Tanzania kuokoa shs. trillion moja kwa kuanzisha TRA EFD app


HII NI PROGRAMU NZURI SANA "" IWE INVENTED KWA MACHINGA MAANA NA WAO WAKATI MWINGINE WANAUZA BIDHAA AMBAZO NI SAWA NA ZILE ZA MADUKANI TENA KWA BEI KUBWA TU""
TAIFA LITA SONGA MBELE KWA MBINU NA TEKNOLOJIA MBALIMBALI.
Reason behind ni wafanyabiasha wanao hama hama hawana makari maalumu**
N.b,;-hii maana yake kila bidhaa itapaswa kuwa na receipt,aliponunua machinga atapewa receipt na atakapouza atatoa online receipt.
 
Wazo zuri Sana wahusika wakilifanyia kazi hili tutaongeza mapato kwa speed ya radi..pia itawezesha ukuwaji wa digital nchini.
 
Zile ni simu tu, zilizoungwa na printer, ile laki8 ni wizi mtu bei halisi haifiki hata laki3, plus software yake.

Najiulizaga why ile mashine isngekuwa upgraded ikawa inaswip bank card kabisa na kiwa scanned na mobile phone kwenye malipo.

Then TRA watoe punguzo au rejesho kwa mtu atakayelipa saaana online kuliko cash. yaani ukifanya malipo meengi then TRA ikutambue na ikizawadie interms of small amount of money au other benefits.

Wenzetu wanatumia hizo kupunguza mikopo yao bank (%interest inapungua), au ukitaka kupanga nyumba ya serikali unaipata kiurahisiau kununua nyumba za serikali and ......

Lazima wawe wabunifu ili malipo mengo zaidi yafanyike online kuliko cash, inafaid kwa mabank na serikali pia
 
Wakuu hili mbona tayari limeshafanyiwa kazi? Na tayari imeingia sokoni inaitwa SIMPLIFY ni web based system.

Inakuja kuziondoa sokoni mashine za EFD na tunakuja na VIRTUAL FISCAL DEVICE, nadhani hizo EFD hazina maisha marefu ndani ya miaka mitatu zitakua zimeisha.
 
Ile 800,000/= ni mwiba kwa wafanyabiashara wadogo wadogo, mwishowe wanauza bila kutoa receipt na kukosesha mapato
 
Safi sana, tunategemea kuona large scale roll out ya huo mfumo ili tupate matokeo chanya zaidi
 
Monopoly again? Open up api.
 
TRA wanazingua iweje mfanyabiashara apewe TiN namba baada ya mwaka adaiwe tsh 700000/=wakati kumkadilia hiyo kodi bado anastail kias hii wajibu mepesi mnayotupa mfumo wa tra umekupiga fine ya tsh 700000/=huo mfumo wenu ulikadilia lini ?nikashidwa kulipa na ifahamu nina mtaji kiasi gani
 
Monopoly again? Open up api.
Ofcourse it is, kuna systems zinatakiwa kuwa hivyo tu and I do support. Hii njia itakua effective hasa kwa upande wa serikali kukusanya mapato kwa usahihi. Inakuja kuponya mischiefs zote zilizotokana na EFD
 
Hii njia itakua effective hasa kwa upande wa serikali kukusanya mapato kwa usahihi. Inakuja kuponya mischiefs zote zilizotokana na EFD
Wakifungua API itakuwa easy kukusanya mapato kwa sababu watu hawatahitaji kujiunga na mfumo wa TRA ambao ukiwa mmoja matatizo ya Monopoly tuliyoyaona kwenye EFD yatarudi tu in different form.

Weka standards, fungua API acha kila mwenye uwezo ajiunganishe. Which means wenye mifumo ya POS, Accounting, Inventory, et al watakuwa na option ya kuwaunganisha wateja wao bila extra cost. Hii itakuwa faida kwa mteja wa TRA na TRA wenyewe!
 
Ofcourse it is, kuna systems zinatakiwa kuwa hivyo tu and I do support.
Mawazo haya ndiyo yameitia nchi hasara kila kona.
Monopoly inaua ushindani na kufanya huduma ziwe mbaya
Monopoly inaua potential businesses na kupunguza ajira
Monopoly hupandisha bei na kuumiza wateja wa mwisho

Monopoly haijawahi kuwa na faida kwa serikali wala kwa raia. Kama na wewe ni moja ya wataalam wanaoishauri serikali au kuhusika na mifumo, nasikitika kwamba tutaendelea kufeli sana tu kwenye mifumo kama hii. Na kwa maana hiyo sitarajii jipya kwenye huo mfumo ujao. Utakuwa na matatizo yaleyale ila tu yatakuwa kwenye form tofauti!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…