Kangosha
Member
- Sep 18, 2023
- 52
- 135
Kwa mara kadhaa nimekuwa nikisafiri toka Mtwara kwenda Dar. Kuna baadhi ya maeneo Kwa kipande cha barabara ya mkoa wa Lindi kuna MASHIMO makubwa sana. Mashimo husika yanaweza kusababisha ajali ama uharibifu wa gari.
Baadhi ya mashimo yapo maeneo ya hatari sana. Unakuta kuna mteremko na lami nzuri halafu mbele kuna shimo. Jambo la kusikitisha ni kwamba hakuna taadhari yeyote iliyowekwa kuhusu hayo mashimo na yana muda mrefu.
Japo sio mtaalamu wa ujenzi, ila baadhi ya mashimo mngepanga hata Mawe ili kupunguza ukali wake wakati mnasubiri mchakato wa kumpata mkandarasi. Chondechonde tunaomba mzibe Yale mashimo ili kuepuka kupoteza ndugu zetu Kwa ajali.
Baadhi ya mashimo yapo maeneo ya hatari sana. Unakuta kuna mteremko na lami nzuri halafu mbele kuna shimo. Jambo la kusikitisha ni kwamba hakuna taadhari yeyote iliyowekwa kuhusu hayo mashimo na yana muda mrefu.
Japo sio mtaalamu wa ujenzi, ila baadhi ya mashimo mngepanga hata Mawe ili kupunguza ukali wake wakati mnasubiri mchakato wa kumpata mkandarasi. Chondechonde tunaomba mzibe Yale mashimo ili kuepuka kupoteza ndugu zetu Kwa ajali.