Sir robby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,396
- 4,080
Watanzania sio kama tunapinga nchi yetu kukopa, kinachowafanya wananchi waonekane kuogopa nchi kukopa ni uwezo mdogo wa watendaji wetu wa kusimamia miradi mikubwa na pia ufisadi mkubwa wa fedha unaofanywa na watendaji "Report ya CAG" imebainisha na pia hakuna hatua zozote zinazochukuliwa na mamlaka husika zaidi ya kulindana.
Ndio maana wananchi wanataka Katiba mpya ili Sheria nyingi ziboreshwe ili kudhibiti ubadhilifu wa fedha za umma na miradi.
Nchi nyingi zilizoamua kukopa zimeboresha kwanza sheria zake ili yeyote atakaye fuja mali ya umma achukuliwe hatua kali.
Mfano ni nchi ya China, na ndio maana wamefanikiwa kiuchumi.
Ndio maana wananchi wanataka Katiba mpya ili Sheria nyingi ziboreshwe ili kudhibiti ubadhilifu wa fedha za umma na miradi.
Nchi nyingi zilizoamua kukopa zimeboresha kwanza sheria zake ili yeyote atakaye fuja mali ya umma achukuliwe hatua kali.
Mfano ni nchi ya China, na ndio maana wamefanikiwa kiuchumi.