Tanzania ndiyo nchi pekee mtu anatekwa mchana, anauawa na mpaka sasa hakuna aliyewajibika

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Hali hii si ya kawaida, Mamlaka zinatambua, watu wameshuhudia Marehemu Kibao alivyokamatwa na kutokomea na gari lenye plate namba ambazo hata kama hazijulikaniki, ni wajibu wa vyombo vya ulinzi na usalama kufanyia kazi haraka.

Lakini mpaka sasa hakuna aliyefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumteka na kuhusika katika kifo cha Bwn. Kibao, Mamlaka zimerelax na watu wameshasahau na maisha yanaendelea as if hakuna kilichotokea!

Yule Mzee ana mke, watoto waliokuwa wakimtegemea, ndugu jamaa na marafiki, ambao wameachiwa uchungu mkubwa katika mioyo yao!

Je, watekaji ni kina nani?
Je,wameshakamatwa? au nani ameshafikishwa katika vyombo vya dola kwa uchunguzi?
Je, kuna kesi imeshafika mahakamani?
Je, gari na silaha zilizotumika ni za kina nani?
Je, familia ya Mzee Kibao imefarijiwa na serikali? Wamehakikishiwa usalama wao?
 
Watekaji wana vikosi imara
 
Wanaangalia lipi litakuwa nafuu "gharama za kufanya uchunguzi" au "kulipa fidia"
 
Na hali hiyo imewafanya hata waahilifu,watu wanaodaiana,dhulumiana wana malizana kwa style hiyo hiyo

Ova
 
Nani afanye uchunguzi ilhali wanaopaswa kuchunguza ndio waliomteka na kumuua.
Halafu Rais Samia kasema uchunguzi umefika pazuri 😡
 
Wewe ndo uanze kuongoza njia ya ukomboz, REVENGE IS FOR STRONG PEOPLE. if you are weak you Will IGNORE.
 
Hii ni kudhihirisha kuwa ni dola ndiyo iliyomuua. Na hakutakuwa na ripoti yoyote ndiyo imetoka hiyo na akina Soka nao wameshauwawa na muuaji huyo huyo.
 
Alafu leo wanakuambia kuna siku ya kupinga hukumu ya kunyongwa
Wakati uraiani watu wanatekwa wanachukuliwa uhai live
Pascal Mayalla

Ova
 
 
Mbaya zaidi chama kilichoshikilia dola.. kwa kuona wanafanya la maana eti wameendankuaandaa dua ya kumuonbea? Mimi ni ningekuwa familia nisingeshiriki..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…