Tanzania na serikali tatu - tupo tayari ?

Tanzania na serikali tatu - tupo tayari ?

MAGEUZI KWELI

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2011
Posts
1,947
Reaction score
253
TANZANIA NA RASIMU YA KATIBA MPYA 2013
Si mbaya kwa watanzania kuwa na maamuzi makubwa ndani ya katiba wanayotaka iitawale nchi kwa sasa.

Ni jambo jema na wengi tumeona Rasimu na kwa mtizamo mkubwa sasa tunaingia katika mfumo wa serikali tatu.

Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tunaona mfumo mpya unalisogelea Taifa maskini kabisa Duniani ambalo ni tajiri kwa Rasilimali ambazo zimeshindikana kuneemesha walio wengi na kuishia pasipogusika kwa namna moja au nyingine.
Kilio hiki kitadumu miongoni kwa wengi wasioiona faida ya rasilimali za Taifa.
SWALI LA KUJIULIZA KWA SASA:
Kwa umaskini huu ambao bado unalisumbua taifa maskini namna hii, kama Huduma za Afya Duni, Elimu isiyo na kiwango kabisa, Shule hazina madawati, Gharama za maisha ni kubwa sana, Shillingi kusidi kuporomoka thamani dhidi ya Dolla, Mishahara midogo, Vifo vya kuepukika, Mafisadi kulindana, Ajira za kujuana na wengi kuhangaika na elimu zao mitaani bila ya ajira NK..
Je ! > Tunaweza kuwekeza tena katika kuwa na serikali Tatu ambazo zitazidi kulikamua taifa hili kwa sababu ambazo bado hatujazitafakari faida zake na Hasara Zake?
Ø Kwa Tanzania hii hii na Zanzibar, Serikali Tatu msingi wake mkubwa ni kulisaidia nini taifa bila kuangalia uhusiano wa kihistoria ulioasisiwa na Waasisi wa Taifa?
Ø Uchumi uliopo sasa unaneemesha asilimia ngapi ya wananchi na baada ya mfumo wa serikali kupanguka wataneemeka kwa kiasi gani ili japo faida ya mabadiliko ionekane?
Ø Je Marais na Serikali zao wataligharimu taifa kiasi gani na ni vyanzo vipi vya mapato vinavyoweza lisaidia taifa hili ambalo bado linatia aibu kwa kukwapuliwa kwa Rasilimali zake bila ya woga wowote?
Ø NINI HASARA KWA SASA IWAPO SERIKALI ZITAAMUA KUACHANA NA MFUMO WA MUUNGANO NA KUJITEGEMEA KWA KUACHA MFUMO WA UJIRANI MWEMA KUSIMAMA KAMA TULIVYO NCHI ZA AFRIKA YA MASHARIKI AMBAZO MPAKA SASA TUNAJUANA NA KILA MMOJA ANAENDESHA MAMBO YAKE?
Ø Kwa mfumo huu hasara zake ni nini na faida zake kwa ujumla?

Ninalililia taifa langu maskini kutaka kuridhia Katiba (Muhimu sana)itakayoleta mtazamo mpya wa utawala kwa taifa maskini na kuanzishwa kkwa serikali zenye Gharama sana kuliko kinachohitajika kwa wananchi sasa.

SI MBAYA NIKIWA TOFAUTI SANA MTAZAMO WA WENGI, PESA NYINGI SANA ZITATUMIKA KULIENDESHA TAIFA NA SPEED YA MAENDELEO SIJUI ITAKUWA YA KASI GANI?

MUNGU IBARIKI NCHI YANGU TANZANIA KWA SASA BAADAE SIJUI ITAITWAJE MUNGU AJUA
 
Wewe mawazo yako yananfanana na mtumishi wa tatu katika kitabu cha biblia ambaye alipewa talanta tano kwa kuona ubahili na kujifanya anaona mbele zaidi kuliko wenzake wawili akazifukia ardhini zile talanta tano alizopewa na bwana wake ili zisipotee! Na wale wnzake wawili wakazifanyia biashara zikazaa kila mmoja talanta tano nyingine!

Nimekuelewa point yake inagusa uchumi zaidi: Bwana mageuzi hivi ingikuwa kama unavyowaza basi maskini wotewasingeoa! Maana maskini anakipato kidogo na tena mara nyingi huoa maskini wenzake na tena majukumu ya maskini huyu muongezeka mara nne (yeye binafsi, mke, watoto, na ndugu wa pande zote)!

