Tanzania na Comoro zaangazia ushirikiano katika TEHAMA

Tanzania na Comoro zaangazia ushirikiano katika TEHAMA

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Kidijitali ya Comoro, Muinou Ahamada.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Balozi Yakubu alimueleza Mtendaji Mkuu Bwana Ahamada kuhusu hatua kubwa ambazo Tanzania imepiga katika kuhakikisha nchi inanufaika na uchumi wa kidijitali ambapo mpaka hivi sasa mapato ya Serikali yamekuwa yakiongezeka kutokana na malipo kufanyika kwa mifumo maalum iliyowekwa. Alimueleza pia uwepo wa mifumo ya utendaji kazi Serikalini ambayo imesaidia kupunguza gharama na kuongeza ufanisi kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake, Bwana Ahamada alieleza utayari wa Comoro kushirikiana na Taasisi za Tanzania kama vile Wakala wa Mtandao Serikalini ( EGA), TCRA ili kuona namna ya kuimarisha Taasisi zao.

Soma Pia: Tanzania na Comoro zajadiliana kuongeza ushirikiano katika Sekta ya Elimu

Aidha, alitoa wito kwa Taasisi binafsi za Tanzania kuangazia fursa za ushirikiano Comoro kwani yako maeneo kadhaa yanatohitaji uwepo wa Sekta binafsi.
IMG-20241030-WA0004(1).jpg
IMG-20241030-WA0006(1).jpg

IMG-20241030-WA0005(1).jpg
IMG-20241030-WA0007(1).jpg
 

Attachments

  • IMG-20241030-WA0008(1).jpg
    IMG-20241030-WA0008(1).jpg
    118.6 KB · Views: 4
Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Saidi Yakubu amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Maendeleo ya Kidijitali ya Comoro, Muinou Ahamada.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Balozi Yakubu alimueleza Mtendaji Mkuu Bwana Ahamada kuhusu hatua kubwa ambazo Tanzania imepiga katika kuhakikisha nchi inanufaika na uchumi wa kidijitali ambapo mpaka hivi sasa mapato ya Serikali yamekuwa yakiongezeka kutokana na malipo kufanyika kwa mifumo maalum iliyowekwa. Alimueleza pia uwepo wa mifumo ya utendaji kazi Serikalini ambayo imesaidia kupunguza gharama na kuongeza ufanisi kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake, Bwana Ahamada alieleza utayari wa Comoro kushirikiana na Taasisi za Tanzania kama vile Wakala wa Mtandao Serikalini ( EGA), TCRA ili kuona namna ya kuimarisha Taasisi zao.

Soma Pia: Tanzania na Comoro zajadiliana kuongeza ushirikiano katika Sekta ya Elimu

Aidha, alitoa wito kwa Taasisi binafsi za Tanzania kuangazia fursa za ushirikiano Comoro kwani yako maeneo kadhaa yanatohitaji uwepo wa Sekta binafsi.
Mkuu ukitoa habari za Balozi Yakub wa Comoro naomba unitag basi ili kama kuna chochote kitu tupate wote mkuu usile mwenyewe neema za balozi Yakubu mkuu
 
Back
Top Bottom