Sking zone
Member
- Jun 20, 2024
- 12
- 7
NATAKA TANZANIA IWE YA MAFANO DUNIANI (USHAIRI)
---------------------------------------------------
maono yalo moyoni, kichwani mwangu akili
asilimia Imani, naona hiyo fahali
Miji paka jijini, niona nzur Hali
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
hii ndoto yangu pevu, kuona ikichipua
na tuli kwa utulivu, ndo ndpo tutafikia
mbeleni upo wokovu, endapo tutawania
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
vinara nao wajenzi, ngazini nao wakwezi
utunzi wenye simanzi, baridi yake ni mwezi
Bando tuweke mabanzi, imara bati wekezi
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
na sio pande za shilingi, maono kubashilia
maono haya misingi, kwa njozi kuifikia
siasa njema sipingi, katiba kuifungua
naona nchi ijayo mfano, kwenye dunia
elimu Bora kwa kina, vitendo ndio dhahabu
sayansi ikaze Sana, nchi tupate tabibu
Sanaa nayo kwa Sana, Sheria iwe irabu
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
amani yenye utija, kuvuta watu kwa Nia
ni wapi panapo vija, nizibe bila Julia
wekeza nchi kwa tija, jifunze wako fikia
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
panua zote fasihi, ondoa rushwa nchini
maono yangu naaihi, fisadi weka kwa chini
uchama sio sahihi, utija nchi mbeleni
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
dondosha walo makupe, inua na wazalendo
hapo pongezi nikupe, Tanzania ya upendo
uchumi na unenepe, kusanya Kodi kwa pendo
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
miundo mbinu imara, mijini na vijijini
uzalendo ndo kafara, kuweka nchi hewani
nasio wake vipara, shauri yetu Imani
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
umeme kote nchini, hususa Ni vijijini
na maji kwetu thamani, uhai wa mishipani
ondoa Mila fitini, itatutoa relini
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
maono yangu upendo, umoja mshikamano
furaha iunge pendo, mbeleni nchi Ni nono
usawa ukaze mwendo, tufike haya maono
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
************************************"" "" "" "" ""
---------------------------------------------------
maono yalo moyoni, kichwani mwangu akili
asilimia Imani, naona hiyo fahali
Miji paka jijini, niona nzur Hali
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
hii ndoto yangu pevu, kuona ikichipua
na tuli kwa utulivu, ndo ndpo tutafikia
mbeleni upo wokovu, endapo tutawania
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
vinara nao wajenzi, ngazini nao wakwezi
utunzi wenye simanzi, baridi yake ni mwezi
Bando tuweke mabanzi, imara bati wekezi
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
na sio pande za shilingi, maono kubashilia
maono haya misingi, kwa njozi kuifikia
siasa njema sipingi, katiba kuifungua
naona nchi ijayo mfano, kwenye dunia
elimu Bora kwa kina, vitendo ndio dhahabu
sayansi ikaze Sana, nchi tupate tabibu
Sanaa nayo kwa Sana, Sheria iwe irabu
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
amani yenye utija, kuvuta watu kwa Nia
ni wapi panapo vija, nizibe bila Julia
wekeza nchi kwa tija, jifunze wako fikia
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
panua zote fasihi, ondoa rushwa nchini
maono yangu naaihi, fisadi weka kwa chini
uchama sio sahihi, utija nchi mbeleni
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
dondosha walo makupe, inua na wazalendo
hapo pongezi nikupe, Tanzania ya upendo
uchumi na unenepe, kusanya Kodi kwa pendo
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
miundo mbinu imara, mijini na vijijini
uzalendo ndo kafara, kuweka nchi hewani
nasio wake vipara, shauri yetu Imani
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
umeme kote nchini, hususa Ni vijijini
na maji kwetu thamani, uhai wa mishipani
ondoa Mila fitini, itatutoa relini
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
maono yangu upendo, umoja mshikamano
furaha iunge pendo, mbeleni nchi Ni nono
usawa ukaze mwendo, tufike haya maono
naona nchi ijayo, mfano kwenye dunia
************************************"" "" "" "" ""
Upvote
2