Tanzania ina akiba ya gasi asili futi za ujazo trilioni 57.54

Tanzania ina akiba ya gasi asili futi za ujazo trilioni 57.54

mkiluvya

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2019
Posts
809
Reaction score
729
1573112992461.png
1573112992461.png
1573112992461.png
1573112992461.png
1573112992461.png

SERIKALI kupitia Wizara ya nishati imesema Tanzania ina akiba ya gesi futi za ujazo trilioni 57.54 huku matumizi ya rasilimali hiyo kwa sasa ni futi za ujazo trilioni 0.5 tu.

Kutokana na hayo imesema itashirikiana kwa ukaribu zaidi na asasi za kiraia kuhakikisha wanaleta maendeleo ya uchumi wa viwanda kwa kutumia rasilimali gesi.

Hayo yamebainishwa Nov.6,2019 na waziri wa nishati Medardi Kalemani wakati akitoa taarifa ya nishati kwenye jukwaa la tisa la wadau wa sekta ya uziduaji wa mafuta , gasi na madini Katika wiki ya AZAKI inayoendelea Jijini hapa.

Waziri Kalemani amesema matarajio ya serikali ni kuhakikisha rasilimali hiyo inashiriki kikamilifu kwenye uchumi wa viwanda na kuchochea maendeleo ya taifa na wananchi wake.

Pamoja na hayo amesema ,jitihada za Serikali zinaendelea Katika kuhundua mafuta kwa manufaa ya watanzania .

Aidha Mhe.Kaleman ame sisitiza masuala ya uwazi,uwajibikaji na ufuatiliaji wa uhakika Katika masuala ya gesi unapaswa kupewa kipaumbele kwa kuzingatia teknolojia na ubunifu kwa uchumi wa viwanda.
 
Aisee! Hivi hao waliokuwa wanaichimba maeneo ya kusini wameshapunguza kiasi gani ya hizo trillion 57.5!?
 
ni sawa na kutuambia Tajiri namba 1 tanzania ni MO DEWJ

inatusaidia nini sisi tukishajua tuna ujazo huo wa gesi?

mavitu yenyewe mnatuambia tu ila hatujawahi hata yaona au mkatupa Bure

Nyamazeni bakini na record zenu huko huko.
 
Back
Top Bottom