Tanzania na Korea: Ziara ya Rais Samia kufungua fursa mpya kwa Watanzania

Tanzania na Korea: Ziara ya Rais Samia kufungua fursa mpya kwa Watanzania

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya kihistoria nchini Korea Mei 31 hadi Juni 6 mwaka huu kwa mwaliko wa Mheshimiwa Rais wa Korea, Yoon Suk Yeol, ziara ambayo ni hatua muhimu katika kuendelea kudumisha, kuimarisha na kuongeza ushirikiano wa moja kwa moja kati ya nchi hizi, ikiwemo kufungua milango kwa sekta binafsi ya Korea na Tanzania.

Katika ziara hiyo, Mheshimiwa Rais anatarajia kufanya mambo makuu mawili ambapo Juni 2 atakutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Korea, na Juni 4 na 5 atashiriki katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali kati ya Korea na chi za Afrika; mkutano unaofanyika kwa mara ya kwanza kwa ngazi ya wakuu wa nchi na serikali, ambapo awali mikutano ilikuwa katika ngazi ya mawaziri na wataalamu.

Ziara hiyo inatarajiwa kuwa chachu na kutoa msukumo kwa wawekezaji kutoka Korea kuja kuwekeza nchini. Aidha, ushiriki wa Tanzania katika mkutano tajwa unatarajiwa kukuza uhusiano wa kimkakati; kupanua wigo wa biashara na uwekezaji; kutafuta namna chanya ya kukabiliana na changamoto za kimataifa; kutengeneza minyororo ya kimataifa ya usambazaji wa madini na nishati muhimu; na kujenga urafiki wa kudumu.

Wakati wa ziara, Tanzania na Korea zitasaini hati saba za makubaliano zitakazogusa sekta mbalimbali, kufungua soko la ajira kwa Watanzania nchini Korea, kuvutia wawekezaji wa Korea ili wawekeze katika soko la sanaa la Tanzania, kuanzisha ushirikiano na Kituo cha Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Chuo Kikuu cha Korea Aerospace University (KAU) utakaosaidia kuboresha sekta ya anga nchini.

Tanzania na Korea zina uhusiano wa miaka 32 ambapo Korea ni nchi ya 12 kwa uchumi mkubwa duniani ambapo Tanzania ni kati ya nchi saba za Afrika za kipaumbele kwa Korea. Pia, kwa sasa Tanzania ni nchi ya kwanza kupokea kwa wingi misaada (ODA) inayotolewa na Shirika la Maendeleo la Korea (KOICA) na ya pili kupokea kiwango kikubwa cha mikopo ya masharti nafuu (Concessional Loans), fedha ambazo zimekuwa na matokeo chanya kwenye ustawi wa kijamii na kiuchumi.

Aidha, Chuo Kikuu cha Anga cha Korea (Korea Aerospace University (KAU)) kitamtunuku Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honorary Degree) katika Usimamizi wa Sekta ya Anga kwa kutambua mchango wake katika mageuzi ya sekta ya anga ikiwemo kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege, kuwajengea uwezo watumishi na uongezaji wa ndege za abiria na mizigo.

Pia soma Ziara ya Rais Samia Korea Kusini itasaini Mkopo wa Tsh. Trilioni 6.51
 
huyu bibi hackoki?
hakai nchini walau ajue hali ya nchi yake?
mbona hajali mateso ya wananchi?

anyway, huyu na kikwete imekua laana kuu tumelaaniwa kama nchi...... sijui kwanini tunapata viongozi wa ajabu kiasi hiki
 
Ziara muhimu sana, na ya manufaa makubwa sana katika kuchochea biashara, uwekezaji, mafunzo na kuimarisha ushirikiano wa kisiasa, kijamii na kiuchumi baina ya nchi hizi mbili, zenye historia ya kipekee sana duniani :KasugaYeah:

well done madam President, Dr.Samia Suluhu hassan, and I wish you, and your delegations all the best :KasugaYeah:
 
huyu bibi hackoki?
hakai nchini walau ajue hali ya nchi yake?
mbona hajali mateso ya wananchi?

anyway, huyu na kikwete imekua laana kuu tumelaaniwa kama nchi...... sijui kwanini tunapata viongozi wa ajabu kiasi hiki

Mama yupo vyema
Kila mtu ale urefu wa kamba yake

Nchi zote zenye maendeleo zimemwaga damu au kuna mapinduzi ya jeshi ndio heshima na maendeleo yakaja

Sasa nyinyi mnataka maendeleo kupitia JF threads and comment

Never on earth
Viongozi na wananchi wore ni sehemu ya tatizo
 
Kiduku ameigeuza Kusini kuwa dampo la kurushia mazagazaga yake

Kiduku akili hana kabisa 🐼
 
Kama Mtanzania ninaunga mkono ziara ya Mhe. Rais Korea Kusini. Jana kupitia luninga nimeiona ndege ya ATCL ikitua kule Korea Kusini. Binafsi ninaona kusafiri na ndege ile kubwa aina ya airbus ni gharama kubwa sana na tena imebeba watu wachache kuliko uwezo wake. Kwa nini Mhe. Rais asingesafiri na usafiri wa makampuni mengine ya ndege akitumia Business Class?. Gharama ya usafiri aliotumia unaweza kujenga hata vituo vya afya vitatu. Kwenye nchi kama hii ya kwetu Mhe. Rais anatakiwa ajishushe na lengo lake kubwa ni wananchi walio katika lindi la umaskini. Tuwe na uchungu na fedha za umma.
 
Screenshot_20240502-211040.png
 
Ila na sisi wabongo tumezidi hatujui tuna taka nini, angekodi ndege ungesikia bora angesafiri na uber haya kachukua ya Atc kila mtu kawa mchumi ,angeenda na meli aaaah atachelewa si angepanda ndege tu yani ili mradi blah blah
 
Kama Mtanzania ninaunga mkono ziara ya Mhe. Rais Korea Kusini. Jana kupitia luninga nimeiona ndege ya ATCL ikitua kule Korea Kusini. Binafsi ninaona kusafiri na ndege ile kubwa aina ya airbus ni gharama kubwa sana na tena imebeba watu wachache kuliko uwezo wake. Kwa nini Mhe. Rais asingesafiri na usafiri wa makampuni mengine ya ndege akitumia Business Class?. Gharama ya usafiri aliotumia unaweza kujenga hata vituo vya afya vitatu. Kwenye nchi kama hii ya kwetu Mhe. Rais anatakiwa ajishushe na lengo lake kubwa ni wananchi walio katika lindi la umaskini. Tuwe na uchungu na fedha za umma.
Unatafuta ugomvi na Lucas mwashambwa bure,yeye ndiye msemaji wa Rais hapa JF.
 
Akimaliza huko nataka aende Kaskazini. Ni kuvuka mpaka tu! Asije akaanzia Tanzania tena jamaaani!
Nimesikia blaza Kim pia ameanza kutoa mikopo!
 
Back
Top Bottom