Tanzania na Uganda zapigwa marufuku na Ulaya kuendeleza Miradi ya Mafuta na Gesi

Tanzania na Uganda zapigwa marufuku na Ulaya kuendeleza Miradi ya Mafuta na Gesi

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Salaam Wakuu,

Bunge la Umoja wa Ulaya limeazimia Azimio linalozitaka Tanzania na Uganda kusitisha mara moja uendelezaji wa Miradi ya mafuta na Gesi katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

Wanadai miradi hiyo inaharibu mazingira.

Wakati Bunge la Tanzania likiwa kimya, Bunge la Uganda limelaani azimio hilo walilodai ni kiwango cha juu cha Ukoloni Mamboleo na ubeberu dhidi ya Uhuru wa Uganda na Tanzania.



Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Kabaale – Hoima Nchini Uganda kwenda kwenye peninsula ya Chongoleani Mkoani Tanga Nchini Tanzania, ni Mradi wenye urefu wa jumla ya kilomita 1443 kati ya hizo kilomita 296 zipo Uganda na kilomita 1147 zipo Tanzania.

Bomba linapita katika mikoa 8 ya Tanzania Bara ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga, vilevile linapita katika wilaya 24, kata 134 na vijiji zaidi ya 180.

Matokeo ya utafiti uliofanywa na kampuni za kimataifa za utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi za TOTAL, TULLOW na CNOOC ulibaini uwepo wa mafuta ghafi takribani mapipa bilioni 6.5. Kutokana na ugunduzi huo imebainika uwezekano wa kuvuna mapipa kati ya bilioni 1.2 hadi 1.7. Kutokana na mahusiano ya ushirikiano ya muda mrefu na faida za kupitisha bomba nchini Tanzania Serikali ya Uganda na wawekezaji wa mkondo wa juu waliamua kujenga mradi huu kupitia Tanzania kutoka Hoima Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Lengo la Mradi
Lengo la mradi huu ni kuwezesha mafuta yatakayozalishwa Uganda kusambazwa katika soko la ndani na sehemu inayobaki kuuzwa nje kwenye soko la kimataifa kupitia bomba la mafuta.

Gharama za kukamilisha ujenzi wa mradi wa bomba zinatarajia kufikia takribani Shilingi Trilioni 8 za Kitanzania. Bomba hili lilitarajiwa kujengwa na kuendeshwa na kampuni za TOTAL ya Ufaransa, CNOOC ya China na TULLOW ya Uingereza, kwa ubia na Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
 
Sikieni enyi nchi na wakaao ndani yake. Vita ya uchumi ni ngumu na kuishinda kwake ni kushupaza shingo bila kubwabwaja. Yaani wanaona tu mnalaza pipes bila kuwatajataja wala kuwabeza na kuwaita majina yasiyo faa n.k.
India china ethiopia n.k miradi yao mikubwa waliziba masikio na wakafanya.

Kwenye swala la nishati sijawahi kuwa rafiki na yeyote anaye kwamisha huo ndio mskmamo wangu
 
Sikieni enyi nchi na wakaao ndani yake. Vita ya uchumi ni ngumu na kuishinda kwake ni kushupaza shingo bila kubwabwaja. Yaani wanaona tu mnalaza pipes bila kuwatajataja wala kuwabeza na kuwaita majina yasiyo faa n.k.
India china ethiopia n.k miradi yao mikubwa waliziba masikio na wakafanya.

Kwenye swala la nishati sijawahi kuwa rafiki na yeyote anaye kwamisha huo ndio mskmamo wangu
Upo sahihi bila hivyo tutayumba
 
Bunge la Umoja wa Ulaya limeazimia Azimio linalozitaka Tanzania na Uganda kusitisha mara moja uendelezaji wa Miradi ya mafuta na Gesi katika Ukanda wa Afrika Mashariki.
Ukweli wa mambo ni huu: Tungekuwa (Waafrika, kiujumla), na akili kidogo za kujitambua, ingekuwa wakati mwafaka kabisa kuanza mchakato wa kuwaweka chini ya ukoloni wetu hawa watu waliotuweka kwenye ukoloni wao miaka iliyopita.

Ni wazi kabisa, hawa watu wanahitaji kutawaliwa kutokana na kutapatapa kwao kunakozidi kuonyesha utayari wao wa kuwa chini ya himaya yetu.

Huenda kizazi kitakachofuata baada yetu kinaweza kuwa na akili nzuri za kuwaweka chini hawa watu.

Ni wazi hawa watu sasa wanahitaji kutawaliwa ili akili ziwarudi kichwani.
 
