Tanzania tunayo malighafi ya kutosha kuendesha viwanda vyetu?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Wakati tunajipanga kuelekea uchumi Wa viwanda je hali yetu ikoje kwenye uwekezaji Wa kupata malighali ya kutosha viwanda tutakavyojenga?

Nijuavyo mimi malighafi iliyoko sasa ni ile ya mtindo wa kuokoteza kutoka kwa raia binafsi wasiokuwa na ujuzi wala mitaji ya kuzalishia.

Kipi kianze kwanza kati ya uwekezaji katika uzalishaji Wa malighafi na uwekezaji kwenye viwanda?
 
Hatuna, na ndio sababu viwanda vinakufa automatically.

Leo TBL wanaagiza malighagi ya bia (malt) kutoka nje, kiwanda chao cha moshi washakifunga.

Gharama za uzalishaji hasa shamban kwa Tz ni kubwa sana, kutokana na inputs bei juu sana.
 
Naona hili jambo liko wazi kwa namna hii;huwezi kujenga viwanda na usijue nini unaenda kuzalisha au upatikanaji wake wa malighafi ni 0 au mdogo saana,.pengine unajua kiwanda kitakuwa cha kuzalisha nguo kwa mfano, je, upatikani wa malighafi za kutengeneza hizo nguo upo?mashamba yapo lakini hayazalishi au ya kizalisha hayakidhi mahitaji sasa bora kipi "kuwekeza kwenye kuzalisha malighafi" kwanza au "kuwekeza kwenye uzalishaji viwanda"?

Hata historia ya " industrial revolution " ukiisoma vzr utajua kilianza kipi kikafuata kipi.
 
Chuma tunayo ya kutosha. Na chuma ndiyo mama wa mapinduzi ya viwanda. Ngozi tunazo za kutosha kuendesha viwanda vya viatu na bidhaa za ngozi. Kahawa ipo nyngi tu. Madini ya phosphate kwaajili ya viwanda vya mbolea yapo. Samaki kwaajili ya viwanda vya samaki wapo wa kumwaga. Malighafi zipo za kutosha.
 
Hatuna, na ndio sababu viwanda vinakufa automatically.

Leo TBL wanaagiza malighagi ya bia (malt) kutoka nje, kiwanda chao cha moshi washakifunga.

Gharama za uzalishaji hasa shamban kwa Tz ni kubwa sana, kutokana na inputs bei juu sana.
Lazima kuwe na plantations za watu wanaozalisha kibiashara sio peasants wanaolima kwa hiari bila utaalam wala mitaji, pembejeo na ruzuku. Mh. Kaijage sio kwamba halijui hili ila kuna sheeda
 
Uko serious? Ngozi zetu ni rejects
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…