Tanzania ya Vipaji

Tanzania ya Vipaji

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Wiki iliyopita siku ya mapumziko nilikwenda kwenye Kiwanja kimoja kutazama Vijana wakicheza Mpira wa miguu kwenye mashindano ya kugombania Kombe la Mbuzi!

Nikagundua kuwa Tanzania tuna vipaji vikubwa sana vya Mpira wa miguu ambavyo vimekosa muongozo wa kucheza mpira wa kitaalam tangu utotoni (Professional football) kutokana na kukosa walimu!

Wakati naondoka akanikimbilia Kijana mmoja akiwa na wenzake

Akaniambia
kaka samahani ninacheza sana mpira lakini nakosa nafasi kwasababu ya hali yetu ni masikini!

Nilishindwa kumuelewa,
Nikamwambia Kipaji hakijifichi, ukifanya vizuri lazima utaonwa, Jifunze zaidi na ongeza juhudi utafanikiwa!

Akaniambia,
Anacheza vizuri mpira wa miguu na aliwahi kujaribiwa katika moja ya klabu kubwa nchini Tanzania na alifuzu majaribio kwa kiwango kikubwa sana lakini alikwamishwa,

Nikamuuliza ilikuwaje,

Akaniambia alipigiwa simu usiku na msimamizi wa yale majaribio ya timu ya Vijana akajulishwa kuwa amefuzu majaribio lakini katika nafasi anayochezea wapo wawili hivyo mmoja atachukuliwa na mmoja ataachwa,
Akaambiwa atoe rushwa ya shilingi laki mbili ili asajiliwe!

Kijana ni mdogo na familia yake ni duni, akajaribu kuongea na wazazi wake lakini nao hawakuweza kuwa na kiasi hicho cha pesa ili watoe rushwa mtoto wao mwenye kipaji asajiliwe!

Ilipofika asubuhi yule mwenzake alifanikiwa kutoa rushwa akasajiliwa na kupewa vifaa na yeye akaachwa!

Hivi ndivyo hali ya rushwa ilivyo kubwa katika Taifa letu!

Hata wenye vipaji wanazuiwa kuonesha karama zao walizojaliwa na Mwenyezi MUNGU!

Kuna wachezaji wanasajiliwa toka nje ambao nikiangalia viwango vyao haviwafikii kabisa wachezaji tulionao hapa Tanzania lakini Watanzania hawa wamezibwa kuonekana na kufanikiwa na ukuta mkubwa sana wa rushwa!

Tuna wachezaji wazuri wengi kuliko akina Sarpong, Mugalu Calinho, Wawa na wengineo lakini rushwa inawakosesha nafasi

Nina hakika ukifuatiliwa usajili wa wachezaji wengi wa nje kuna rushwa kubwa sana,

Wanachukuliwa wachezaji wa nje wasio na viwango kwa madau makubwa ambayo wachezaji hawaambulii fedha hizo, fedha zinaliwa na kamati za usajili!

Tunatoa Pesa nje bila sababu za msingi!

Hata kwenye sanaa nako hali ipo hivyo hivyo!

Nyimbo nzuri nyingi hazipigwi kwasababu walioimba hawajatoa rushwa,

Kwa wasanii wa kike hulazimishwa mpaka kutoa rushwa ya ngono ili nyimbo zao ziweze kupigwa ama waweze kucheza kwenye filamu!

Ni muhimu sasa kwa Serikali kupitia wizara ya Habari, Sanaa na Michezo kushirikiana na Takukuru ili kuchukua hatua za kupambana na rushwa katika sanaa na michezo na kuweka sheria ya Fair competition ili kuzuia watu wabaya wachache wanaotaka kuhodhi sanaa na michezo na kuifanya Tanzania isiendelee!
 
Nafikiri kadri team zinazoshiriki league zinavyozidi kuongezeka labda hili tatizo litapunga.
 
Atoke aende mikoani au nje ya mipaka ya Tanzania hapa Dar kutoboa kisoka ufanye kazi ya ziada rushwa,ulozi,umimi na ualwatan.lakini pia chipukizi waliowengi wanataka Simba,Yanga akikosa hizo zote basi angalau Azam.
 
Uliposema wawa kiwango chake ni cha kawaida nikaishia hapo
Usingeishia hapo Tu mkuu, amesema wako wengi ungemuuliza akutajie wachezaji wawili Tu wa kitanzania wanaomzidi uwezo Wawa
 
Tupaze sauti walau tuwe kwenye MIFUMO ya Mpira ambayo ipo Rasmi.

Tuanze kwenye shule zetu za Msingi na Sekondari. Halafu tuje kwenye Level za Vyuoni. Mimi naimani kwenye level za shule kama tutaweka mfumo vizuri basi hivi vipaji tutaviona na kuviendeleza vizuri.

Kwenye Academy kuna Shida Sana kwa Sababu kuu Moja. Academy zinaendeshwa kwa Fedha kwahiyo mshiriki lazima alipe sasa Familia zetu nyingi kwenye hili tunakwama.
 
Back
Top Bottom