Tanzania - Mapendekezo ya mpango wa maendeleo wa taifa wa mwaka 2018/19

Maeneo Mengine ya Kukuza Uchumi na Ujenzi wa Msingi wa Uchumi wa Viwanda
4.6.1 Viwanda
  1. Kupanua na Kuimarisha Shughuli za Shirika la Viwanda Vidogo – SIDO: Mapendekezo yamelenga kuifanya SIDO kuwa ndiyo chombo muhimu katika kuleta mageuzi ya viwanda nchini;
  2. kuendelea kujenga viwanda vinavyotumia malighafi kutoka nchini ikiwemo kilimo, madini na gesi asilia;
  3. kuendeleza viwanda vitakavyozalisha bidhaa mbadala wa zile zinazoagizwa kutoka nje ya nchi;
  4. viwanda vitakavyotoa ajira kubwa kwa makundi yote ya jamii;
  5. kuhakikisha upatikanaji wa mitaji ya kuendeleza viwanda kupitia Benki ya Rasilimali na Benki ya Maendeleo Kilimo na mifuko ya wajasiriamali wadogo;
  6. Kuanzisha na kuendeleza maeneo ya viwanda (Industrial parks) na maeneo ya Teknolojia (Technological Parks);
  7. Kuimarisha uanzishwaji na uendelezaji wa kongane za viwanda vinavyotumia malighafi za mazao ya kilimo na shughuli nyingine za kiuchumi
  8. Kuimarisha na kuzitumia taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Taasisi hizo ni pamoja na: NDC, STAMICO, TPDC, TIRDO, CARMATEC, TEMDO, COSTECH, na Nyumbu na Mzinga.
 
Viwanda vya vyerehani na kukamulia juisi vipi? Saluni naskia paia ni viwanda? Hebu fafanua haya maneno pole pole bila kuheme hema.
 
Long term plans are taboo there.
“A lie can only make a temporary sense. The truth is permanent and lasts forever.”
Ndiyo wakenya wapo katika ulimwengu wa kudangwanywa and fake life. Tanzania we live in a real world.
 
There is 2025 vision, way back before your 2030. Now broken down in 5 yrs term and now a yearly workplan.
Got problem with that?

It may not be a point on right now, thats why it is up for discussion by wabunge.

Me think this Nrb-Dar who's better is bullshit.
 
Kwani hivo viwonder vinajengwa?......sababu hii ni kenya news section pekee

Nashangaa pia! Mbona mleta mada asiweke Uzi huu kwa Tanzania news section. Huko ndiko anaweza hamazisha wenzake na mipango ya viwonder ili wajipange.

Haisaidii Mkenya hii.
 
Miradi ya sekta binafsi viwanda vipya vilivyojengwa:-
  • viwanda vya kuzalisha vifungashio
    • Global Packaging (T) Ltd
    • Madoweka Co. Ltd
  • viwanda vya kuzalisha bidhaa za ujenzi
    • Goodwil Ceramics Ltd
    • Waja General Co. Ltd;
  • viwanda vya kuzalisha vinywaji baridi
    • Saini Food Products Co. Ltd; Sayona Drinks Ltd
  • Viwanda cha kusindika nyama
    • Mitoboto Farmers Co. Ltd
    • Paul Kisivani
  • viwanda vya kuzalisha mafuta ya kula
    • Jielong Mills Ltd
    • Mkongori Oil Mills na Nkupa Oil Mills
    • Super Cooking Oil
    • Mount Meru Millers
 
Hospitali ya Taifa Muhimbili:
kukamilika kwa ukarabati na upanuzi wa vyumba 7 vya upasuaji na kuongeza idadi ya vyumba kufikia 20 katika jengo kuu la upasuaji; kukamilika kwa ukarabati wa vyumba vinne (4) vya upasuaji katika jengo la watoto pamoja na kuweka mfumo wa hewa medical gas piping; kununuliwa kwa mashine 1 ya kisasa ya CT-Scan, mashine 14 za upasuaji (diathermy machines), mashine 2 kubwa za usafishaji vifaa (auto clave machines), vifaa vya usikivu (cochlear implants), mashine za kutolea huduma ya kupandikiza vifaa vya usikivu (audiometer and ABR machine) na lifti 2 kwa ajili ya majengo ya Kibasila na Sewahaji;
 
Viwanda vya vyerehani na kukamulia juisi vipi? Saluni naskia paia ni viwanda? Hebu fafanua haya maneno pole pole bila kuheme hema.
Vp kuhusu Mega projects za kuchora chora. Soon mta electrify SGR kwa kutumia pink paint [emoji28]
 
Yea,just ensure the towels are made in Tanzania and not from China! Fine cotton lint will do!
Unahangaika sana kama kuku anatafuta kutaga mayai. Unatakiwa uwe mpole ili unyolewe vizuri.
 
Shamba la Miwa na Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi:
Ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 7 kwa kiwango cha changarawe kutoka barabara kuu ya Dodoma – Morogoro inayoingia katika kiwanda cha kuzalisha sukari cha Mbigiri;
kununuliwa kwa matrekta 3; na kukamilika kwa usafishaji wa shamba kubwa (ekari 1000) ambapo ekari 320 zimepandwa miwa. Aidha, ujenzi wa majengo ya kiwanda cha sukari unaendelea;
 
Huduma ya Maji Vijijini:
kukamilika kwa ujenzi wa miradi 90 ya maji vijijini na hivyo kufanya jumla ya miradi iliyokamilika kufikia 1,423; ujenzi wa jumla ya vituo vya maji 117,190;

Mradi wa Maji wa Same – Mwanga – Korogwe: kukamilika kwa asilimia 26.3 ya mradi ikiwemo ujenzi wa chanzo; mtambo
wa kusafisha maji; na tanki la kuhifadhi maji;

Mradi wa Maji kwa Vijiji 100 Vinavyopitiwa na Bomba Kuu kutoka Ziwa Victoria, ambapo miradi ya vijiji 14 na upimaji na usanifu wa miradi ya vijiji 32 umekamilika;

Ukarabati na Upanuzi wa Mfumo wa Kusambaza Majisafi Dar es Salaam: ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita 77 umekamilika katika maeneo ya Mbezi na Kiluvya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…