Tanzania na Oman Kushirikiana kwenye nishati ya Petroli

Tanzania na Oman Kushirikiana kwenye nishati ya Petroli

Getrude Mollel

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2022
Posts
270
Reaction score
362
Chini ya Rais Samia Suluhu, mipango hivi sasa inasukwa kati ya TANOIL, kampuni tanzu chini ya TPDC na Oman OQ ya Oman kufanya kazi kwa pamoja kwenye sekta ya kufanya bidhaa za Petroli.

Mpango huu umewekwa kazi wakati wa kikao kati ya Waziri wa Nishati, Mh January Makamba na Balozi wa Oman Tanzania Saud Hilal Al Shidhani. Mipango mingine pia ni kufanya kazi kwa pamoja kati ya Oman OQ na TPDC katika ujenzi wa mitambo ya gesi asilia.

Haya yote yanajiri hivi sasa baada ya safari ya Rais Samia Suluhu Oman Juni 2022 ambapo mikataba ya awali ilisainiwa huko Oman kati ya Tanzania na Oman. Ambapo mikataba hiyo si katika nishati tu, bali hata utalii, elimu na uwekezaji.

Hivyo ambayo Rais wetu Samia Suluhu anafungua nchi yetu, analeta fursa za uwekezaji ambazo ni kichocheo kikubwa cha ajira, kukuza pato la taifa na kuongeza biashara ambayo inaingiza fedha nyingi za kigeni ambazo ni muhimu sana katika kuimarisha uchumi wetu.
 
Tuachane na petrol tutumie ethanol ni cheap na ipo kwa wingi TANZANIA malighafi zipo tele. Tutazalisha ajira tele nchini pili tutaokoa pesa za kigeni kununulia petrol na dizeli nje pesa hizo zitaenda kwenye maeneo mengine ya uchumi.

Engine zote za petrol kuanzia gari, pikipiki, toyo, Bajaj, waterpump, generator, chainsaw, nk zote zinatumia ethanol kwa 100% au uchanganye na petrol kwa ratio ya E85 yaani lita kumi ya ethanol mix na lita 1.5 ya petrol ni mapenzi yako tu.

Brazil wao wanatumia 80% ya ethanol ambayo wanazalisha wenyewe. Waarabu wakatafute Kazi zingine sio kutegemea mafuta tu ndo waishi.
 
Back
Top Bottom