Tanzania ina wachezaji wawili wenye uwezo wa kucheza ulaya kwenye ligi za maana

Mndengereko One

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2015
Posts
340
Reaction score
243
Ni maoni yangu nimeona Tanzania tuna wachezaji wawili wa maana ambao hawastairi kucheza Tanzania ila mfumo wetu unaendelea kuwabakisha nawa zungumzia Saidi Ndemla na Faridi Musa hii ni dhahabu hila sitashangaa wakipotelea hapa hapa bongo nikianza na ndemla huyu ni kiungo mshambuliaji aliye kamilika anapiga zenye macho akimiliki mpira uwezi kuuchukua hapotezi mipira siku yeyote atakayo bahatika kupata timu ya kwenda try lazima afuzu tatizo uthubutu wake

Ndumbaro alishawai kumtafutia timu yeye na Frank Sekule wakafuzu baada ya wiki kazaa wakarudi wakasema ujerumani baridi chakumshauri ajenge mwili ni raha sana kumtazama ndemla akiwa na mpira lazima akuburudishe .farid musa winga bora kwa sasa tanzania anajua kupiga chenga ana speed pass zake za mwisho hapigi bila ya kuangalia siku nae atakayopata nafasi ya nje ana asilimia kubwa ya kufuzu naamini ni mchaga mwenye kipaji kuliko wote niliyo wahii kuwaona
 
Watatu mkuu, umenisahau mimi
 
Mkuu umenena vema sana na ninaheshimu mawazo yako.
Mimi ni mnazi wa Simba lakini napenda niongeze mtu wa tatu kwa maana ya wachezaji wanaoshiriki VPL ambao n Watanzania.
Kuna mtu anaitwa MUDATHIR YAHAYA kutoka kwa Bakhressa kule Chamazi.Kwa mtazamo wangu naona jamaa anaweza na anastahili kuungana na Ndemla na Farid.
Aidha,naamini pamoja na kuwa na uwezo wa kucheza Ulaya,wanahitaji kujengwa kisaikolojia ili waelewe maana na sababu ya wao kustahili kuwa huko na si hapa walipo.
Pia,wajengewe consciousness ambapo itawasaidia kujitambua.Hili ni jambo ambalo wabongo wengi wanalikosa.Tuna mifano ya watu kama Boban,Ngassa na Kapombe.
Siamini kama Ngassa ilikuwa lazima acheze West Ham tu,bali angeweza kucheza popote pale kule Ulaya,lakini amezinduka late,leo anacheza South Africa.
Siamini kama Kapombe angeshindwa kumudu mikikimikiki ya Ligue 1 ambayo imejaa Waswahili ambao "wanajiita" Wafaransa,leo yuko Azam ambayo ni timu bora Tanzania lakini huwezi kuipoteza fursa ya Ulaya kwa ajili ya VPL au AZAM FC.
Pia,wachezaji hawa watatu na wengine,wajaze mikataba ambayo ina vifungu vinavyowaruhusu kutumkia Ulaya kwa ajili ya kusaka malisho bora pindi wapatapo nafasi.
Nawasilisha,
LVG.
5/12/2015
 
ni kweli ndugu lakini mudathit bado kidogo ajakomaa vizuri na alekebishe nidhamu yake
 
kuna habari nimeipata hivi punde kwa faridi musa anaenda slovenia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…