Mirrey Nchimbi
New Member
- Jul 19, 2022
- 3
- 5
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...!
Ni kawaida kusikia Tanzania kufananishwa na nchi mbalimbali barani Afrika hasa katika nyaja za kiuchumi, kisiasa, kijamii na utamaduni. Na tumeziona nchi za Magharibi kama mfano katika nyanja hizo na muda mwingine imekuwa ngumu kujilinganisha nao. Hii ni kwa sababu nchi hizo za Magharibi zimepiga hatua kubwa za kimaendeleo katika sekta mbalimbali. Tanzania haipo pabaya sana, kama tunavyofikiria, mfumo wa elimu ukifanyiwa maboresho kadhaa utafanana na kuwa na mchango chanya kama ule wa Singapore.
Singapore ni moja ya nchi duniani inayosifika kwa mfumo bora wa elimu. Kabla ya Singapore kufikia mafanikio haya, mfumo wake wa elimu ulikuwa unafanana kabisa na mfumo wa Tanzania hivi sasa. Singapore ni mfano bora kwani historia zetu zinashabihiana; nchi zote mbili zilitawaliwa na Uingereza, Singapore ilipata Uhuru mwaka 1965 na Tanganyika mwaka 1961, huku Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikua mwaka 1964.
Yafuatayo ni mabadiliko mbalimbali yaliyofanywa na Serikali ya Singapore ili kuboresha mfumo wa elimu nchini humo, ambayo yakichukuliwa kwa uzito ndio majibu ya changamoto zinazokabili sekta ya elimu Tanzania;
Elimu na Maisha; Baada ya kupata uhuru (1965), elimu iliyotolewa nchini Singapore ilikuwa na lengo la kutoa wafanyakazi wenye ujuzi mbalimbali ili kwendana na kasi ya ukuaji wa sekta ya viwanda duniani. Hivyo basi, elimu rasmi ilitolewa ikiambatana na elimu ya ufundi. Lakini pia lugha ya kiingereza ilipewa kipaumbele kama lugha ya kwanza ili kuongeza nafasi ya wananchi wao kuajiriwa katika nchi mbalimbali duniani kwani Kiingereza ni lugha ya Kimataifa hivyo kusaidia wahitimu kutoka Singapore kuwa na nafasi kubwa kuajiriwa katika nchi za magharibi kulinganisha na nchi nyingine zilizoko bara la Asia. Tanzania pia, mnamo mwaka 1967 ulianzisha mfumo wa elimu ya kujitegemea. Tofauti iliopo ni kuwa lengo la elimu ya kujitegemea ni kutumia rasilimali zilizopo nchini kuikomboa nchi na kuboresha maisha ya Mtanzania mmoja mmoja. Elimu hiyo haikulenga kuteka soko la kimataifa kama ile ya Singapore.
Elimu na ubora wa kazi; Baadae ikaja kuonekana kuwa, mfumo ule wa elimu uliweza kuzalisha wafanyakazi katika nyanja mbalimbali lakini ubora wa ufanyaji kazi wao ulikua hauridhishi. Hivyo Serikali ya Singapore, ikaboresha tena mfumo wa elimu nchini humo kwa lengo la kuongeza ufanisi wa wafanyakazi waliokuwepo nchini humo, lakini pia kuhakikisha kuwa wanafunzi walioko shuleni, vyuo vikuu na vyuo vya ufundi wanahitimu wakiwa na uwezo wa kufanya kazi kikamilifu pale watakapoajiriwa au kujiajiri. Kabla ya maboresho haya kufanyika katika mfumo wa elimu ya Singapore ilionekana kuwa wafanyakazi nchini humo hawakuweza kushindana katika soko la ajira, na wafanyakazi wa mataifa mengine kama Amerika na Japan.
