Tanzania na Burundi Kuimarisha Ushirikiano Sekta ya Sheria

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Machi 11, 2025 Jijini Dar Es Salaam amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Burundi nchini Mhe. Leontine Nzeyimana

Katika Mazungumzo yao viongozi hao wamejadiliana mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya Sheria ikiwemo ushirikiano katika kupambana na uhalifu, na masuala ya haki za binadamu baina ya mataifa hayo mawili.

Ikumbukwe kuwa Tanzania na Burundi zimekuwa na uhusiano wa karibu na ushirikiano wa muda mrefu, tangu enzi za waasisi wa mataifa hayo ambapo urafiki wa kidiplomasia umejengwa juu ya msingi wa historia, tamaduni zinazoendana, na maslahi ya pamoja.

 

Attachments

  • Gl6bnP6WwAAyOE9.jpg
    319 KB · Views: 1
  • Gl6bnPoWkAA4W4g.jpg
    284.2 KB · Views: 1
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…