Tanzania ina wagonjwa wa Sikoseli 200,000, ambapo watu 5 mpaka 7 kati ya 100 (chini ya miaka mitano) hufariki

Tanzania ina wagonjwa wa Sikoseli 200,000, ambapo watu 5 mpaka 7 kati ya 100 (chini ya miaka mitano) hufariki

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Serikali kupitia Wizara ya Afya imeingiza ugonjwa wa Sikoseli katika mpango mkakati wa kupambana na magonjwa yasiyoambukiza ili kuweza kupambana nao na kuhakikisha huduma za vipimo na matibabu zinapatikana katika vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe kwa niaba ya Naibu Waziri Dkt. Godwin Mollel wakati wa maadhimisho ya siku ya sikoseli duniani ambayo kitaifa yamefanyika jijini Arusha.

Dkt. Shekalaghe amesema Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kupambana na ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuanzisha kliniki katika Hospitali za wilaya, mikoa, Kanda na taifa hivyo wakati umefika kwa wagonjwa kutosafiri umbali mrefu kutafuta huduma hizo.

“Tunaweka mikakati Wizarani kuwa mwaka ujao wakati tunaadhimisha siku hii tutahakikisha changamoto ya kutafuta huduma umbali mrefu inakua haipo kwani kliniki za Sikoseli zitakua karibu za wananchi lakini pia NHIF kuhakikisha kuwa katika vile vitita huduma hizi zinaingizwa katika bima ya Afya ili waweze kupata huduma hii vizuri kwa sababu huu ni ugonjwa ambao watu wanaishi nao maisha yao yote”. Amesema Dkt. Shekalaghe.

Dkt. Shekalaghe ameongeza kuwa Tanzania ni nchi ya tano Duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wenye Sikoseli ambapo kila mwaka wanazaliwa watoto 11,000 na mpaka Sasa idadi ya watu wenye sikoseli ni 200,000 ambapo watu 5 mpaka 7 kati ya 100 waliopo chini ya miaka mitano hufa kwa sababu mbalimbali kutokana na madhara yanayosababishwa na Sikoseli.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Silvia Mamkwe ameitaka jamii kuondoa mila potofu juu ya ugonjwa wa Sikoseli badala yake wazingatie kufanya vipimo wakati wa kupata wenza ili kuepuka kuoana wote wakiwa na vinasaba vya Sikoseli vinavyofanana hali itakayosaidia kutozaa watoto wenye ugonjwa huo.

“Huwezi kujijua kama una ugonjwa huu bila kupima hivyo tukate hii cheni ya kuendelea kurithi kwa kupima, kwani Serikali peke yake haiwezi ni muhimu tukashirikiana na jamii kumaliza tatizo hili”. Amesema Dkt. Mamkwe.
 
SICKLE CELLS RED BLOOD CELLS KEEPING DR SEBI'S

HEALING & LEGACY ALIVE IT IS THE DEPRIVATION OF IRON FLUORINE SICKLE CELL ANEMIA IS WHEN THE BLOOD PLASMA

HAS BEEN BROKEN DOWN BY MUCOUS INTO A SICKLE MUCOUS SINKS INTO THE PLASMA INTO THE CELL ITSELF BREAKS AND DISUNITES THE CELL

REMOVING THE MUCOUS THE CELL UNITES AGAIN TO MAINTAIN THAT LEVEL YOU HAVE TO FEED THE PATIENT

LARGE DOSES OF IRON PHOSPHATE NOT FERROUS OXIDE -

DR SEBI ON SICKLE CELL ANEMIA IT IS IMPOSSIBLE FOR YOU TO GET SICK IF YOUR IRON LEVEL IS UP TO PAR IF YOU HAVE A DISEASE

NO MATTER WHAT KIND OF DISEASE IT IS YOU ARE ANEMIC IRON IS

THE MINERAL THAT CONVEYS OXYGEN TO THE BRAIN IRON SHOULD HAVE CARBON HYDROGEN AND OXYGEN

THE CHO CHAIN IRON IS THE SPARK PLUG OF THE HUMAN BODY WHEN YOU ARE DEFICIENT IN IRON YOU ARE SUSCEPTIBLE TO A WHOLE BUNCH OF DISEASES

IRON FIRES THE BODY UP AND IS THE ONLY MINERAL ON THE PLANET THAT IS MAGNETIC BEING THAT IRON IS MAGNETIC IT HAS A TENDENCY

TO PULL OTHER MINERALS TO IT IT PULLS MAGNESIUM ZINC GOLD CALCIUM PHOSPHOROUS ETC

IT WOULD BE SAFE TO SAY THAT WHEN YOU TAKE LARGE DOSES OF IRON

THAT YOU ARE TAKING ALL THE OTHER MINERALS THE LACK OF IRON CAUSES 40 MANIFESTATIONS OF DISEASE

WITHOUT IRON THE BODY LOOSES ENERGY AND THE IMMUNE SYSTEM BEGINS TO GIVE WAY THERE IS NO OXYGEN GOING TO THE BRAIN

WHEN IRON IS LOW WITHOUT IRON WE WRINKLE AT A YOUNG AGE AND NO LONGER ABLE TO WALK STRAIGHT~

DRSEBI BLACKHEALTHMATTERS BLACKHEALTH IRON PLANTBASED DRSEBIAPPROVED VEGAN RAWVEGAN FRUITARIAN

ALKALINEFOODS PLANTBASEDDIET SWIPE LEFT TO SEE HERBS HIGH IN IRON & POTASSIUM PHOSPHATE

SICKLE CELLS RED BLOOD CELLS KEEPING DR SEBI'S.jpg


 
....."Swipe left to see herbs high in Iron and Potassium Phosphate".

Mkuu Jazia nyama hicho ndiyo kipengele cha muhimu zaidi umekiacha.


azawaizi Shukrani kwa Bandiko!!
 
.... SWIPE LEFT TO SEE HERBS HIGH IN IRON & Potassium Phosphate"......
.......

[emoji39][emoji39]
 
Back
Top Bottom