by the way si mnajua jinsi wa Tz hatuna forums za walaji kulalamikia mifumuko ya bei,hii siyo ktk simu tu,hata ewura ktk gas ya kupikia,luku tanesco na petroli ,na VAT ni miongoni mwa vyanzo vichache vya mapato ya TRA.kimsingi hakukutakiwa kuwa na VAT ktk kununua vocha na kuitumia vocha kwani sioni value addition ktk hilo,unanunua vocha ili upige simu kwa kutumia mtandao wa mwenye vocha,sasa hiyo value addtion Tax inatokea wapi.
Mtoa mada umeongea la msingi sana ktk hili.Now how do we tackle this VAT ili ipungue ktk cost za kutumia simu.
tumezoea kulialia vijiweni huku tunaumia
okay....what you said is plausible lakini...value inayokuwa added kutoka mtu unaponunua airtime dukani hadi kutumia ni kiasi gani?
Je, unaponunua soda dukani hadi pale unapokunywa nyumbani, napo kunakuwa na value added?
Kwa nini hizi bidhaa mbili zinakuwa treated tofauti?
Sasa hayo makato yanayokatwa wakati wa kuongea si ndio matumizi yenyewe hayo. Sidhani kama tunaweza kuyaita VAT.
Kwa case yako unataka tusikatwe means tuongee bure au mimi ndio sijaelewa hapo.
Pia nasikia ukinunua vocha kuanzia ya elf 2 tayari ishakatwa vat ila za kurudi chini ndio vat inakatwa unapotumia.
zinakuwa treated tofauti kwa sababu na zenyewe ni tofauti.
nadhani hiyo ya pili tunawalipia shivacom na alfatel gharama za uendeshajiKwa hiyo,una maana hiyo ya pili ni kwa ajili ya kulipia madeni ya kanga/vitenge/kofia nk za uchaguzi na madeni ya Dowans sio !!!!!!!