Tanzania hakuna tume ya kukabiliana na maafa, matokeo yake hakuna uwajibikaji. Waziri Mkuu Simamia sheria ya maafa uunde timu husika mapema

Tanzania hakuna tume ya kukabiliana na maafa, matokeo yake hakuna uwajibikaji. Waziri Mkuu Simamia sheria ya maafa uunde timu husika mapema

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Vijana wa chadema walipokwenda Rufiji Mkuu wa wilaya alijibu kimzaa kwamba tatizo siyo kubwa. Waliposema wataanza kurusha picha za hali ilivyo serikali imeshtuka imepeleka mawazri na watendaji wengine wengi.

Serikali inachokosa ni TUME YA KUKABILIANA NA MAJANGA; Duniani kote walipofanikiwa kukabiliana na majanga waliunda chombo. Chombo hicho kinakuwa na budget , watumishi wa kudumu na mpango mkakati. Kwa Tanzania anayekabiliwa na na maafa ni Waziri Mkuu lakini hana timu na ndiyo maana gharama za viongozi kwenda kushuhudia mafuriko Rufiji ni kubwa lakini hakuna misaada.

Chadema wanapaswa kuja na mbinu za kufundishia serikali kuhusu umuhimu wa kuwa na kikosi au tume ya maafa ambayo inajumuisha Polisi, Zimamoto, JW na vikosi vingine . Kazi yao kubwa ni kurespond kwenye majanga na kufanya utafiti kuepusha vifo.

Na hii ipo kwa mujibu wa sheria ila watawala hawataki kuiunda chombo kwa sababu wanapiga fedha kwenye eneo hili. Waziri Mkuu unda chombo achana na hao mawaziri wanapambatana na makatibu wakuu kwenda kushuhudia maafa. Tuliona Manyara hakukuwa na organization leo tupo Rufiji na jana tumeona Arusha.
 
Kwamba badala ya kuwa Pro-active na kuhakikisha hatufanyi vitu hatarishi ambayo matokeo yake tunajua na Hasi.., Tupeleke vijisenti vyetu ambavyo tungevitumia kuwa Pro-active kuunda Tume ili ilete majibu ambayo tunayo na hayatafanyiwa Kazi ili baadae Tuunde Tume ya Kuchunguza Tume ?
 
Kwamba badala ya kuwa Pro-active na kuhakikisha hatufanyi vitu hatarishi ambayo matokeo yake tunajua na Hasi.., Tupeleke vijisenti vyetu ambavyo tungevitumia kuwa Pro-active kuunda Tume ili ilete majibu ambayo tunayo na hayatafanyiwa Kazi ili baadae Tuunde Tume ya Kuchunguza Tume ?
Siyo tume kama tume kama unayodhani, sheria inataka kuundwa kwa chombo kitakachoratibu , kudhibiti na kusimamia maafa chini

Leo hii yanapotokea maafa wanaokwenda kwenye maeneo hayo ni Mawaziri na viongozi wa wizara; jiulize waziri anakwenda kuokoa nini? Mfano jana tumeona Rufiji mawaziri wanafika hakuna cha maana wanachofanya.

Tungekuwa na chombo cha wataalamu kinachosimamia haya majanga maana yake leo uokoaji na tathmini ingefanywa kwa kina na tungeelewa tunapotakiwa kwenda
 
Siyo tume kama tume kama unayodhani, sheria inataka kuundwa kwa chombo kitakachoratibu , kudhibiti na kusimamia maafa chini

Leo hii yanapotokea maafa wanaokwenda kwenye maeneo hayo ni Mawaziri na viongozi wa wizara; jiulize waziri anakwenda kuokoa nini? Mfano jana tumeona Rufiji mawaziri wanafika hakuna cha maana wanachofanya.

Tungekuwa na chombo cha wataalamu kinachosimamia haya majanga maana yake leo uokoaji na tathmini ingefanywa kwa kina na tungeelewa tunapotakiwa kwenda
Ni kipi hakijulikani na kipi hakipo ? Kama kuna sehemu prone kwa mafuriko, matetemeko au jambo fulani kitu cha kwanza ni kuhakikisha community ya watu wengi haijengi pale....

Kama sehemu kuna milima mawe basi usiweke shughuli za kibinadamu sababu ukichokonoa vitu au ikitokea erosion utapata land slides...

Ukichenga jengo refu au kila sehemu kwenye watu wengi hakikisha kuna fire hydrants sababu moto ukitokea ni rahisi kuliko kupitisha magari na ili magari yaweze kupita hakikisha kila watu wanapojenga wanaacha sehemu za uchochoro barabara ya kuweza kufikia kila sehemu...

Hio Tume na wataalamu wa kukaa baada ya maafa wakae wakati wa ujenzi wa miundombinu ili kupunguza utokeaji wa majanga au kuwa na plan ya nini kifanyike pindi la kutokea likitokea.... Lakini being pro-active ndio mpango mzima na ajali nyingi ukiangalie ni uzembe fulani umetokea.....; na kwa Teknolojia na Historical data tulizonazo kuna accidents kibao waiting to happen lakini tunazifumbia macho (hatuzibi ufa lakini tunasubiri kujenga ukuta)
 
Back
Top Bottom