Tanzania Chungeni mambo ya Eurobond

Tony254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2017
Posts
16,017
Reaction score
16,431
Nawapongeza Watanzania kwa kupata status ya middle income country. Lakini nataka niwaonye kuwa kuna tatizo moja kubwa mtakayo kumbana nayo. Mtaweza kuomba mikopo yoyote ile na kuipata kwa urahisi sana sio kama zamani ambapo masharti yalikuwa mazito.

Pia mtaweza kupata commercial loans kutoka kwa benki za Ulaya kwa haraka bila maswali mengi. Lakini tatizo kubwa ni "Eurobond". Hii Eurobond ni deni na lazima ulipe hakuna kusamehewa na inapewa sana nchi za middle income. Hili jitu linaitwa Eurobond limeumiza nchi nyingi sana za Afrika. Tukianzia na Ghana. Ghana walikimbia kuomba Eurobond ya kwanza, tena baadaye wakaomba ya pili. Madeni yaliwazonga karibu washindwe kulipa.

Pili, kuna Zambia ambao walipata status ya middle income 2011 na wao pia wakakimbilia kuomba deni la Eurobond. Wao pia karibu washindwe kulipa deni hio pamoja na madeni mengi ambayo walikuwa wameomba

Tatu, Kenya ambayo miaka sita iliyopita tulipata hii status ya middle income lakini kwa bahati mbaya tukapata waziri wa fedha corrupt na mwenye alikuwa na appetite ya juu sana ya kuomba madeni. Rais Uhuru naye hakuzuia kuongezeka kwa bajeti kila mwaka sasa ikabidi Kenya iombe Eurobond one na Eurobond two na juzi tulikuwa tunapanga kuomba Eurobond three. Debt to Gdp ratio ya Kenya by 2021 itatinga 70%. Hii ni hatari.

Yaani kwa kumalizia tu ni kuwaonya msikimbilie madeni ovyo ovyo na hata mkiomba basi mchukuwe zile ambazo zina interest rates nafuu. Pia mtumie deni hio vizuri kwa maendeleo (development expenditure) mujenge barabara, dams na kadhalika. Msiitumie vibaya kwa corruption au matumizi ya kila siku (recurrent expenditure) maana kuomba ni harusi kulipa ni matanga.
 
Asante kwa ushauri wako naona umeanza kuikubali TZ ila Magufuli hakurupuki.
 
Asante kwa ushauri maana muda huu Tanzania na Kenya tuko meza moja ya watu wenye uchumi wa kati tunaweza kujadili biashara mbalimbali.
 
Sidhani kama Kenya inaweza kuifundisha Tanzania jinsi ya kutafuta pesa na kuzitumia vizuri, badala yake ni kwamba Tanzania ndio inapaswa kuwafundisha wakenya jinsi ya "Financial management'.

Tatizo la hizo nchi ulizozitaja, hasa kwa Kenya sio Eurobond wala kukopa pesa, tatizo ni uwezo mdogo wa Kenya katika kupanga matumizi ya miradi yenye kuleta faida na usimamizi wa miradi kutokana na uwezo mdogo, ukabila, rushwa na upendeleo.

Hakuna mchumi yeyote nje ya serikali ya Jubilee aliyekubaliana na ujenzi wa SGR ya Kenya kutoka mwanzo, watu wenye akili walisema waziwazi kwamba huu mradi hauna faida kwa Kenya, gharama zake zipo juu sana hivyo hakuna sababu ya kujengwa kwa sasa.

Nani asiyejua kwamba Lamu Port pia haiwezi kuleta faida kwa Kenya, nani asiyejua kwamba baadhi ya viwanja vya ndege vilijengwa kama ISiolo lakini ni hasara kwa Kenya, nani asiyejua kwamba Kenya inataka kujenga bomba la mafuta toka Lokachiar hadi Lamu ambalo halina faida kwa Serikali?

Miradi kama hii hata ukipewa mikopo bila interest haiwezi kurudisha hiyo pesa. Wacha kulaumu Eurobonds, tatizo ni uwezo mdogo wa viongozi wenu katika kupanga vipaumbele vya nchi na matumizi mazuri ya Fedha.
 
Uhuru angezuia Nini na yeye na Rotich ni Kama mate na ulimi,ama hukumbuki uhuru alipokua waziri wa fedha Ile computer error? Rotich na waiguru walikua pale Kama wasaidizi wake ,hao wawili anawatumia kuiba pesa za umma siku hizi amempumzisha Rotich na kumuacha kipenzi waiguru aendeleze mchezo Kama kawaida.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Tony254,

Magufuli anatafutwa na mabeberu ili akopeshwe kwa sababu wamemjua ni MTU makini na analipa madeni vizuri hataki longo longo.
 
Tony254,

Tanzania tunaelekea high income country sasa wewe jiulize Zambia inanini cha kuikaribia tz kiuchumi ? Mabeberu wameumbuka kwa unafiki wao wakaona waseme ukweli kuwa tz hipi MIC ila ukweli tz tupo tangu 2008 maana Zambia ya sasa ni kama tz ya 1995.
 
Tony254,

Kama nchi zetu za kiafrica zikitulia na kupata watu makini nahamini kabisa wala hatuitaji mikopo sana ili kufanya project kwa nchi zetu, najua suala mikopo lipo haijalishi nchi imehendelea au aijaendelea ndio mahana hata nchi tajiri zinakopa, tofauti yetu na wao, nchi tajiri zinakopa pale wanapohona kuna umuhimu wa kufanya hivyo na pia wanakua makini kuakikisha fedha za mkopo zinatumika kufanya mambo iliyokusudiwa.

Mataifa tajiri yanatumia mikopo kama trap yakuweza kujipenyeza ili waendele kutumia rasilimali zetu, ndio mahana bahadhi ya mikopo yao hua na mashariti magumu na ukizingatia walishajua udhaifu wa viongozi wegi wa kiafrica kua wengi wanatumia mikopo hiyo kwa manufa yao wenyewe na fedha nyingi wanazificha kwenye mabenki ya ulaya hivyo unakuta zile fedha badala ya kutumika kuleta maendeleo huku africa zinarudi ulaya kuwanufaisha wazungu.

Lakini kama tutahacha michezo michafu ya kuziujumu nchi zetu wenyewe, binafsi nahamini tutapiga hatua kubwa na tunaweza kabisa kuanza kuwasaidia wazungu badala ya kuitaji mikopo yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…