Tanzania Hamna Referee

SK2018

Senior Member
Joined
Jan 6, 2018
Posts
156
Reaction score
149

Marefa wakibongo hawana viwango vinavyohitajika na ndio maana hawachaguliwi kwenye mechi za Afcon. Rwanda, Tchad, Djibouti, Burundi, Mauritius, Comoros, Seychelles, na Lesotho zote zikichanganywa pamoja ni ndogo kuliko Tanzania. Ila kwa jinsi marefa wetu wanavyotoa maamuzi yao inasikitisha sana.

Mfano ni ile mechi ya Yanga na Namungo. Penati ilikuwa ya utata halafu tena refa anaruhusu penati kupigwa wakati wachezaji washaingia kwenye box. CAF wakitazama mechi ile wanacheka tu.

Kingine, mechi za CAF wanahitaji marefa waweze kuwasiliana na wachezaji kwa Kiingereza, Kifaransa, ama Kiarabu. Marefa wetu wanaweza hilo?
 
Kuna yule refa wa ligi kuu mwaka juzi golikipa alidakia mpira kwenye mringoti ndani halafu eti akaamuru ipigwe corner.
Yule hana hata sifa ya kuchezesha michuano ya umitashumta.
 
Nadhani marefa duniani wanavituko ila Tz kinachowakosesha ulaji zaidi ni lugha

Hivi ushawahi kuona refa akachezesha mechi Acra au Cairo na asilalamikiwe??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…