Tanzania kushirikiana kijeshi na Iran



Nadhani huyu Hussein Mwinyi anataka kufuata nyayo za baba yake Raisi mstaafu Ali Hassan Mwinyi kufufua uhuasiano ule wa Kijeshi na Iran uliokuwa na agenda za hovyo za siri miaka ile ya Raisi Ali Hassan Mwinyi wakati ule waziri wa Ulinzi akiwa Abdulrahman Kinana.Kipindi kile activities za wairan zilikuwa nyingi sana kwenye kuanzia kijeshi,KISIASA,KIDINI n.k Na agenda zao zilijaribu kupenyezwa hadi jeshini.

Anyway yale mashamba ya mradi wa kilimo cha umwagiliaji ya Wairan yaliishia wapi?

Hatujasahau na hatutarajii kusahau yaliyotokea na tutafuatilia kwa makini mno yatakayotokea .

Lakini ni vizuri Huyu Hussein Mwinyi anayeweweseka akiota kuwa Raisi wa Zanzibar akamuulize baba yake na waziri Kinana nini kilitokea kwao kutokana na jeuri zao za kujifanya vichwa ngumu wa kuendekeza upuuzi wa Iran.

Huyu Mtoto wa Raisi mstaafu Mwinyi anachofanya ni kuendeleza pale baba yake alipoishia.Anataka ku-revive zile ajenda za Baba yake na za Kinana ndani ya Jeshi na Usalama wa Taifa.

Anyway kwa sasa nadhani wananchi wako more prepared kukabiliana na chochote kibaya kiwe cha kutoka Iran au kwingineko kokote ambako huyo mtoto wa Mwinyi atatia sahihi zake kwa kwenda mwenyewe kwa nafsi yake au kwa kutumwa na yeyote mwenye cheo au asiye na cheo.

Swali la mwisho la kujiuliza ni je mfupa uliomshinda fisi mbwa atauweza?
 
Yaan hawa ndio ma analysts za JF?

halafu baadae mnalalamika kushuka kwa debate standards JF...naona kila kukicha graph inazidi kuteremka.

NAONA HATA MWANZILISHI KAAMUA KUKIMBIA MAANA ANAJUA KUNA WATU WAMEKAA STANDBY KUMJIBU
 
Rais wao ni MSAFI kwa viwango vya Mwalimu alivyokuwa hapa kwetu.
 

Mkuu Moshi,

Kama hivyo ndivyo, Iran haikuanza leo hizo taratibu zake ambazo wewe uko against nazo, na kwa vile uhusiano wetu na Iran umekuwepo kwa muda mrefu, Je, ni kwanini hujalisema hilo huko nyuma na umeamua kulisema sasa kana kwamba wewe umekuwa mwanasiasa? Endapo kama ulikwisha lisema basi tuweke ushahidi hapa na hatua ambazo tayari umezifikia.

Pili, Je una ushahidi gani ambao unaweza kutuonesha hapa JF kwamba maamuzi ya waziri Mwinyi hayakupitia katika ngazi zinazostahili?

Tatu, as a rule of thumb, tueleze vya kutosha kuwa ni kwanini hadi leo hujapinga kuwekwa kizuizini wa wale watu pale Guantanamo?

Nee, Je unakubaliana na mimi kuwa Marekani hairuhusu waislam ndani ya Marekani ku-exercise baadhi ya mambo ambayo dini yao inawaruhusu?
 
Kwa nini tuwe na uhusiano wa karibu kiasi hiki wa kijeshi na iran? tunahitaji nini kutoka iran? Je iran kuna technolojia ya hali ya juu kiasi gani kuweza kulisaidia jeshi letu? Je ni kwa nini ziara ya Mwinyi kwenda Iran kwa jambo nyeti kwa usalama wa nchi yetu haijatangaza na vyombo vya ndani na hasa vile vya serikali? Je, Jeshi la Iran lina majukumu gani katika kutekeleza usimamiaji wa amani na ushiriki katika ulinzi wa amani duniani ( What are the roles of Iranian army in other countries especially afrika and peace keeping)? Je iran ilishawahi kushiriki katika operasheni mbalimbali za kulinada amani au kusaidia watu katika mataifa mbalimbali? Ni upi msimamo wa Iran katika masuala mbalimbali ya kiusalama duniani? Ni upi msimamo wa Iran huko mashariki ya kati? Ni upi msimamo wa iran kuelekea uwepo wa taifa la israel? Je kuna miradi yoyote inayofadhiliwa na iran hapa nchini? Je kuna masharti yoyote ambayo ni sharti yatimize ili kuwezesha hiyo misaada kutolewa? Ni upi mchango wa iran katika bajeti zetu za kila mwaka? Je kuna masharti yoyote yaliyotolewa kuhusiana na mkataba huu wa kijeshi? Je, ni muhimu kiasi hicho kuingia katika mkataba na jeshi la nchi linalopinga uwepo wa taifa lingine katika ramani ya dunia na jeshi lililo katika mivutano na mataifa mbalimbali kuhusu masuala ya kiusalama?

