TANZANIA TOP 100: 70%+ ya makampuni yaliyoshiriki hizi tuzo yanamilikiwa na wageni

TANZANIA TOP 100: 70%+ ya makampuni yaliyoshiriki hizi tuzo yanamilikiwa na wageni

Cybergates

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2016
Posts
697
Reaction score
1,474
Naangalia hapa hizi tuzo za tanzania top 100 campanies mpaka sasa wengi wa wamiliki wa hizi kampuni naona ni masingasinga,
naona hizi tuzo watanzania tumetupwa nje
inabidi tujipange miaka ijayo kushindana na hawa watu
 
Kwani usingasinga unamuondolea mtu sifa ya kuwa mtanzania? Tuache ubaguzi, dunia ni kijiji kwa sasa, tualike watu zaidi kuwekeza bila kujali rangi ya mtu na nchi atokayo. Asilimia kubwa ya watanzania kipato cha kufungua biashara kubwa hatuna...

Asante kwa kuhamasisha nasi kujaribu fursa
 
Kwani usingasinga unamuondolea mtu sifa ya kuwa mtanzania? Tuache ubaguzi, dunia ni kijiji kwa sasa, tualike watu zaidi kuwekeza bila kujali rangi ya mtu na nchi atokayo. Asilimia kubwa ya watanzania kipato cha kufungua biashara kubwa hatuna...

Asante kwa kuhamasisha nasi kujaribu fursa
Unajua tofauti ya investor na citizen mkuu??
 
Hao waandaaji wako weak Sana kwenye tathimini ya makampuni.kuna kampuni baadhi za mifukoni za kuunga unga Dili mjini, hazina ofisi, porojo tu. Eti NAZO zimeshinda with sifa kemkem..
 
Kwani usingasinga unamuondolea mtu sifa ya kuwa mtanzania? Tuache ubaguzi, dunia ni kijiji kwa sasa, tualike watu zaidi kuwekeza bila kujali rangi ya mtu na nchi atokayo. Asilimia kubwa ya watanzania kipato cha kufungua biashara kubwa hatuna...

Asante kwa kuhamasisha nasi kujaribu fursa
Kweli wewe hujawaza kitu uzima kabisa.Umemwelewa mtoa mada kweli au?Nadhani hayupo ki-ubaguzi zaidi ila anachomaanisha ni kuwa,inakuaje wandendereko ngozi nyeusi kama sie wazawa hawakuchomoza katika top tena(nadhani alimaanisha hivyo).Tatizo NINI hawa wahindi kuwa na ukwasi?Sisi wazawa hatuna mbinu za ujasiriamali?Walikuja na ukwasi huo hapa nchini au mifumo ya kifisadi ndio imewabeba?

Ndio maana Rais Magufuli huwa anasema hii nchi ni ya Watanzania,ni lazima tunufaike na rasilimali zilizopo badala ya kuwanufaisha wasio wazawa halisi(wakuja).Watu huwa hamuelewi mantiki yake.Kiufupi Matengo na Wakurya ni lazima nao wawe matajiri badala ya Wahindi tu.

Hivi hawa wanaokuwa na makazi ya kudumu Ulaya,Amerika,Asia na kwingineko kwa ajili ya permanent life lakini wanachuma rasilimali toka Tanzania/Africa utasema kweli mleta mada ni mbaguzi eti dunia sasa ni kijiji?

Hivi UNAWEZA wewe au Mtanzania yeyote kwenda India ukapata fursa za kuukwaa utajiri kweli?Haiwezekani aslani.Hivyo basi vyema uwe unajibu hoja na majibu yanayotamalaki nje ya box badala ndani ya box.

Sitetei ubaguzi lakini najaribu kufikiri kwa mapana zaidi nia hawa ya mleta mada.
 
Wabongo wengi wenye kampuni hawana mpango wa kuzifanya ziwe kubwa hatua kwa hatua hata baada ya wao kufa, unaweza kuta mtu anakufa na kampuni yake inakufa mda huo huo ila kwa hao wahindi hali ni tofauti kabisa.

Kwa mfano kampuni ya NEELKANTH SALT LIMITED ambayo kwa sasa inakuja juu sana kwa kutangaza bidhaa yao ya NEEL SALT. Kampuni hii inamilikiwa na mhindi na inakua kwa kasi hata kwa kuangalia kwa macho au kusikia kwa masikio utalibaini hilo.

Ni bora ukawa sole proprietor mwenye maono kuliko kuwa na kampuni ya mfukoni.
 
Back
Top Bottom