Tanzania yaanguka kwenye chati za "Urahisi wa kufanya Biashara" Duniani

Kang

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2008
Posts
5,655
Reaction score
2,506

Rwanda wako freshi sana, Huu ufisadi un atuangamiza, na hakuna anaye shughulikia haya viongozi wanacho anagalia ni maisha yao na familia zao hamna anaye care,

Rwanda na kupigana vita bado wanatupita mbali sana na Rwanda wangekuwa na resources kama za Tanzania wange kuwa wanaitafuta south africa kwa uchumi imara, wakati sisi tunafanya political economy, na kila kitu ni siasa Umeme siasa, Kodi siasa, Mikopo siasa
 

Kwa kweli nashindwa kuelewa ni nini kinachoendelea nchi! Ni kweli mazingira ya kufanya biashara yamekuwa magumu sana kwa wawekezaji wa nje, lakini hasa kwa wawekezaji wadogo wa ndani. Kuna watu sijui ni kwamba hawajui implication ya hii kitu au uzembe tu katika taasisi zao.

Hebu fikiria mipango kama Business Environment Strengthening Programme (BEST) na Property and Business Formalisation Programme (PBFP) inavyokula hela za walipa KODI lakini impact na output zake bado ni ndogo sana. Ina maana Eng. Salema na Lyimo hamuoni haya?

Yaan nchi kama RWANDA ukienda kusajil kampuni, inakuchukua takribani masaa nane to get it done (and when I say to get it done, i mean all the paper work), lakini Tanzania kufanya Name Search tu, ni zaidi ya siku tatu na bado tunasema eti tuko kwenye information era.

Sijui hawa watu huko wizara ya viwanda na biashara wanafanya nini? Kwa mfano Bunge lilipitisha sheria moja iitwayo BARA ( Business Activities Registration Act, 2007) lakini mpaka leo (%years later) haijaanza kutumika. Jamani hata kwa pilot project zinawashinda? Sheria hii pamoja na mambo mengine ilikuwa ina-decentralize shughuli za BRELA ili watu waweze kufanya usajili katika wilaya zao bila kulazimika kwenda Dar es Salaam, tena in ONE STOP SHOP.
 


True mkuu, kwa kweli Tanzania kuna Taasisi nyingi za kibiashara lakini wanacho fanya hakionekani,
1. BEST-
2. SIDO
3. MUVI- MUUNGANO WA VIKUNDI YA UJASIRIAMALI VIJIJINI

Na zingine nyingi hawa watu ukiona ripot zao utakubali kwamba wanafanya kazi ila ni usanii mtupu na wanaongoza kwa kutengeneza Data,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…