Tanganyika kuongozwa na Waziri Mkuu

Tanganyika kuongozwa na Waziri Mkuu

EasyFit

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
1,269
Reaction score
1,082
Imefahamika kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa Tume ya katiba kuwa kiongozi wa Serikali ya Tanganyika atajulikana kama Waziri Mkuu, vile vile kiongozi wa Serikali ya Zanzibar atajulikana kama Waziri Mkuu au anaweza kuendelea kujulikana kama Rais hii itategemea mapendekezo yao, hili litaondoa mgongano wa kuwa na marais watatu bila sababu za msingi walisema baadhi ya wajumbe waliohojiwa na Gazeti hili.

Source: Gazeti la Rai.




Alhamisi, Juni 06, 2013 06:43 Na Sarah Mossi


WAKATI wananchi wa Tanzania wakijiandaa kurejea tena kwa Serikali ya Tanganyika kama ilivyoainishwa kwenye rasimu ya Katiba mpya, kiongozi wa Serikali hiyo atajulikana kama Waziri Mkuu, Rai imebaini. Wanazuoni na baadhi ya wajumbe wa Tume ya Katiba wameieleza Rai kuwa, Katiba ya Tanganyika inayotarajiwa kutungwa, ndio itakayotamka jina la kiongozi wa nchi na kwa vyovyote vile ataitwa Waziri Mkuu, ambaye chama chake au kwa kushirikiana na vyama vingine anaweza kuunda Serikali kwa kuwa na wingi wa viti bungeni.

Wanazuoni hao wamesema nafasi hiyo ya Waziri Mkuu itaondoa ukakasi wa kuwa na marais watatu katika Serikali tatu zitakazokuwapo mara baada ya kukamilika kutungwa kwa Katiba mpya.

Rasimu ya Katiba mpya iliyotangazwa juzi na Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, imeainisha namna Jamuhuri ya Muungano itakavyokuwa yenye muundo wa shirikisho lenye Serikali tatu.

Serikali hizo ni Serikali ya Jamhuhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, huku shughuli zote za Muungano zikisimamiwa na Serikali, Bunge na Mahakama ya Jamuhuri ya Muungano.

Akizungumza na RAI, Mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba, Profesa Mwesiga Baregu, alisema Serikali ya Jamhuri ndio itakuwa na mamlaka ya juu ya Dola na itaongozwa na Rais, kama itakavyoainishwa kwenye Katiba mpya.

Profesa Baregu alisema Serikali za Tanzania Bara na Serikiali ya Mapinduzi Zanzibar zitakuwa na viongozi wao ambao watatamkwa kwenye kwenye Katiba zao.

Alisema, ingawa Zanzibar tayari inayo Katiba yake inayotamka jina la kiongozi mkuu wa nchi hiyo ambaye ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, lakini bado ipo nafasi ingawa si kwa ulazima kuwapo kwa marekebisho mengine ya Katiba ya Zanzibar, ambayo itatoa nafasi kwa Katiba kutamka jina jingine litakalopendekezwa.

Kwa upande wa Serikali ya Tanzania Bara, Profesa Baregu alisema huu ndio wakati wake wa kutunga Katiba ya nchi ambayo itatamka jina la kiongozi mkuu wa nchi.

"Kwa upande wa Zanzibar, Katiba inaweza kutamka kiongozi aitwe, Waziri Kiongozi na kwa Tanzania Bara litaweza kuwa Waziri Mkuu, hili litaondoa mgongano wa kuwa na marais watatu bila sababu za msingi.

"Ni matumaini yangu Katiba za Tanzania Bara na Zanzibar zitakazotungwa zitapata majina muafaka na kuondoa utata huo," alisema.

Mjumbe mwingine wa Tume ya Marekebisho ya Katiba kutoka Zanzibar, Ally Saleh, aliiambia RAI kuwa, upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar tayari wanayo Katiba yao inayomtaja kiongozi wake kuwa ni Rais, hivyo hakutakuwa na ulazima wa kulibadili jina la kiongozi huyo.