Maboresho yalijikita kuongeza ubora wa elimu ya ufundi na viwanda, lakini pia kusaidia wanafunzi ambao kwa namna moja au nyingine walishindwa kufaulu vizuri ili kuweza kuingia katika soko la ajira au kujiajiri. Tanzania pia ina programu mbalimbali zinazoweza kuambatana na semina elekezi kwa lengo la kutoa ujuzi fulani kwa wafanyakazi hao. Lakini hakuna mpango wa kudumu kama ule wa Singapore kuhakikisha kuwa hata wanafunzi ambao bado hawajaingia katika soko la ajira kuwa na ufanisi katika kazi zao lakini kuwawezesha kushindana kimataifa. Kwani Tanzania inashindana kimataifa katika la soko la ajira na nchi mbalimbali katika jumuiya ya Afrika mashariki , Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Umoja wa nchi za Afrika na duniani kwa ujumla. Ni muda muafaka kwa Tanzania kutengeneza kizazi ambacho kitakuwa kimelimika na wabunifu kama ilivyo Singapore.
Elimu kama mfumo wa Maisha; Badiliko hili lililofanywa na Singapore, ni mpango wa kudumu wa kufanya elimu kuwa mfumo wa maisha wa kila siku ya watu wake wa rika zote. Kwa kuendeleza mikakati ya kuongeza ujuzi, ubunifu na uvumbuzi katika nyanja mbalimbali hasa uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kiujumla. Singapore imeweza hili, kwa kupunguza msisitizo na mkazo kwenye mitihani ya kuandika shuleni na katika taasisi mbalimbali za kujifunzia kama vyuo vya ufundi na vyuo vikuu. Na kuweka mazingira madhubuti ya kupima uelewa wa wanafunzi wao kwa vitendo, lakini kumsaidia mwanafunzi kufurahia na kufanya kwa majaribio vile anvyofundishwa darasani. Hivyo kuongeza chachu ya kusoma zaidi , kuwa wabunifu na kuvumbua stadi mbalimbali zinazohusiana na masomo husika. Msisitizo huu, haujajikita kwenye masomo rasmi pekee. Sekta kama michezo, saana na mambo mbalimbali ya kijamii yanapewa kipaumbele.
Hivyo kuongeza wigo wa ajira binafsi kupelekea kupunguza wimbi la kukosa ajira kwa vijana nchini Singapore. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakitu cha kujifunza hapa ili kuboresha mfumo wa elimu utakaopelekea matokeo chanya ikiwemo kupunguza wimbi la vijana kukosa ajira, kuwa na kizazi kinachotambua umuhimu wa elimu katika maisha, na sio umuhimu wa vyeti tu.
Nini kifanyike Tanzania iwe kama Singapore?
Kuboresha mitaala ya masomo katika shule za awali na msingi. Elimu ya awali “ chekechea” kama tulivyozea kusema ni muhimu sana katika kuweka msingi mzuri wa kielimu kwa watoto wanaoanza shule. Waswahili wanasema “Samaki mkunje, angali mbichi” , mitaala ya masomo katika shule za awali na msingi zimuandae mtoto wa Kitanzania kupenda shule na kutambua umuhimu wa elimu kama hazina yake binafsi na taifa zima na sio kama nyenzo ya ajira rasmi maana vijana wengi wanahitimu vyuo na vyuo vikuu wakiwa na mategemeo ya ajira rasmi na sio kutumia elimu na ujuzi katika kuletea mabadiliko chanya katika jamii zao, na kuwaletea faida kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
Lakini pia, kuhakikisha viwango na ujuzi wa walimu na wakufunzi katika taasisi mbalimbali za elimu. Ubora wa elimu inayotolewa shuleni na vyuoni una uhusiano wa karibu na uwezo wa walimu husika. Ubora wa walimu usipimwe tu kwa kuangalia ufaulu wao lakini namna wanavyowasilisha mada za masomo kwa wanafunzi. Kuwajengea uwezo walimu, kuwasilisha mada kwa vitendo hasa katika masomo ya Sayansi na Teknolojia.
Kuona Sanaa kama fursa.
Serikali, kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kuandaa mpango maalumu wa kuratibu na kupima uwezo wa vijana kwenye sekta hii ili kuweza kuongeza nafasi za ajira na kujiari.
