Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Tunaomba kusahihisha kwamba:
Nguzo za daraja hazijaathirika wala hazikusogezwa na mafuriko kutoka sehemu moja kwenda nyingine (Daraja lingeanguka).
Kilichoathirika ni sehemu ya juu ya daraja (deck) ambapo nusu ya kwanza ya deck (m 54) ilisukumwa na mafuriko ya maji yaliyokuwa yamebeba magogo kwa takribani sentimeta 20. Deck hiyo ilitembea kupitia bearing zilizo juu ya nguzo za Daraja.
Tukio hili lilitokea mwezi wa pili 2022 baada ya mvua kubwa isiyo ya kawaida kunyesha na kusababisha mto Muhuwesi kujaa na maji mengi kupita juu ya Daraja yakifunika kabisa Daraja.
Hata hivyo, kwa tathmini ya kutosha iliyofanyika, Daraja lipo imara. Kutokana na kusogea huko kwa deck kwa kiasi cha sm 20, watumia barabara wanaombwa kuendelea kuzingatia alama na tahadhari zilizopo wakati wa kupishana katika Daraja kwa kutumia upande mmoja.
Kutokana na uzito wa deck iliyosogezwa na mafuriko, anahitajika mkandarasi maalum na vifaa maalum vya kuinulia deck ili kuirudisha mahala pake. Vifaa hivyo vinaletwa kutoka nje ya nchi.
Taratibu za kimkataba kumwezesha Mkandarasi kuleta vifaa vya kunyanyulia deck zipo katika hatua za mwisho ili kazi ya marekebisho ianze mara baada ya msimu wa mvua na kazi inatarajiwa kukamilika mwezi wa sita 2023.
TANROADS.
Pia, Soma:
www.jamiiforums.com
www.jamiiforums.com
Nguzo za daraja hazijaathirika wala hazikusogezwa na mafuriko kutoka sehemu moja kwenda nyingine (Daraja lingeanguka).
Kilichoathirika ni sehemu ya juu ya daraja (deck) ambapo nusu ya kwanza ya deck (m 54) ilisukumwa na mafuriko ya maji yaliyokuwa yamebeba magogo kwa takribani sentimeta 20. Deck hiyo ilitembea kupitia bearing zilizo juu ya nguzo za Daraja.
Tukio hili lilitokea mwezi wa pili 2022 baada ya mvua kubwa isiyo ya kawaida kunyesha na kusababisha mto Muhuwesi kujaa na maji mengi kupita juu ya Daraja yakifunika kabisa Daraja.
Hata hivyo, kwa tathmini ya kutosha iliyofanyika, Daraja lipo imara. Kutokana na kusogea huko kwa deck kwa kiasi cha sm 20, watumia barabara wanaombwa kuendelea kuzingatia alama na tahadhari zilizopo wakati wa kupishana katika Daraja kwa kutumia upande mmoja.
Kutokana na uzito wa deck iliyosogezwa na mafuriko, anahitajika mkandarasi maalum na vifaa maalum vya kuinulia deck ili kuirudisha mahala pake. Vifaa hivyo vinaletwa kutoka nje ya nchi.
Taratibu za kimkataba kumwezesha Mkandarasi kuleta vifaa vya kunyanyulia deck zipo katika hatua za mwisho ili kazi ya marekebisho ianze mara baada ya msimu wa mvua na kazi inatarajiwa kukamilika mwezi wa sita 2023.
TANROADS.
Pia, Soma:
DOKEZO - Ruvuma: Nguzo za Daraja la Mto Muhuwesi zadaiwa kufikisha miaka minne bila kufanyiwa marekebisho
Hizi picha hapa chini zinadaiwa ni za daraja la mto Muhuwesi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma. Inadaiwa kwamba inakaribia mwaka wa nne sasa tangu nguzo zake zicheze na halijafanyiwa marekebisho hivyo inalazimika gari zote zipite upande mmoja. ====== UPDATES ======= Ufafanuzi wa Mkuu wa Wilaya...
Ruvuma, Tunduru: Daraja la Muhuwesi lajaa maji. Barabaraba yafungwa
TAHADHARI KWA MAGARI YANAYOSAFIRI KUJA AU KUTOKA TUNDURU KUPITIA DARAJA LA MUHUWESI. Pamoja na simu nyingi ambazo mmepiga wenzetu wa vyombo vya habari na nyingine nimezijibu kwa kifupi mna na wanisamehe wale ambao nimeshindwa kuwapa ushirikiano, leo ilikuwa siku ngumu kikazi, vikao na mambo...