"Tukumbuke hatuwezi kuwachagulia Wazanzibar jina la Rais wao, tayari wanaye Rais, hii ni fursa zaidi kwa Serikali ya Tanzania Bara itakayoundwa kuamua Rais wao aitwe jina gani," alisema Saleh.

 
Imefahamika kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa Tume ya katiba kuwa kiongozi wa Serikali ya Tanganyika atajulikana kama Waziri Mkuu, vile vile kiongozi wa Serikali ya Zanzibar atajulikana kama Waziri Mkuu au anaweza kuendelea kujulikana kama Rais hii itategemea mapendekezo yao, hili litaondoa mgongano wa kuwa na marais watatu bila sababu za msingi walisema baadhi ya wajumbe waliohojiwa na Gazeti hili.

Source: Gazeti la Rai.
Hawa wajumbe wana matatizo gani? Atakavyoitwa Zanzibar ndivyo hivyo hata Tanganyika. Kama Zanzibar watabaki kuwa na Rais na sisi tunamtaka wa Kwetu Tanganyika. Hakuna kubembelezana kwa kupeana "options" hapa. Tanganyika na Zanzibar zote ni nchi zilizokubali kuungana hakuna mwenye haki ya "kudeka" mbele ya mwingine, ebo!
 
wa Zanzibar hawawezi hata siku moja kuikubali hii, yaani Zanzibar iongozwe na waziri mkuu? no way
 
Hawa wajumbe wana matatizo gani? Atakavyoitwa Zanzibar ndivyo hivyo hata Tanganyika. Kama Zanzibar watabaki kuwa na Rais na sisi tunamtaka wa Kwetu Tanganyika. Hakuna kubembelezana kwa kupeana "options" hapa. Tanganyika na Zanzibar zote ni nchi zilizokubali kuungana hakuna mwenye haki ya "kudeka" mbele ya mwingine, ebo!
Ndo manaake basi, tunataka kujipanga kupiga rushwa kwa nguvu zetu zote, kuhakikisha uchumi wetu unakuwa kwa haraka sana.
 
Sawa bora tuwe na kiongozi wa tanganyika waziri mkuu maana marais wameshindwa kuleta maendeleo.Zanzibar iwe waziri kiongozi
 
wa Zanzibar hawawezi hata siku moja kuikubali hii, yaani Zanzibar iongozwe na waziri mkuu? no way

Sema wazanzibar"hatuwezi!"na sio hawawezi!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
wa Zanzibar hawawezi hata siku moja kuikubali hii, yaani Zanzibar iongozwe na waziri mkuu? no way
Kwa hiyo una maana tukubaliane na KILA wanachokitaka Wazenj kwa kuwa "hawawezi kukubali hata siku moja"? Muungano una maana kila mtu ana sehemu ya ku compromise na ku sacrifice. Kama wao hawataki any of those...they may well go!
 
Ni kweli na hilo hata kwenye rasimu lipo na wamependekeza viongozi hao yaani wa Tanzania bara na Zanzibar waitwe Magavana
 
Huwezi kuwa na maraisi watatu au wawili ndani ya nchi moja, hakuna kitu kama hicho mahali popote duniani! Tanganyika tutakuwa na waziri mkuu (mtendaji mkuu wa serikali ya Tanganyika) na Zanzibar nao itabidi wabadili katiba yao ili iendane na ya Jamhuri ya Muungano kwa maana kwamba nao itawalazimu kufuta cheo cha rais na kuwa na Waziri mkuu au waziri kiongozi (majina yote haya ni sawa, nyingine ni mbwembwe tu)! ambeye atakuwa mtendaji mkuu wa serikali ya mapinduzi zanzibar!
 

