Tangazo la haki elimu linalohusu albino

Tangazo la haki elimu linalohusu albino

Mambo Jambo

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2008
Posts
1,100
Reaction score
82
Kuna tangazo linalorushwa hapa nyumbani Tz Dsm majira ya saa tatu hivi usiku na channel 10 by hakielimu halinipendezi hata kidogo, kama kuna mtu anayeweza kulirekodi nakuliweka hapa itakuwa vizuri zaidi ili wote mlione.

Tangazo hilo linaanza kama hivi.

Asubuhi mabinti wawili albino wako nje ya nyumba mmoja wao amevaa sare za shule na anaelekea shule, binti yule mara yuko barabarani na mbele yake kuna vijana watatu ambao wanaelekea uelekeo atokao wanakaribia kupishana, huyu binti albino anapata hofu kubwa kwa kuwa ni katikati ya barabara tena zile ambazo siyo za mijini na kati ya wale vijana wanaokuja mbele yake mmoja wao amebeba jembe, yule binti anapata woga anakwenda mwisho pembeni ya barabara kwa woga no hofu kubwa, mara ghafla nyuma yake wanaoneka mabinti wengine watatu(siyo albino) wenye amani na furaha tele wasio na woga wala hofu, wanapishana na wale vijana watatu ambao mmoja wao kabeba jembe bila tatizo.mwisho wa tangazo.

My Take:
Tangazo lile linawajengea hofu na woga mkubwa ma-albino badala ya kinyume chake.

Tafadhari kama umeliona tangazo lile na uko pamoja nami naomba kwa pamoja tuwaandikie wahusika wa tangazo hilo HAKI ELIMU waweze kulibadisha au kuliboresha zaidi badala ya kuwajengea hofu albino.
anuani yao pepe ni : info@hakielimu.com

Have got nothing against hakielimu wanafanya kazi nzuri.

MJ
 
Kuna tangazo linalorushwa hapa nyumbani Tz Dsm majira ya saa tatu hivi usiku na channel 10 by hakielimu halinipendezi hata kidogo, kama kuna mtu anayeweza kulirekodi nakuliweka hapa itakuwa vizuri zaidi ili wote mlione.

Tangazo hilo linaanza kama hivi.

Asubuhi mabinti wawili albino wako nje ya nyumba mmoja wao amevaa sare za shule na anaelekea shule, binti yule mara yuko barabarani na mbele yake kuna vijana watatu ambao wanaelekea uelekeo atokao wanakaribia kupishana, huyu binti albino anapata hofu kubwa kwa kuwa ni katikati ya barabara tena zile ambazo siyo za mijini na kati ya wale vijana wanaokuja mbele yake mmoja wao amebeba jembe, yule binti anapata woga anakwenda mwisho pembeni ya barabara kwa woga no hofu kubwa, mara ghafla nyuma yake wanaoneka mabinti wengine watatu(siyo albino) wenye amani na furaha tele wasio na woga wala hofu, wanapishana na wale vijana watatu ambao mmoja wao kabeba jembe bila tatizo.mwisho wa tangazo.

My Take:
Tangazo lile linawajengea hofu na woga mkubwa ma-albino badala ya kinyume chake.

Tafadhari kama umeliona tangazo lile na uko pamoja nami naomba kwa pamoja tuwaandikie wahusika wa tangazo hilo HAKI ELIMU waweze kulibadisha au kuliboresha zaidi badala ya kuwajengea hofu albino.
anuani yao pepe ni : info@hakielimu.com

Have got nothing against hakielimu wanafanya kazi nzuri.

MJ

Kwakweli kwa tangazo hilo hata mimi nakuunga mkono hawakufikiria positively wakati wa kuliandaa! Kwakweli linawatia hofu albino na kuwafanya wawaogope wanajamii wenzao kinyume na jitihada zetu na serikali ambazo zinaitaka jamii iwaone albino kama sehemu ya jamii na albino pia wajione ni sehemu ya jamii na hawana haja ya kuishi kwa hofu! Nitaindikia haki elimu sasa hivi. Ni kweli haki elimu wanafanya kazi nzuri sana ya kukosoa, lakini kwa hili walipaswa wapresent positively, ni kweli hali waliyoinyesha ni halisi kwa sasa, lakini tunataka common ground kwahili swala kuliko tofauti!
 
Kwakweli kwa tangazo hilo hata mimi nakuunga mkono hawakufikiria positively wakati wa kuliandaa! Kwakweli linawatia hofu albino na kuwafanya wawaogope wanajamii wenzao kinyume na jitihada zetu na serikali ambazo zinaitaka jamii iwaone albino kama sehemu ya jamii na albino pia wajione ni sehemu ya jamii na hawana haja ya kuishi kwa hofu! Nitaindikia haki elimu sasa hivi. Ni kweli haki elimu wanafanya kazi nzuri sana ya kukosoa, lakini kwa hili walipaswa wapresent positively, ni kweli hali waliyoinyesha ni halisi kwa sasa, lakini tunataka common ground kwahili swala kuliko tofauti!


Nashukuru sana kaka hapa nia ni kuwaarifu hawa ndugu zetu wa hakielimu upande wa pili wa shilingi, na nia yetu ni kuwataka wajaribu kubalisha script ya lile tangazo na kulifanya liwe bora, naelewa kama nchi kila mmoja wetu anawajibu wa kupinga mauaji ya ndugu zetu albino lakini upingaji huo basi uwe mzuri.
Hili tangazo halijengi linabomoa.

Ningepata watu kama wewe zaidi nadhani hakielimu wangebadilisha lile tangazo.

MJ
 
Nashukuru sana kaka hapa nia ni kuwaarifu hawa ndugu zetu wa hakielimu upande wa pili wa shilingi, na nia yetu ni kuwataka wajaribu kubalisha script ya lile tangazo na kulifanya liwe bora, naelewa kama nchi kila mmoja wetu anawajibu wa kupinga mauaji ya ndugu zetu albino lakini upingaji huo basi uwe mzuri.
Hili tangazo halijengi linabomoa.

Ningepata watu kama wewe zaidi nadhani hakielimu wangebadilisha lile tangazo.

MJ

Nasimama kinyume na mawazo yako/yenu. Hivi kwani ni uongo hawa watu hawana hofu? Wala hawajengewi hofu ndo hali halisi iliyopo. Kama kitu rangi yake ni bluu sema bluu usidanganye eti ni nyeupe ili kumfurahisha bi harusi kipofu. BYE
 
Back
Top Bottom