.
Kama ungekuwa na skuli hata ya Degree ya kwanza basi ungejua nini maana ya Chuo kikuu na ni wapi vinapata usajili.
Sidani kama nahitaji hiyo degree kujua hizo procedures za kuandikisha university+kujua ubovu wa mamlaka za viwango.
Nadhani unahofia sana jina university, wakati nao pia wana hata mamlaka inayoandikisha meli zinazoua wazanzibar kila kukicha.Nao wanapiga kelele kuwa wana viwango.
Ninavyozungumza kuna vyuo vikuu vitano vimesajiliwa na TCU ambacho ni chombo cha muungano katika kuhakiki ubora wa ilmu na mazingira ya vyuo vikuu huko Tanzania.
Sitaki waingilia hao jamaa wa TCU.Ila kutoaminiana kwa vyuo hadi kuwekea mizengwe kwa graduate wa chuo kimoja kwenda kingine ktk TZ ni kukubwa sana.
Kuna vyuo kibao Tz havina lecturers wa viwango,wameagaliwa marks bila kujua wamezipata vipi.Matokeo yake vichekesho katika hivyo vyuo,wanafunzi wanajua walimu gani wababaishaji na wangapi kidogo wanaweza piga domo.Walimu wa vyuo vikuu wengi wanachojidai ni kuwa wanatoa reference +assignments+wanatangaza test,wanajua wanafunzi watakimbizana na kuleta majibu.Wengine ukiwapa hizo test na kuwapatia mwalimu wa nje jamaa hawapiti.Unaweza shangaa ila mika ya chuma walimu wa primary walisapewa mitihani ya wanafunzi wao ikawashinda.
TCU hawapo hapo kama TBS wasivyo katik mfumo mzima wa production/manufacturing ila wanatokea katika final product.Pengine hata hizo sample wanaletewa zile za maonyesho.
Sipendi Bishana na wewe ila jaribu pitapita katik walimu wa vyuo tena wa taaluma za computer halafu uangalie powerpoint presentations zao, zilivyo za ubora wa chini,halafu uniambie kama anaweza fikisha ujumbe sahihi kwa wanafunzi darasani.Achilia mbali uwezo wa kitaaluma katik kutumia vifaa vya kazi pamoja na kuwa mwepesi na huru kujibu n akujieleza darasani.Nadhani utaona kuamini kuwa TCU hawajafikia kuangalia elimu katik kila stage.Ndio maana tuna wasomi WA AKILI NDOGO KUENDESHA KUBWA.
Je ni nani asiyeijua State university of Znz , Znz university etc. Hivi ni vyuo ambavyyo vimetoa wanafunzi wengi sana na wengi tu wapo sehemu mbalimbali katika mashirika na taasisi za Muungano hususan katika fani za Uchumi, sharia na ualimu etc.
Mi sijui kama kuna zaidi ya chuo kikuu kimoja zanibar.Ndio unaeleza hapa.Naomba list vyote basi.
Kumbuka kufahamika kwa University sio mbwembwe bali ni kwa zile product wanazozitoa nazo zimeshaanza kwa kasi sana kutoa matunda.
teh teh..sitaki kupinga wala kuwa kikwazo katik juhudi zako za kueleza habari njema toka kisiwani.Ila tatizo ni kuwa umekuwa influenced na mitazamo fulani ya wasomi wa Zenj."Wanajitamani wenyewe" wanajiangalia katika vioo na kujipa viwango, halafu wanatafuta udhaifu mdogo kwa wengine wanautumia kujipa matumaini.Ndugu yangu zenj mna mmabo mengi sana yaliyo nje ya elimu yanayofanya elimu yenu isiwe reliable sana.Naamini mengi unayajua ila haupo tayari kuyasema.
Elimu inaweza unganishwa na utalii ila elimu si utalii by itself,so utangaze kwa makini.
Vile vile kukosa mahusiano ya ilmu na kuelimika ndio yanayowaletea wengi matatizo huko tanganyika. Kwani hata ukitembea barabarani utaona wale madereva wa daladala na bajaji wanavyo sababisha foleni kwa ima kukiuka taratibu na kanuni za udereva au kupuuza kutokana na kukosa ilmu.
Ndugu yangu foleni na daladala ndizo zimekufanya uone hivyo?Mbona kuna daladala nyingi za wapemba na unguja na madereva ni waho pia?Mbona mimi nimeona Uchafu unaweza kuwa ndio kukosa elimu kuliko na hayo yapo zaidi visiwani.Pamoja na udogo za Zenj ,hata mitaa yenye ukaribu na mji kabisa watu hawana vyoo?Daladala inaweza kuwa ni ukorofi tuu kwa vile tamaa,ubinafsi, shida za watu mwisho wa siku ndizo ziwafanyazo wajikute hivyo.Ila kukuwa na choo na kujihahatarisha kwa magonjwa ni ujinga zaidi.
