco. Kama wananchi kweli wanataka Tanesco ifanye kazi yake sawasawa, basi Serikali iipe kazi mbili. Moja ya kuzalisha umeme na ya pili ya kutengeneza noti ili kila wanapotaka kununua mitambo au kujenga grid mpya basi wanazalisha noti za kiasi cha mahitaji yao. Hapo wakishindwa na mimi nitawalaumu.
Nitafurhi sana sasa katika hali hii tuliyofikia kumsikia Mh. Mwakyembe akitoa tena maoni yake kuwa ni bora nchi iingie gizani kuliko kununua mitambo ya Dowans. Ila safari hii kauli yake hiyo, ai back na tathmini ya faida na hasara zake kwa uchumi wa nchi kama alivyofanya Mh. Zitto. Asibane kimya tu au kuja na lawama zisizo na msingi za kuilaumu Tanesco.