Kusema Tanzania kama uko Singapore, inawezekana!
Ni kawaida kusikia Tanzania kufananishwa na nchi mbalimbali barani Afrika hasa katika nyaja za kiuchumi, kisiasa, kijamii na utamaduni. Na tumeziona nchi za Magharibi kama mfano katika nyanja hizo na muda mwingine imekuwa ngumu kujilinganisha nao. Hii ni kwa sababu nchi hizo za Magharibi zimepiga hatua kubwa za kimaendeleo katika sekta mbalimbali. Tanzania haipo pabaya sana, kama tunavyofikiria, mfumo wa elimu ukifanyiwa maboresho kadhaa utafanana na kuwa na mchango chanya kama ule wa Singapore.
Singapore ni moja ya nchi duniani inayosifika kwa mfumo bora wa elimu. Kabla ya Singapore kufikia mafanikio haya, mfumo wake wa elimu ulikuwa unafanana kabisa na mfumo wa Tanzania hivi sasa. Singapore ni mfano bora kwani historia zetu zinashabihiana; nchi zote mbili zilitawaliwa na Uingereza, Singapore ilipata Uhuru mwaka 1965 na Tanganyika mwaka 1961, huku Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikua mwaka 1964.
Yafuatayo ni mabadiliko mbalimbali yaliyofanywa na Serikali ya Singapore ili kuboresha mfumo wa elimu nchini humo, ambayo yakichukuliwa kwa uzito ndio majibu ya changamoto zinazokabili sekta ya elimu Tanzania;
Elimu na Maisha; Baada ya kupata uhuru (1965), elimu iliyotolewa nchini Singapore ilikuwa na lengo la kutoa wafanyakazi wenye ujuzi mbalimbali ili kwendana na kasi ya ukuaji wa sekta ya viwanda duniani. Hivyo basi, elimu rasmi ilitolewa ikiambatana na elimu ya ufundi. Lakini pia lugha ya kiingereza ilipewa kipaumbele kama lugha ya kwanza ili kuongeza nafasi ya wananchi wao kuajiriwa katika nchi mbalimbali duniani kwani Kiingereza ni lugha ya Kimataifa hivyo kusaidia wahitimu kutoka Singapore kuwa na nafasi kubwa kuajiriwa katika nchi za magharibi kulinganisha na nchi nyingine zilizoko bara la Asia. Tanzania pia, mnamo mwaka 1967 ulianzisha mfumo wa elimu ya kujitegemea. Tofauti iliopo ni kuwa lengo la elimu ya kujitegemea ni kutumia rasilimali zilizopo nchini kuikomboa nchi na kuboresha maisha ya Mtanzania mmoja mmoja. Elimu hiyo haikulenga kuteka soko la kimataifa kama ile ya Singapore.
Elimu na ubora wa kazi; Baadae ikaja kuonekana kuwa, mfumo ule wa elimu uliweza kuzalisha wafanyakazi katika nyanja mbalimbali lakini ubora wa ufanyaji kazi wao ulikua hauridhishi. Hivyo Serikali ya Singapore, ikaboresha tena mfumo wa elimu nchini humo kwa lengo la kuongeza ufanisi wa wafanyakazi waliokuwepo nchini humo, lakini pia kuhakikisha kuwa wanafunzi walioko shuleni, vyuo vikuu na vyuo vya ufundi wanahitimu wakiwa na uwezo wa kufanya kazi kikamilifu pale watakapoajiriwa au kujiajiri. Kabla ya maboresho haya kufanyika katika mfumo wa elimu ya Singapore ilionekana kuwa wafanyakazi nchini humo hawakuweza kushindana katika soko la ajira, na wafanyakazi wa mataifa mengine kama Amerika na Japan.
