Tanzania: Tembea uone

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,015
Reaction score
2,680


Basi si kama hapa barabara inajengwa, magari yamepita mengine mbele yameziba njia, ili mradi siku hazigandi
 
Yaah! na haya yapo sehemu kubwa sana ya Tanzania. Inatisha, na usiombe kuwa mahali kama hapo.
 
Nchii hii ni tajiri sana kwa kila kitu lkn hakuna anayejali si sisi raia tunaoshabikia na kupiga umbea kila kukicha kuhusu mafisadi bila kuchukua hatua zozote, wala hawa viongozi wetu wanaojali matumbo yao na jamii zao.

Mao mwenyekiti wa uchina alilazimisha watu wafanye kazi akaonekana dikteta lkn miaka kadhaa sasa china iko level moja na marekani, sisi hata kujenga mitaro tunalilia wafadhili, tunahitaji dikteta aina ya watu km mao ze dong.

Kuna watu km wajapani wanafanya kazi kwa masaa 15 kwa siku, sisi masaa sijui nane na nusu tena kwa mbinde kuyatimiza, utakuta mtu analalamika kweli kweli.

Tunasherekea miaka sijui 48 ya uhuru hata barabara tu zimetushinda, kweli tutabaki wadanganyika
 
Eee bwana ee asante sana, mbona hapo kama home kwetu vile?
 
Mie pia nimepafananisha kama kwetu vile ..mnakwama na gari na kukaa siku nzima wakati huo una sensitive issue ya kuattend
 
Huo udongo kama wa Kigoma vile, kule Kasulu na Kibondo!
 
Hii itakuwa ni yale Majimbo wanayotoka wabunge "wapambanaji" -
 
Mwaka ujao Tunasherehekea miaka50 ya UHURU! Tunachojivunia ni kuona msafara wa rais ni sawa na wa Bush na wa First laddy kama wa Laura bush! maendeleo makubwa hayo!
barabara, hospitali , shule wala sio vya msingi kwetu!
Nakumbuka miaka ya 60 nikiwa bado mdogo barabara zilikuwa ni za udongo kutoka mkoani kwenda kijijini kwababu yangu na mabasi yalikuwa yale ya Leyland Albion lakini yaliweza kwenda na kurudi siku hiyohiyo kwa kuwa kila baada ya umbali fulani kulikuwa na kambi za kuhudumia barabara na vifaa pia vilikuapo na vilitumika ipasavyo!
Lakini baada ya CHAMA kushika hatamu( sijui farasi alikuwa nani) kila kitu kiliuwawa!
Maana kila kwenye shirika au taasisi ya serikali kuliwekwa eti makamisaa wa CHAMA!
Angalia shirika la reli lilivyouwawa! ilikuwa mtu unaweza kusafiri kutoka Songea hadi Bukoba kwa kutumia tiketi ileile na bila usumbufu pamioja na kwamba simu zilikuwa ni za kukoroga! huduma za bus, train , meli zilkuwa bomba1 Chakula ndani ya train na usafi wa vyumba usipime!
Leo tunajigamba eti tumepiga hatua kumbwa! kwa lipi hasa? au hayo marasa ya sekondari yaliyojengwa kwa kulipua, yasiyokuwa na vifaa wala walimu?
tumejaliwa kuwa na maliasili za kumwaga lakini angalia ni nini tumefaidika? migodi jamaa wanazidi kutuachia mashimo na Mrahaba wa 4% ambao karibu theluthi nzima kala Alex Stewart!
Rada na ndege ya serikali zimegharimu mabilioni ya Watanzania halafu akina Mramba bado wanapeta! Kesi za kiini macho ndio wanatuzuga nazo! China watu waliwalisha maziwa yenye sumu na Shughuli iliishamalizika!(FIRING SQUARD) Hapa sie tupotupo tu mara imeahirishwa mara ee ali muradi tu UTULIVU NA AMANI!
Rwanda wakuwa kwenye vita miaka mingi na hivi majuzi wafanya kutulia baada ya kumpata Mwanaume wa Shoka(sio kama yule wa Sofia Simba) angalia jinsi wanavyotuacha na kale ka wimbo ketu UTULIVU NA AMANI
Utulivu huu ni sawa na Ng'ombe anayekamuliwa inafika mahali umekamua na hana kitu cha kutoa na ukaendelea kukamua atakutandika mateke!
Natabiri si mbali sana Ng'ombe watawatandika mafisadi mateke!
 


Hapa itakuwa ni Masaki eh?
 


Hapa itakuwa ni Masaki eh?​
kazi kwelikweli.... sasa hii nguzo ya umeme ktk ya barabara ina maana wahusika waliojenga barabara ndio waliikuta nguzo imeshawekwa au muweka nguzo alikuta barabara imeshajengwa, mbona nashindwa kuelewa hapa imekaaje...... kweli kazi tunayo na hao ndio wataalamu wetu wanaomaliza vyuo sehemu mbalimbali na wana madegree kibao, halafu ikipita muda unasikia wanasema bomoa haijajengwa kama mpango mji unavyotakiwa,...,, mlikuwa wapi???!!!??
 
Haya matatizo ni kutokana na uzembe wetu wa kutokusoma na kutokutumia tafiti za wataalamu wetu. Mimi ninafanya Ph.D in Geotechnical Engineering na nimesoma sana mambo ya soil stabilzation na application zake!

Tunachokaa ya kutosha kuanzia Tanga hadi Lindi. Chokaa inaweza kumaliza matatizo yote hayo .... soma National lime association www.lime.org ya wamarekani utaona kuwa mambo haya yalifanyiwa utafiti tangu mwaka 1890 na yako documented!!!
Just we need application...... wizara ya miundombinu imeandika vizuri sana kwenye manual yao ya matengenezo ya mwaka 1999..... tatizo ni nini?
 










Tushazoea hali hii, na "KULA" tutaendelea kuwapa tu 🙁
 


Hii hapa ni jirani kabisa na CBE (Akiba) jijini Dar es Salaam kwenye kituo cha daladala
 
Kweli tembea uone, waweza kuta nguzo hiyo ina muda mrefu tu hapo mpaka itokee kugongwa ndo ihamishwe, cjui ni dili, haya yapo sana katika TZ yetu utakuta barabara ina shimo dogo linaachwa liwe kubwa ndo lije lizibwe tena kwa garama kubwa
 


Pssssssssssssssiiiiiiii! usiseme....!!!!
 


Kina 'flani' huu ndo usafiri wao kila siku
 
believe me if you live out of the country you will miss all that...

I missed the smell of this land ... I miss people... I miss vumbi... I miss everything... thank u for sharing...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…