Sikieni enyi nchi na wakaao ndani yake. Vita ya uchumi ni ngumu na kuishinda kwake ni kushupaza shingo bila kubwabwaja. Yaani wanaona tu mnalaza pipes bila kuwatajataja wala kuwabeza na kuwaita majina yasiyo faa n.k.
India china ethiopia n.k miradi yao mikubwa waliziba masikio na wakafanya.

Kwenye swala la nishati sijawahi kuwa rafiki na yeyote anaye kwamisha huo ndio mskmamo wangu
Mama anafungua nchi. Kwa Fitna za Kenya utasikia Mradi umepangwa kupitia Kenya ili kulinda mazingira. #mama anafungua nchi.
 
Sukuma gang wanazidi kukomeshwa.

1. Bomba la mafuta chali.

2. Mradi mkubwa wa umeme chali.

3. Gesi mtwara chali.

4. Reli ya umeme chali.

5. Corona chali.... tuna chanjo kutoka ulaya.

6. Ujenzi wa miundombinu chali.

7. Kila kitu chali. Tunamkomesha mwendazake na genge lake la burundi.

Mama anaupiga mwingi. SUKUMA GANG WATAOMBA POO.

Mletee mzunguuu..
Kama unamaanisha ulicho andika(japo sijawahi kuwa sapota wa magufuli kwa mengi isipokuwa kwa mradi wa umeme) basi tanzania tunayo safari ndefu sana
 
Upo sahihi bila hivyo tutayumba
Ninakubaliana na wazo hili.

Hakuna sababu muhimu ya kuendelea kuwapapatikia hawa watu.

Dunia inavyogeuka sasa, utegemezi kwao hautakuwa wa lazima sana, kama China, India, Urusi na mataifa mengine yataamua kuachana na mifumo inayotumiwa na hawa wahuni kuendelea kutawala dunia kiuchumi. Teknologia sasa imeenea, haihodhiwi tena na haya mataifa machache.
 
Sukuma gang wanazidi kukomeshwa na uongozi shupavu na madhubuti wa MAMA YETU:

1. Bomba la mafuta chali.

2. Mradi mkubwa wa umeme chali.

3. Gesi mtwara chali.

4. Reli ya umeme chali.

5. Corona chali.... tuna chanjo kutoka ulaya.

6. Ujenzi wa miundombinu chali.

7. Kila kitu chali. Tunamkomesha mwendazake na genge lake la burundi.

Mama anaupiga mwingi. SUKUMA GANG WATAOMBA POO.

Mletee mzunguuu..
Vp unafurahia mkuu?
 
Sikieni enyi nchi na wakaao ndani yake. Vita ya uchumi ni ngumu na kuishinda kwake ni kushupaza shingo bila kubwabwa
Bomba litapita karibu kabisa na mbuga ya Murchison ambayo wageni wake wengi ni kutoka Ulaya khasa "royal families" na wengine wenye mapesa.

Hivyo wanaharakati tayari wamevuta mpunga na wameanza na kushambulia kampuni za mafuta zitazoshirikiana kujenga hilo bomba pamoja na mabenki yatayotoa fedha kugharamia mradi.

Na AU walipoaswa kuiingilia kati moja kwa moja kwa kutoa kauli ya kupinga ukwamishwaji huo.

Uganda na Tanzania wao waendelee na ujenzi wa bomba ambalo lajengwa Afrika na sio Ulaya na ni kwa manufaa ya waafrika.
 
Bomba litapita karibu kabisa na mbuga ya Marchison ambayo wageni wake wengi ni kutoka Ulaya khasa "royal families" na wengine wenye mapesa.

Hivyo wanaharakati tayari wamevuta mpunga na wameanza na kushambulia kampuni za mafuta zitoshirikiana kujenga hilo bomba pamoja na mabenki zitazotoa fedha kugharamia mradi.

Na AU walipoaswa kuiingilia kati moja kwa moja kwa kutoa kauli ya kupinga ukwamishwaji huo.

Uganda na Tanzania wao waendelee na ujenzi wa bomba ambalo lajengwa Afrika na sio Ulaya na ni kwa manufaa ya waafrika.
Sikupingi kwa lolote. Utakuwa ni ujuha kutetemekea mataifa ambayo tayari wamesimika viwanda vizito huku wakiviendesha kwa nishati ambayo hawataki tuwe nayo.
 
Salaam Wakuu,

Bunge la Umoja wa Ulaya limeazimia Azimio linalozitaka Tanzania na Uganda kusitisha mara moja uendelezaji wa Miradi ya mafuta na Gesi katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

Wanadai miradi hiyo inaharibu mazingira.
Tuwekee source ya habari hii, la sivyo ni porojo tu
 
 
Back
Top Bottom