Maboresho yalijikita kuongeza ubora wa elimu ya ufundi na viwanda, lakini pia kusaidia wanafunzi ambao kwa namna moja au nyingine walishindwa kufaulu vizuri ili kuweza kuingia katika soko la ajira au kujiajiri. Tanzania pia ina programu mbalimbali zinazoweza kuambatana na semina elekezi kwa lengo la kutoa ujuzi fulani kwa wafanyakazi hao. Lakini hakuna mpango wa kudumu kama ule wa Singapore kuhakikisha kuwa hata wanafunzi ambao bado hawajaingia katika soko la ajira kuwa na ufanisi katika kazi zao lakini kuwawezesha kushindana kimataifa. Kwani Tanzania inashindana kimataifa katika la soko la ajira na nchi mbalimbali katika jumuiya ya Afrika mashariki , Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Umoja wa nchi za Afrika na duniani kwa ujumla. Ni muda muafaka kwa Tanzania kutengeneza kizazi ambacho kitakuwa kimelimika na wabunifu kama ilivyo Singapore.
Elimu kama mfumo wa Maisha; Badiliko hili lililofanywa na Singapore, ni mpango wa kudumu wa kufanya elimu kuwa mfumo wa maisha wa kila siku ya watu wake wa rika zote. Kwa kuendeleza mikakati ya kuongeza ujuzi, ubunifu na uvumbuzi katika nyanja mbalimbali hasa uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kiujumla. Singapore imeweza hili, kwa kupunguza msisitizo na mkazo kwenye mitihani ya kuandika shuleni na katika taasisi mbalimbali za kujifunzia kama vyuo vya ufundi na vyuo vikuu. Na kuweka mazingira madhubuti ya kupima uelewa wa wanafunzi wao kwa vitendo, lakini kumsaidia mwanafunzi kufurahia na kufanya kwa majaribio vile anvyofundishwa darasani. Hivyo kuongeza chachu ya kusoma zaidi , kuwa wabunifu na kuvumbua stadi mbalimbali zinazohusiana na masomo husika. Msisitizo huu, haujajikita kwenye masomo rasmi pekee. Sekta kama michezo, saana na mambo mbalimbali ya kijamii yanapewa kipaumbele.
Hivyo kuongeza wigo wa ajira binafsi kupelekea kupunguza wimbi la kukosa ajira kwa vijana nchini Singapore. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakitu cha kujifunza hapa ili kuboresha mfumo wa elimu utakaopelekea matokeo chanya ikiwemo kupunguza wimbi la vijana kukosa ajira, kuwa na kizazi kinachotambua umuhimu wa elimu katika maisha, na sio umuhimu wa vyeti tu.
Nini kifanyike Tanzania iwe kama Singapore?
Kuboresha mitaala ya masomo katika shule za awali na msingi. Elimu ya awali “ chekechea” kama tulivyozea kusema ni muhimu sana katika kuweka msingi mzuri wa kielimu kwa watoto wanaoanza shule. Waswahili wanasema “Samaki mkunje, angali mbichi” , mitaala ya masomo katika shule za awali na msingi zimuandae mtoto wa Kitanzania kupenda shule na kutambua umuhimu wa elimu kama hazina yake binafsi na taifa zima na sio kama nyenzo ya ajira rasmi maana vijana wengi wanahitimu vyuo na vyuo vikuu wakiwa na mategemeo ya ajira rasmi na sio kutumia elimu na ujuzi katika kuletea mabadiliko chanya katika jamii zao, na kuwaletea faida kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
Lakini pia, kuhakikisha viwango na ujuzi wa walimu na wakufunzi katika taasisi mbalimbali za elimu. Ubora wa elimu inayotolewa shuleni na vyuoni una uhusiano wa karibu na uwezo wa walimu husika. Ubora wa walimu usipimwe tu kwa kuangalia ufaulu wao lakini namna wanavyowasilisha mada za masomo kwa wanafunzi. Kuwajengea uwezo walimu, kuwasilisha mada kwa vitendo hasa katika masomo ya Sayansi na Teknolojia.
Kuona Sanaa kama fursa.
Serikali, kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kuandaa mpango maalumu wa kuratibu na kupima uwezo wa vijana kwenye sekta hii ili kuweza kuongeza nafasi za ajira na kujiari.
Kusema Tanzania kama uko Singapore, inawezekana!
Upvote
6