Kwa hiyo kwa maskini huyu kama akiangalia hali ya uchumi wake tu basi kamwe hataoa! Hoja hapa kwa huyu maskini si kutoungana na mwenzi wake kwa sababu ya umaskini wake hoja hapa ni vp aongeze kipato ili aweze kuendesha maisha yake vizuri kwa kutumia fursa alizonazo au zianazomzunguka!

Muungano wa nchi si jambo baya kama ilivyo ndoa na cnhi nyingi sana dunianai zinatamani kuungana lakini zinashindwa! Ndio maana kwa kuona huo umuhimu ndio maana hata rwanda na burundi zimejiunga kwenye kwenye east africa community!

Suala la msingi kwanza ni kwa tanganyika na zanzibar kutumia rasilimali zake kikamilifu kwa ajili ya kuwaletea wananchi wake maendele badala ya kuwagawia wazungu na wachina halafu sisi tunabaki hoi na kulalamika kama wewe!
 
Wewe mawazo yako yananfanana na mtumishi wa tatu katika kitabu cha biblia ambaye alipewa talanta tano kwa kuona ubahili na kujifanya anaona mbele zaidi kuliko wenzake wawili akazifukia ardhini zile talanta tano alizopewa na bwana wake ili zisipotee! Na wale wnzake wawili wakazifanyia biashara zikazaa kila mmoja talanta tano nyingine!

Nimekuelewa point yake inagusa uchumi zaidi: Bwana mageuzi hivi ingikuwa kama unavyowaza basi maskini wotewasingeoa! Maana maskini anakipato kidogo na tena mara nyingi huoa maskini wenzake na tena majukumu ya maskini huyu muongezeka mara nne (yeye binafsi, mke, watoto, na ndugu wa pande zote)!

Kwa hiyo kwa maskini huyu kama akiangalia hali ya uchumi wake tu basi kamwe hataoa! Hoja hapa kwa huyu maskini si kutoungana na mwenzi wake kwa sababu ya umaskini wake hoja hapa ni vp aongeze kipato ili aweze kuendesha maisha yake vizuri kwa kutumia fursa alizonazo au zianazomzunguka!

Muungano wa nchi si jambo baya kama ilivyo ndoa na cnhi nyingi sana dunianai zinatamani kuungana lakini zinashindwa! Ndio maana kwa kuona huo umuhimu ndio maana hata rwanda na burundi zimejiunga kwenye kwenye east africa community!

Suala la msingi kwanza ni kwa tanganyika na zanzibar kutumia rasilimali zake kikamilifu kwa ajili ya kuwaletea wananchi wake maendele badala ya kuwagawia wazungu na wachina halafu sisi tunabaki hoi na kulalamika kama wewe!
Luriga, Thanks for your comment,
Ushasema maskini kuoa maskini mwenzake, Ina maana kuna tabaka la asili hata kwenye selection ya wenzi wentu kuwa huwezi funga nira na either msomi au asiye msomi, maskini na tajiri.
Cha msingi ni kuangalia faida na hasara, kwani ni lazima tuwe na mlolongo wa marais ambao hata marekani walioungana mataifa mengi kuwa na USA na rais wao mmoja. Iweje sisi tuwe na mlolongo wa kutafuna pesa za nchi kwa msimamo wa kulinda muungano?
Kwa nini zanzibar isiwe familia tu kama kwaida na serikali zikawa kila mmoja kivyake tukakutana tu kwenye jumuiya ya Africa mashariki?
Sorry for that...We are together
 
kimtizamo wangu serikali tatu sio njia muafaka .tunaongeza gharama za uendeshaji nchi usio wa lazima badala ya kuwa na watu wachache wachapakazi tunakuwa na watu ambao ni mizigo kwa walipa kodi .tuige mfumo wa kenya wa utawala na kuleta hii hoja kunaomnyesha tume kukosa weledi haija kaa kitaifa zaidi badala yake hii hoja imejikita kisiasa zaidi .turejee nukuu za mwalimu na akina tuntemeke sanga kuhusu serikali tatu ,kwenye kura hili tuseme noooo.
 
Back
Top Bottom