Tanzania Kuwe na sheria inayosimamia Cash Money

AZUSA STREET

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2013
Posts
2,007
Reaction score
1,897
hivi cash economy tz itaisha lini jamani? mtu anaenda dukani na milioni tano, milioni kumi anaenda kufanya shoping na mihela kwenye begi! kwanini tz tusiweke mipaka, mfano: kuanzia manunuzi ya laki tano kwenda juu malipo yafanyike electronically, sheria itungwe na hapo ndipo hata kodi itakatwa vizuri bila kukwepa (pamoja na kwamba hata ufanyeje wabongo hupenda uchochoro na shortcuts na udanganyifu). SHERIA itungwe jamani!
 
hilo nalo neno..
lakini watanzania bado hatuaminiani...cyber crime inazidi kushika kasi.
ushafikiria charges za kufanya hizo transactions?
 
kama alivyosema aliyenitangulia, matumizi ya kielektroniki yatasaidia tu katika kurahisisha manunuzi, lakini issue ya usalama ipo pale pale kwani kuna wizi wa kimtandao...
 
Mmmh hebu usituletee matatizo we nae
 
Naunga mkono hoja huku kubeba mahela cash ni kukaribisha matatizo, huo wizi utachukuliwa kama
changamoto tu, mbona mobile money zina perfom vizuri tu iweje debit card ziogopewe?
 
Watanzania hatuheshimu sheria. wewe itunge tu utaitunza kwenye mafaili huku tukitembea na mihela yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…