Tanzania nchi 'pole'

Tanzania nchi 'pole'

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Hivi, mbona hatujawahi kusikia tz imefanya uamuzi ambao umepigiwa kelele na mataifa ya nje? Kutopigiwa kelele haimaanishi kuwa sie ni waungwana sana. Pengine wanaomba tuendelee na ububu na upole wetu. Kelele toka nje zilikuwepo enzi za mwalimu. Ukisikia kelele sehem flani duniani ujue anaepiga kelele kashikwa pabaya. Tz ni kama mwanamke anaevutia sana lakini kwa bahati mbaya kazaliwa katika familia fukara. Kutokana na ufukara na kutojiamini na uzuri wake, wenye vihela wanamrubuni na kumzini kwa zam. Ni lini tz baada ya mwalim kafanya uamuzi ulioisisimua dunia? Hakuna anaekubaka ila unawakubalia tu. Hii hali ishaingia damuni. Ni lini tz itafanya maamuzi kwa maslah ya watz? Kwa nini viongozi wetu ni makuwadi? Hii ni silika, utamaduni, upuuzi, kutojiamini au nini? Upole wa tz unatisha. Hakuna maslah ya taifa kwanza. Mbona uchumi wa tz unashikiliwa na wanaojiita watz wakati kimtazamo na kitamaduni sio? Viongozi wanawaza nini? Inavyoonekana kuna ajenda ya siri ya kumfifisha mtu mweusi ikisaidiwa na 'wateule' weusi. Tz ni pole kiasi cha kutia kinyaa. Tz ni sawa na mume anaemkuwadia mkewe kwa midume. Dola ni nini na inafanya nini na iko kwa manufaa ya nani? Ni nani anamwogopa nani na kwa nini? Naomba siku ifike ije menejiment toka nje kushika hatam za uongozi. Labda hawatamwogopa wala kumchekea mtu. Hiyo siku ije upesi.
 
Hata wachangiaji humu ni wapole na wapita njia tu. Wanajua kumeza vilivyotafunwa na wenye meno na wanaojua kutafuta. Changamoto kwenu
 
Back
Top Bottom