Tanzania(Taifa Stars) yanyolewa bila wembe na Algeria goli 4 kwa 1

tulivofungwa na brazil hapa taifa bado huwalaumu kina nyoso? tuna safari ndefu ya soka letu la figisufigisu hili la kina manara
 
ndugu mtoa mada ni kweli kabisa wewe ulitegemea kuwa tungeshinda ile mechi??????? c'mon tuacheni masikhara kuna mambo wala si ya kuumiza kichwa taifa stars kufungwa na algeria si habari hata kidogo. habari ingekuwa kama taifa stars imeifunga algeria. ni kama mbwa kumuuma mtu si issue ya kuumiza kichwa. issue inakuwa mtu kumuuma mbwa. hii ndo ingeweza kuleta gumzo.
 
Kipigo cha goli 4 kwa Timu yetu ya Taifa dhidi ya Algeria Tatizo la msingi ni nin hasa...? Lakini nini kifanyike tutoke hapa tulipofikia
Jamii nzima ya Tanzania ni kama Taifa stars tu. Tuna potential sana lakini tunawekeza muda na akili zetu kwenye vitu petty petty.
 
siasa nyingi,wenzetu soka lao linajiendesha lenyewe sisi kila kitu ni siasa tu,angalia wenzetu wa Zambia,msumbiji,Zimbabwe n.k,wana wachezaji wengi tu wanaocheza mpira wa kulipwa nje,timu zao za vijana zipo na zinaendeshwa kitaalamu.
 
hamna shortcut kwenye maendeleo ya michezo! waboreshe miundo mbinu, soka lichezwe kwenye grassroots! ratio ya mwanafunzi kwa eneo liboreshwe! watoto wapate maeneo ya kuchezea! mitaala ya michezo mashuleni irudishwe/iboreshwe,
kingine kikubwa ligi za ndani ziboreshwe bila kusahau academy za ku scout na kuandaa wanamichezo!
 
misri this week wameongeza mtaalamu wa nutrition kwenye benchi la ufundi la timu ya taifa
 
Tunawekeza kwenye Viwanda, diwani, ubunge
 
Mwalimu mbovu hana mbinu wachezaji nao wabovu harafu benchi kaufundi lina majungu unaanzaje kumuacha mkude taifa stsrs
 
Tatizo tunaforce fan tusiyoiweza
 
Tatizo ni TFF maana ndiyo wenye jukumu la kusimamia mpira nchini. mbaya zaidi FIFA hawataki serikali iingilie mpira vinginevyo jiwe angeshawatumbua na angekuwa kafanya kazi nzuri sana. TFF wanawaza matumbo ma si mpira wetu.
Bora enzi za jk timu ilikuwa inajikongoja
 
Hivi mlitegemea Stars wangeshinda kweli?

Hebu kuweni serious basi.
 
Lile goli la nne tulilifungwa ni fedhea sana. Chenga mtu 3 iliniuma sana asee
 
[3/22, 22:30] masolele: *mm naomba basata waifungie taifa starz*
[3/22, 22:30] masolele: *yaan kama timu ya taifa ingekua inashuka daraja taifa stars ingekua kuzimu*
 
Kila siku namwambia hapa Wakudadavuwa fanya kazi yako vyema tupate maendeleo! Yeye ni malumbano ya nguo fupi na nyimbo
 
Hivi yule waziri wa michezo ambae ni shabiki wa mikia alisema kuwa kwa kuwa mikia imeimarika basi na taifa sitazi itaacha kuwa head of crazy [emoji1][emoji1][emoji1][emoji38]
 
Algeria wanajua mpira Tanzania kichwa cha mwendawazimu kila mtu anajifunzia kunyoa
 
Kwa mechi ya Jana tatizo ni kukosa wachezaji wakubwa wa sehem ya kiungo. Mpira wa unahitaj kutawala sehem ya kiungo otherwise lazma muisome namba.
 
Kila siku mnajifunza

Kwani kuna ' ukomo ' wa Kujifunza? Sikujua kama uko ' hopeless ' hivi. Halafu kaa ukijua kwamba Kufungwa kwa Timu kuna mjumuisho wa vitu vingi ila wengi wenu ambao mmekuja kufuatilia mpira wakati wa ujio wa Kocha ' Morinyo ' ndiyo Timu ikifungwa tu mnakimbilia kulaumu Wachezaji au Benchi la Ufundi. Hivi utakuwaje na Timu bora ya Taifa wakati benchi lake tu la Ufundi halina Watu stahili? Wachezaji hawana mwamko? Uteuzi wa Wachezaji unategemea Simba, Yanga, Azam na kidogo Mtibwa? TFF muda mwingi imewekeza katika ' malumbano ' badala ya maendeleo? Serikali inajitokeza tu pale Timu ikifanya vyema lakini ikiwa katika maandalizi wanaisahau?

Nadhani Elimu hii ndogo tu na ya awali itakufungua kidogo ' Ubongo ' wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…