Alhamisi, Juni 06, 2013 06:43 Na Sarah Mossi


WAKATI wananchi wa Tanzania wakijiandaa kurejea tena kwa Serikali ya Tanganyika kama ilivyoainishwa kwenye rasimu ya Katiba mpya, kiongozi wa Serikali hiyo atajulikana kama Waziri Mkuu, Rai imebaini. Wanazuoni na baadhi ya wajumbe wa Tume ya Katiba wameieleza Rai kuwa, Katiba ya Tanganyika inayotarajiwa kutungwa, ndio itakayotamka jina la kiongozi wa nchi na kwa vyovyote vile ataitwa Waziri Mkuu, ambaye chama chake au kwa kushirikiana na vyama vingine anaweza kuunda Serikali kwa kuwa na wingi wa viti bungeni.

Wanazuoni hao wamesema nafasi hiyo ya Waziri Mkuu itaondoa ukakasi wa kuwa na marais watatu katika Serikali tatu zitakazokuwapo mara baada ya kukamilika kutungwa kwa Katiba mpya.

Rasimu ya Katiba mpya iliyotangazwa juzi na Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, imeainisha namna Jamuhuri ya Muungano itakavyokuwa yenye muundo wa shirikisho lenye Serikali tatu.

Serikali hizo ni Serikali ya Jamhuhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, huku shughuli zote za Muungano zikisimamiwa na Serikali, Bunge na Mahakama ya Jamuhuri ya Muungano.

Akizungumza na RAI, Mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba, Profesa Mwesiga Baregu, alisema Serikali ya Jamhuri ndio itakuwa na mamlaka ya juu ya Dola na itaongozwa na Rais, kama itakavyoainishwa kwenye Katiba mpya.

Profesa Baregu alisema Serikali za Tanzania Bara na Serikiali ya Mapinduzi Zanzibar zitakuwa na viongozi wao ambao watatamkwa kwenye kwenye Katiba zao.

Alisema, ingawa Zanzibar tayari inayo Katiba yake inayotamka jina la kiongozi mkuu wa nchi hiyo ambaye ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, lakini bado ipo nafasi ingawa si kwa ulazima kuwapo kwa marekebisho mengine ya Katiba ya Zanzibar, ambayo itatoa nafasi kwa Katiba kutamka jina jingine litakalopendekezwa.

Kwa upande wa Serikali ya Tanzania Bara, Profesa Baregu alisema huu ndio wakati wake wa kutunga Katiba ya nchi ambayo itatamka jina la kiongozi mkuu wa nchi.

“Kwa upande wa Zanzibar, Katiba inaweza kutamka kiongozi aitwe, Waziri Kiongozi na kwa Tanzania Bara litaweza kuwa Waziri Mkuu, hili litaondoa mgongano wa kuwa na marais watatu bila sababu za msingi.

“Ni matumaini yangu Katiba za Tanzania Bara na Zanzibar zitakazotungwa zitapata majina muafaka na kuondoa utata huo,” alisema.

Mjumbe mwingine wa Tume ya Marekebisho ya Katiba kutoka Zanzibar, Ally Saleh, aliiambia RAI kuwa, upande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar tayari wanayo Katiba yao inayomtaja kiongozi wake kuwa ni Rais, hivyo hakutakuwa na ulazima wa kulibadili jina la kiongozi huyo.

“Tukumbuke hatuwezi kuwachagulia Wazanzibar jina la Rais wao, tayari wanaye Rais, hii ni fursa zaidi kwa Serikali ya Tanzania Bara itakayoundwa kuamua Rais wao aitwe jina gani,” alisema Saleh.

 
Kwa Tamaa ya Madaraka tunaivuna vunja nchi yetu sisi wenyewe... Sasa kwanini Bara iwe na Waziri Mkuu? Ina Maana atakuwa hana hadhi kama Rais wa Zanzibar?

Hivi ni kwanini tena walimchagua WARIOBA awe kiongozi ??? Yaani ukiangalia kamati yote ni WHO's WHO in TANZANIA POLITICS up to FATMA SAID ALLY...
 
Sijui siku ya kujadili rasimu itakuwaje?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom