Tanzania Bara ina Mawakili 1,188 Tu!

Tanzania Bara ina Mawakili 1,188 Tu!

Buchanan

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2009
Posts
13,192
Reaction score
1,972
Wapendwa WanaJF,
Tanzania Bara ina Mawakili wa kujitegemea 1,188 tu kwa takwimu za hadi Desemba 15, 2009 (Bonyeza hapa kwa taarifa zaidi). Kwa kuwa Mawakili wengi sana wanapenda kuishi Dar es Salaam (angalia uk 120 na 121 wa The Legal Profession in Tanzania: The Law and Practice by Dr Fauz Twaib, Published by LawAfrica Publishing (T) Ltd, 2008) kuliko mikoa mingine, si rahisi wa watu wengi, especially wenye vipato duni na wanaoishi vijijini kupata huduma za kisheria kwa kuwa idadi ya mawakili hawaishi nao na ni wachache.
Kwa kuwa CCM Katika Ilani yake ya Uchaguzi, 2005 Ibara ya 108 (i) na (j) inasema kwamba CCM ingeanzisha mfumo wa kuwasaidia watu wasiokuwa na uwezo kupata msaada wa kisheria na vilevile ingeanzisha mfumo utakaotumia wanasheria wa awali (para-legals) katika Mahakama za Mwanzo, mifumo hiyo ianzishwe mapema ili haki wa raia wa nchi hii zilindwe! CCM ikija kuomba kura tena mwishoni mwa mwaka huu 2010 tuwaulize juu ya utekelezaji wa ahadi hii, japokuwa ahadi kibao hazijatekelezwa!
Tujadili zaidi!
 
Ndio maana nipo katika mchakato wa kuwa mwansheria na badaye wakili ili kuziba mapengoo hayoo. Ni career ambayoo bado ina fursa nyingii zaidii.
 
Ndio maana nipo katika mchakato wa kuwa mwansheria na badaye wakili ili kuziba mapengoo hayoo. Ni career ambayoo bado ina fursa nyingii zaidii.

Jitahidi ndugu, maana kuingia kwenye Roll of Advocates nako ni issue, ndio maana wako wachache!
 
Jitahidi ndugu, maana kuingia kwenye Roll of Advocates nako ni issue, ndio maana wako wachache!



mwezi june wataongezeka.kwani wanafunzi wa zao la kwanza la shule ya sheria(law school) wataapishwa.
 
Tena katika hao 1188 toa wale ambao wameshatangulia mbele ya haki na wengine ambao they are no longer active in practice utabakiwa labda na mawakili 700 tu ambayo ndio "idadi kamili"
 
Jitahidi ndugu, maana kuingia kwenye Roll of Advocates nako ni issue, ndio maana wako wachache!

mi nilidhani wapo wengi ndo maana inatuchukua miaka kuitwa kwenye bar exam!!!!
 
Wapendwa WanaJF,
Tanzania Bara ina Mawakili wa kujitegemea 1,188 tu kwa takwimu za hadi Desemba 15, 2009 (Bonyeza hapa kwa taarifa zaidi). Kwa kuwa Mawakili wengi sana wanapenda kuishi Dar es Salaam (angalia uk 120 na 121 wa The Legal Profession in Tanzania: The Law and Practice by Dr Fauz Twaib, Published by LawAfrica Publishing (T) Ltd, 2008) kuliko mikoa mingine, si rahisi wa watu wengi, especially wenye vipato duni na wanaoishi vijijini kupata huduma za kisheria kwa kuwa idadi ya mawakili hawaishi nao na ni wachache.
Kwa kuwa CCM Katika Ilani yake ya Uchaguzi, 2005 Ibara ya 108 (i) na (j) inasema kwamba CCM ingeanzisha mfumo wa kuwasaidia watu wasiokuwa na uwezo kupata msaada wa kisheria na vilevile ingeanzisha mfumo utakaotumia wanasheria wa awali (para-legals) katika Mahakama za Mwanzo, mifumo hiyo ianzishwe mapema ili haki wa raia wa nchi hii zilindwe! CCM ikija kuomba kura tena mwishoni mwa mwaka huu 2010 tuwaulize juu ya utekelezaji wa ahadi hii, japokuwa ahadi kibao hazijatekelezwa!
Tujadili zaidi!

Moja kati ya ahadi nyingi walizoahidi na hazipo, wakija tena tuwaambieje?????? Kama mtu ulipata ridhaa ya watu kwa kuahidi kitu halafu hutendi hicho kitu iluchoahidi sisi tiliokupa ridhaa tuna haki gani juu ya ahadi zako????
 
Moja kati ya ahadi nyingi walizoahidi na hazipo, wakija tena tuwaambieje?????? Kama mtu ulipata ridhaa ya watu kwa kuahidi kitu halafu hutendi hicho kitu iluchoahidi sisi tiliokupa ridhaa tuna haki gani juu ya ahadi zako????
Lawful means ni kutowapa kura tena wakija kuomba au kuwakumbushia tena ahadi zao maana inawezekana wana maelezo. Pia kufanya maandamano halali ili kushinikiza. Unlawful means ni kupindua serikali, kumpiga Rais mawe anapokuja ziarani, kuzomea, nk! All in all, haki huwa haziombwi, zinapiganiwa!
 
Kenya ina mawakili zaidi ya 6000 na Uganda ina mawakili zaidi ya 3000
Hii jumuia ya EA tutaweza kweli kushindana na hao jamaa?
Cha kusikitisha zaidi Mawakili wengi toka Kenya na Uganda wamekuja kusoma TZ hapo Mlimani.
 
Kenya ina mawakili zaidi ya 6000 na Uganda ina mawakili zaidi ya 3000
Hii jumuia ya EA tutaweza kweli kushindana na hao jamaa?
Cha kusikitisha zaidi Mawakili wengi toka Kenya na Uganda wamekuja kusoma TZ hapo Mlimani.

Tutafika tu ndugu, hii EAC itatufungua macho!
 
Kenya ina mawakili zaidi ya 6000 na Uganda ina mawakili zaidi ya 3000
Hii jumuia ya EA tutaweza kweli kushindana na hao jamaa?
Cha kusikitisha zaidi Mawakili wengi toka Kenya na Uganda wamekuja kusoma TZ hapo Mlimani.

Actually tunachekesha sana. Halafu chimbuko la sheria East Africa ni Unidar ajabu sisi ndio tunasuasua. kutokana la saturation ya mawakili kwa majirani ndo maana nchi zingine issue yao kubwa ni cross border practice.

Take that with the fact that Kenya ni nucleus ya multinationals katika Est and Central Africa mawakili wa tanzania wataambulia kushika kesi za matusi na kesi za talaka.
 
Actually tunachekesha sana. Halafu chimbuko la sheria East Africa ni Unidar ajabu sisi ndio tunasuasua. kutokana la saturation ya mawakili kwa majirani ndo maana nchi zingine issue yao kubwa ni cross border practice.

Take that with the fact that Kenya ni nucleus ya multinationals katika Est and Central Africa mawakili wa tanzania wataambulia kushika kesi za matusi na kesi za talaka.

Tatizo la legal profession ni ubinafsi umetawala! Walioko juu wanaona wakifungua milango soko litavamiwa na status ya uwakili itashuka! Hivi tuseme kwa upande wa Kenya na Uganda kwa kuwa mawakili ni wengi kwa hiyo hawana status? It is so sad, Kitivo cha Sheria cha UDSM ni cha kwanza kwa Afrika Mashariki kuanzishwa, lakini sasa hivi tuko wa mwisho kuwa na mawakili! In fact, it is ridiculous!
 
Back
Top Bottom