Tanzania Kutomtambua Mugabe: Je, Unaunga Mkono Serikali Yetu au Huungi? Piga Kura..

Tanzania kutomtambua Mugabe, unaunga mkono tamko la serikali au hauungi?

  • Haujali, lolote na liwe

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    33
  • Poll closed .
At least umekiri kwamba Miafrika iko nyuma sana (kwa kila kitu).....

Ndiyo Nyani nimekiri, lakini naipongeza baadhi ya miafrika hii pale inapoonesha kuchachafywa na yale yanayoizunguka na kuonesha moyo wa kuweza kujikomboa yenyewe... ndiyo maana naiunga mikono na kushiriki katika yote ninayoamini yataisaidia miafrika hii katika kuleta maendeleo yake....

Miafrika mingi iko nyuma Ngabu, lakini iliyo nyuma zaidi ni ile inayokubali kumeza yoyote yale mizungu inayowarushia....na kusema mambo ndiyo yalivyo, kwa vile miafrika myenzetu iliyo mingi haijitambui na haijui kama iko nyuma wala mbele, basi ni bora kujiunga nayo na kukubali hivi ndivyo ilivyo nami ngoja niwe kama hiyo hiyo...
 

Sidhani kama Miafrika mingi ingekuwa inameza kila kitu kinachorushwa na mizungu Afrika ingekuwa jinsi ilivyo maana Mizungu inarusha Demokrasia, utawala wa sheria, utawala bora, uhuru wa mawazo/ maoni na kujieleza, haki za binadamu, uhuru wa vyombo vya habari, chaguzi zilizo huru na haki, na mengine mengi tu. Ni Mizungu michache mno inayosemaga (at least hadharani) kuwa Miafrika Ndivyo Tulivyo. Mizungu mingi inatutia moyo kila siku kuwa tunaweza kabisa kupiga vita umaskini. Mizungu mingi inatusaidia sana na misaada ya maendeleo. Isingekuwa kwa Mizungu mimi na wewe pengine tungekuwa tunachunga ng'ombe na mbuzi tu sasa hivi. Ni Miafrika yenyewe ndiyo chanzo cha mabalaa ya Afrika. Ukiliuliza leo LiMugabe au LiKibaki litakuambia kuwa Mizungu ndiyo ya kulaumiwa na ndio chanzo cha matatizo Afrika.
 
NN, naomba kurekebisha pale niliposema nimekiri... nimegundua kuwa ulisema 'kwa kila kitu'...... ukiwa umemaanisha haya maneno kwa kila kitu, mimi naondoa kukiri kwangu kwa asilimia 100% kama vile inaweza kuashirika kwa kusema tu 'nimekiri.'

Sababu za kutokiri kwa 100% ni nyingi... zinahitaji maelezo yake marefu na sidhani kama nitaweza kuandika na kuyaelezea kinaga ubaga kwa kifupi... hivyo nayastahi maelezo hayo.
 

Na mimi naomba nirekebishe/ nibadilishe hayo maneno "kwa kila kitu" na badala yake niweke "katika mambo mengi".....niwie radhi kwa kupigwa chenga na lugha....
 
Umesikia wapi Tanzania kutomtambua Mugabe?

Tofautisha Tanzania na African Union.

Niwekee sehemu wanasema "Tanzania haitambui Zimbabwe." Naongelea independent decision ya Tanzania, siyo inayo flow by default as a member of AU.

mkuu joka kuu ametuletea hii kwenye thread nyingine. sasa wapi au imesema haimtambui mugabe?



naamini sentensi hiyo inamaana au inamtambua mugabe kama raisi wa zimbabwe. vinginevyo wangesema "encourage parties..." au kitu kinachofanana nacho. ni muhimu kuzingatia kwamba reference ya "presidenti mugabe" ipo namba 1.

ndio maana naamini serikali ingefuata njia nyingine kutatua huu mgogoro na wala sio kusema usikike tena baada ya kutoka kikao kikuu cha au ambapo tz ni mwenyekiti.
 

Lakini title ya president si huwa ipo, kama ishara ya heshima kwa maraisi wa zamani?, mfano wakati mwingine Mandela huwa wanamuita president Mandela, au President Carter, President Clinton n.k, kwa hiyo sidhani kama kwa statement hiyo eti Mugabe katambuliwa rasmi
 

huwezi kumuita mtu "president" kwenye document rasmi ya mkutano rasmi wa nchi wanachama. ninahakika ujumbe wa zimbabwe uliliona hilo wakati wa majadiliano ya hiyo document. siamini kama wote walioshiriki uandishi wa hiyo document walipigwa "bao" bali wamefanya hivyo wakijuwa wazi maana yake ni kumtambua mugabe kama president.

kwa kweli bado naamini tz imekosea kutoa tamko lake kwani naamini kulikuwepo na njia nyingine bora zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…