Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
December 12, 2018 by Global Publishers
WATU wawili wamefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa huku sita kati yao wakiwa na hali mbaya baada ya basi la Royal Classic waliokuwa wakisafiria, kuacha njia na kupinduka eneo la Kibaoni wilayani Lushoto jana Jumanne Desemba 11.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema basi hilo lilikua likisafiri kutoka Tanga kwenda wilayani Lushoto. Amedai chanzo cha ajali hiyo ni utelezi uliotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika eneo hilo.
“Majeruhi sita kati ya 21 hali zao ni mbaya na wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa matibabu zaidi,” amesema Bukombe.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema basi hilo lilikua likisafiri kutoka Tanga kwenda wilayani Lushoto. Amedai chanzo cha ajali hiyo ni utelezi uliotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika eneo hilo.
“Majeruhi sita kati ya 21 hali zao ni mbaya na wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa matibabu zaidi,” amesema Bukombe.