Nachelea kusema, huku ni kukukurupuka.
 
Wanajiandaa na uchaguzi wa mwaka 2010 Tanzania Zanzibar.Mpaka hapo sihitaji kuongea zaidi coz Wa-IRAN wamekuwa msaada sana kwa kambi yao
 


Iran imetajwa na Marekani kuwa ni kitovu cha Uovu pamoja na N. Korea. Sasa kujiingiza kwenye ushirika huu naona ni hatari kwetu. Isitoshe Iran imeshatangaza kuwa Israel ifutwe kutoka kwenye ramani ya dunia na nia yake ni kuiangamiza Israel; mimi nahisi ni hatari sana kujiingiza kwenye mahusiano ya Kijeshi na Iran kwa kuzingatia kauli za Rais wao na kuunga kwa mkono magaidi kama vile Hamas na Hizbollah.
 

Kama unaangalia swala hili kwa mtizamo wa kidini unaweza kupotea kabisa. Ukumbuke kuwa Wairan sio watu wanaopenda shari wao walianza kubanwa na Marekani, na sasa wanatafuta sehemu ya kupumulia na sehemu ya kuwawezesha kutoa ujumbe kuwa hali hiyo wameichoka.
Sisi ni umaskini wetu labda na uvivu wetu w kutumia akili kama alivyosema mkapa ndio unatufanya tuanze kushirikiana na hili dola la kishetani. Lakini mkuu unahakika kama Algeria na Egypt ni nchi za Kiislamu?
 
Sijawahi kuona thread hata moja yenye chembe chembe za udini ambayo iliishia vizuri...

Anyway nina swali moja tu?

Kama munayolalamika ni ya kweli na inabidi yafanyiwe kazi... naomba majibu ya maswali yangu hapo chini?

1. Munafahamu tuna uhusiano wa Kibalozi na Iran?
2. Nchi ambayo muna-uhusiano wa Kibalozi si maana yake munashirikiana kwenye nyanja fulani fulani?
3. Je mambo ya sheria za ndani ya Nchi zinawahusu nini watu wa taifa lingine?

4. Je kama mambo ya ndani ya nchi yangekuwa kigezo... Iran si isingekuwa na uhusiano na nchi zote isipokuwa zile zinazoamini upande wake?

Imani yangu kwamba mashirikiano yanayofanyika ni ya two soverign states... katika nyanja walizokubaliana... sio nyanza za dini na kadhalika... ndio maana Tanzania inauhusiano na Vatcan na hilo sio tatizo kwa sababu ni kwa maslahi yale tu ya kitaifa sio ya kidini

<<<OUT and OVER<<<

NB: Naona vita ya ufisadi imeisha sasa vita ya kidini,,, yaani na ugonjwa wa kunyooshea watu vidole... utafanya hivyo mpaka uingie kaburini.
 


Wewe ulitegemea nini baada ya ndugu na jamaa kupelekwa Kisutu. Wengine walidhani mafisadi ni kabila jipya katika Tanzania kumbe ni baba, mama, dada, kaka, mjomba n.k. Ilikuwa ni siasa kama kawaida yake ...

Kuhusu Iran: Ningependa ushirikiano ulenge katika kupata teknolojia ya kinyuklia maana haya mambo wanayotufanyia TANESCO si mambo. Nadhani wameshindwa kabisa katika teknolojia za Hydro, etc.
 
Anafwata nyao za Mzee wake ruksa, enzi zake alikwenda Iran kutafuta msaada wa mafuta na nchi ikawa inamlipa Iran kahawa, nadhani kwa sasa huko wamefuata vifaa zaidi ya mafunzo kwani zana za kijeshi ni ghali sana.
 
As much as napenda urafiki na mataifa mbalimbali duniani nisingekimbilia kuunda uhusiano wa kijeshi na Iran.

hivi kwani hakukuwa na kungine cha kuhusiana zaidi ya kijesi tuu kwa mfano kibiashara???
 
