Tanzania Premier League (TPL).... Simba SC dhidi ya Azam FC, moja kwa moja kutokea uwanja wa Uhuru, Dar es salaam

Tanzania Premier League (TPL).... Simba SC dhidi ya Azam FC, moja kwa moja kutokea uwanja wa Uhuru, Dar es salaam

Snipes

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2013
Posts
9,165
Reaction score
16,791
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara klabu ya Simba ambao ni vinara kwa pointi 81 ikifatiwa na Yanga yenye pointi 80 na Azam nafasi ya tatu pointi 68, itashuka dimbani kumenyana na Azam FC ktk mechi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa leo 13/05/2019 saa 10:00 jioni, baada ya ule mchezo wa kwanza tulishuhudia timu ya Simba ikichomoza na ushindi wa 3-1.
Simba ndio bingwa mtetezi wa Ligi Kuu Bara. Endapo wataibuka na ubingwa msimu huu, utakuwa wa 20 kwao na kushika nafasi ya pili nyuma ya Yanga ambao wamechukua mara 27.
SIMBA SC; Aishi Manula, Nicolas Gyan, Mo Hussein, Yusuph Mlipili, Erasto Nyoni, James Kotei, Jonas Mkude, Haruna Niyonzima, Emmanuel Okwi, Meddie Kagere, Clatous Chama.
SUBS; Deogratias Munish, Zana Coulibaly, Said Ndemla, Hassan Dilunga, John Bocco, Rashid Juma, Mzamiru Yassin.
AZAM: Abalora, Wadada, Bruce, Yakubu, Moris, Kingue, Domayo, Ngoma, Mahundi, Singano, Chirwa
SUBS; Mwadini, Mwasapili, Amouah, Hoza, Atta, Kutinyu, Lyanga

FULLTIME: Simba Sc 0-0 Azam Fc
 
Vipi mkuu hali ya hewa uwanja inaruhusu mpira kuchezwa?
hali ya hewa si nzuri sana eneo la uwanja ila halina tofauti sana ukilinganisha na mechi ya Kagera hivyo sioni dalili ya mechi kutochezwa leo.
 
Sawa japo mie nashangilia mnyama ila naona leo pia ana nafasi kubwa ya kupoteza
 
Vikosi vipi vilishatoka?
Kikosi cha Simba SC..Kulitaka Mwana, Kulipewa Mwana, NguvuMoja
IMG_20190513_150637_329.jpeg
 
wakati wowote kuanzia sasa mpira utaanza
 
Sisi mashabiki wa Yanga Leo tunaishangilia Simba ili tujidhatiti ktk nafasi ya pili,Azam asije akatupokonya akishinda,au mnasemaje mashabiki wenzangu wa Yanga??
Ivo ivo baba,daima mbele nyuma mwiko....uzalendo hauwezi kutushinda kote kote nje na ndani....!!!!.ila mi mnyama unyamani
 
01' mpira umeanza kutokea uwanja wa Uhuru Dar es salaam
 
3' Chama anamchezea rafu Ramadhan Singano refa anaamuru mpira upigwe kwenda lango la Simba
 
9' Azam wanapata kona ya pili inaenda kupigwa na Singano ambayo imeokolewa na kipa Aishi Manula

10' Simba 0-0 Azam
 
14' Simba wanapata kona ya kwanza mpigaji ni Chama..... Simba wameanza kona fupi Gyan anapiga krosi ndefu anatoa nje na inakuwa goal kick
 
16' kadi ya njano kwa Chirwa baada ya kumsukuma Erasto Nyoni, free kick kwenda lango la Azam
 
18' Simba wanapata kona ya tatu, wameanza kona fupi Niyonzima anapiga krosi kati, wanaokota mabeki wa Azam
 
21' Joseph Mahundi anapewa kadi ya njano baada ya kumsukuma Clatous Chama
 
Back
Top Bottom