Tanzania,mwanafunzi akifeli, kidato cha nne anapangiwa, ualimu shule za msingi. Akifeli kidato cha sita eti ndio amepata sifa za kuwa mwalimu wa sekondari, je SHULE zetu hazihitaji mtu mwenye uwezo kitaaluma? Nafikiri ualimu usitazamwe kama kitu cha ziada, bali uwe kama taaluma nyingine mfano UdaKtari, Engineer, Uhasibu e.t.c. ukimkuta mtu anayesomea ualimu, atakuambia ni bahati mbaya tu nasomea ualimu, maana nilishindwa kufauli mtihani wa NECTA VIZURI, swali ni kwamba ualimu hauhitaji waliofaulu vizuri?