Dunia sasa imebadilika, hata Marekani nao wanatafuta njia za kuwasiliana na Iran moja kwa moja bila kuwepo na vikwazo jambo ambalo wakati wa George Bush halikuwepo. Barack Obama ameahidi katika kampeni yake ya urais na sasa anataka kufanya kwa vitendo tazama katika Foreign Policy kwa hiyo kwa mheshimiwa Mwinyi sidhani kama kuna tatizo.


Diplomacy: Barack Obama supports tough and direct diplomacy with Iran without preconditions. Now is the time to use the power of American diplomacy to pressure Iran to stop their illicit nuclear program, support for terrorism, and threats toward Israel. Obama and Biden will offer the Iranian regime a choice. If Iran abandons its nuclear program and support for terrorism, we will offer incentives like membership in the World Trade Organization, economic investments, and a move toward normal diplomatic relations. If Iran continues its troubling behavior, we will step up our economic pressure and political isolation. In carrying out this diplomacy, we will coordinate closely with our allies and proceed with careful preparation. Seeking this kind of comprehensive settlement with Iran is our best way to make progress.
 
Mwinyi alisoma Medicine kule ndo maana ana interest!

Kama huna ushahidi kaa kimya, Mwinyi Hakusoma Iran....kawaulize waliokutuma kasoma wapi!!! au waulize wabunge wenzake au waliokaribu...

ni chuki au ndio mtindo wa kujiongeze posts ukifikisha xyx upewe Hongera...Maana baadhi ya watu wa JF tumekuwa kama watu wa CCM, vya kusubiri ngonjera!!!
 

Kaka punguza Chuki...Hivi China kuna Haki za Kibinaadamu...? Kuna DINI yoyote inayoruhusiwa Huko?...wafuasi wa DINI wote wapo limited na wengine huishia Jela au kuuwawa!!!...
China Hakuna Democrasia....leo mbona uhusiano wao unakuzwa?...na wachina waja Bongo hadi kuja kuuza njugu na pirates CD na macomputer mabovu bongo...? ila kwako IRAN tatizo....? kuwa mtu huru...kaka!!!

Tafuta uulize...IRAN ni tofauti kabisa na namna walivyo waarabu...Wao wamekuwa DOLA kabla ya waarabu...for your information wairan wanataka kufananana na wachina ktk sense ya kuwekeza na bila kutegemea watu wengine...

Tafuta maendeleo ya IRAN uyajue...for me sina tatizo kama GOT itawekeza vema kama wenzetu, na wajifunze mazuri ya Nje wayalete Home..na si kuwa visitors kwenda kusign guest book....na kula pesa bure!!!...

Bahati mbaya safari za Viongozi wetu za Nje mafanikio yake ni Madogo sana....!!!
 


Afadhali wewe umesema iliyo kweli, suala hapa ni uislam na chuki za Mwanakijiji, Philemon Mikael, Augustine Moshi et al...



Hapa ni udini kwa kwenda mbele... kwa hiyo wakisema Marekani nchi fulani ni kitovu cha uovu ndio sahihi? au "ulimwengu" ukitamka fulani ni gaidi ndio sahihi? well. Nelson Mandela aliitwa gaidi na "ulimwengu" leo hao hao "walimwengu" wanamjengea minara ya heshima nchini kwao kama shujaa...

Semeni linawalo wasumbua acheni kuzunguka m-buyu ebo!
 
Yaan hawa ndio ma analysts za JF?

halafu baadae mnalalamika kushuka kwa debate standards JF...naona kila kukicha graph inazidi kuteremka.

NAONA HATA MWANZILISHI KAAMUA KUKIMBIA MAANA ANAJUA KUNA WATU WAMEKAA STANDBY KUMJIBU

Yaah right! I know standards of late have slip abit down here, but damn! this is beneath low....
 
Last edited:
This thread bares the hallmarks of American propaganda and stupidity... just from the way defense is spelt lol.. Wamarekani, supposedly the greatest nation on Earth cant differentiate between defence and defense... Tanzania wanashirikiana na nnchi kibao, ambazo haziongelei kuuwa watu like the Iranian president talked about.. they actually DO IT.. but thats not news.. coz Iran is the Devil.. (a bronze age mythological figure)... this is BS.
 
I suggest, among others a summary of all these be made and hand talk on cost-benefit analysis of the same be tabled among the 2010 Presidential contestants.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…