Sijui ni mitizamo tuu au ndio kuwa na mitizamo ambayo ni too confined, na kuwa na uelewa mdogo au ni kudharauliana bila sababu.Kwa mategemeo ya wengi kuwa PhD holders watakuwa na uwelewa wa kuridhisha,ila wabara huwa wanawashangaa sana wanaotoka visiwani,wanawaona kama vile misukule fulani.Pengine na wao wakirudi huko huja na mijisifa kibao kuwa wanakubalika na mengine,hivyo kuwafanya watu mliobanwa huko kutamani baki visiwani na mara mkitoka jicho lenu huwa kama vile wale jamaa wa ubishi wa dini huwa wanasoma vipande vya mistari kwa staili ya kuwasaidia ubishi"negatively".
Hata wale jamaa wa UDSM na Muhimbili hawachoki piga domo kuwa elimu ya US ni ndogo kuliko ya Bongo,ila wenzao wanachana ubongo, wanabadili sura za watu, na mengineyo.
By the way ukienda South East Asia,India,malaysia, indonesia, philipines, vietnam,thailand, pakistan etc tena katik miji mikuu kama Mumbai,Delhi,manill etc utaona jinsi gani sisi tuna afadhali ingawa hatuwezi shindana na hizo nchi kwa mambo mengi.
Kukusaidia tuu ni kwamba masuala ya barabara na misongamano katika miji ni suala la mamlaka ya mipango miji.Miji iliyo na watu wengi wasio na hakika ya maisha, na walio katika hofu ya kutomiza malengo ya jioni ni kama kudondosha chakula somalia, hakuna atakayesubiri wapokee mmoja moja wakati hana hakina kuwa ikifika zamu yake atakuta kitu.
naamini wazi kama wote hawa wangeelimika kusingekuwa na foleni za kipumbavu huko tanganyika.
Kuna mengi sana ambayo vijana wa KiZnz kwa ilmu iliyowekezwa na SMZ wameweza kujifunza na kufanya maisha kuwa rahisi sana hususan katika nyanja za siasa na kwengineko.
Endelea amini hivyo ndugu yangu kwnai kuna faida kwa usalama wa nchi.Amini kama watanzania walivyokuwa wakiaminishwa kuwa legacy newspapers kama uhuru na mzalendo, sijui na daily news, ndio magazeti bora na yenye weledi..ila sijui hata rangi zake nasikia tuu watu walilalaa kuwa yanapiga story sana.
Sijui unamaanisha nia ya SMZ ambayo siwezi pinga kwa vile siwezi isema.Ila kuna mengi wasomi wa Zenj wamewaangusha,wamewadhalilisha, wameitosa zenj,kupitia siasa na propaganda.Ila waulize hao viongozi kwanini wanapenda kula maisha dar?Uliza vizuri ubaguzi uliopo huko.Pengine utabisha kiushabiki au upo katika madhabahu na unakula vyema na wenye madhabahu.
Zanzibar ipo na watu wa lost generation,zanzibar moral standards zimeshuka,huku wakiamini kuwa wapo juu.Pengine mzanzibar anaweza jivunia kwa kuwa na sheria mapema za haki za binadamu ila hawezi jua ni kwanini ziliwekwa tena chini ya watawala wasioheshimu haki za binadamu.Zanzibar wangekuwa jamii ya uwazi kama za ulaya pangekuwa na kashfa kuliko za ulaya(ushoga, ubakaji na udhalilisaji wa watoto).Unicef na mashirika mengine yalikuwa na report za kutisha kuhusu udhalilishaji wa kingono/ukabaki katika madrassat, na school hadi serikali haikuweza pinga sheria kuwekwa.Sijui kama story ilikuwa hivyo katika macho yenu?
Nimekuwa zanzibar sana na nimeongea na watu, nimesikiliza watu wakiongea, nimesikia tafsiri zao za haki hata kwa wale wanaolia kuwa ni wapenda haki,nimesikiliza mitazamo yao juu ya watu wa bara, ..napata huruma.Ndipo napata picture kwanini viongozi wa Zanzibar wakiingia katik Muungano huwa wanajenga dar ili wakae mbali na watu wao.Kwa vile wanahisi hawawezi wabadili watu na ni bora wawatumie hivyohivyo, wawape habari wazipendazo kuzisikia.Nawalaumu kw ahilo kwa vile wanazidi waharibu na mwisho kuja waachia viongozi wajao watu wasioongozeka.