Tanzania yaenguliwa Mchezo wa Volleyball kwa kushindwa kutoa ada ya Dola 1,000

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
10 September 2021
Kigali, Rwanda

Tanzania imeshindwa kulipia ada ya dola za kimarekani US$ 1,000 zilizotakiwa kulipwa kabla ya kuruhusiwa kushiriki mashindano makubwa ya Afrika ya mchezo wa volleyball.

Pia nchi ya Tanzania ilishindwa kulipia US$ 50 kwa kila mtu aliyetarajiwa kuwepo ktk msafara wa wachezaji na viongozi, kiasi hicho kingetumika kama malipo ya malazi kwa timu ya Tanzania.

Michezo ni diplomasia, ni siasa, ni eneo la kujijenga kishawishi kimataifa n.k ni eneo lingine linaloweza kutumika kama njia ya kuitangaza nchi kikanda na kimataifa, na ndiyo maana nchi nyingi hutumia fedha kuhakikisha nchi zao zinashiriki ktk michezo na michuano mbalimbali ya kikanda na kimataifa.

======

Tanzania removed from African Volleyball Championship​

By Damas Sikubwabo
Published : September 10, 2021

The African Volleyball Federation has removed Tanzania from the ongoing CAVB Men's Africa Nations Volleyball Championship for failure to comply with their financial obligations.

Tanzania is understood to have failed to pay $1,000 participation fee and $50 per person per day for the 12 days meant for accommodation.

A statement from CAVB said that the team's removal is in accordance with the Africa volleyball confederation CAVB regulations.

As a result, Tanzania has lost their Group D game against Kenya by forfeiture, and will also not continue playing in the tournament.

The victory will be awarded to Kenya with a 3-0 score.
 
11.09.2021

RWANDA VS MOROCCO | CAVB Volleyball Men's Africa Nations Championship QUATER FINALS - 11.09.2021


Source : FRVB MEDIA
 
Tatizo sio Tanzania ni uongozi wa Volleyball.
 
Kwa kushindwa kulipa ada ya Tsh $1,000.

Serious kabisa au utani?
 
Kuna mjanja kala hiyo dola 1000... 🤣 🤣
Aiseee...
 
Tatizo sio Tanzania ni uongozi wa Volleyball.

Tatizo ni kubwa zaidi ya hilo, hapa ni viongozi kukosa kujenga utaifa, uzalendo na kubeza Michezo bila kufahamu umuhimu wake kwa taifa na kimataifa.

Viwanja vya wazi kuporwa na CCM kuvigeuza maegesho ya magari mijini/ car parking, shule kukosa viwanja vyake vya michezo, kushindwa kujitayarisha vizuri kwa ajili ya mashindano ya kimataifa, dunia na olimpiki.

Kwa kifupi CCM na serikali yake haijuwi nguvu ya michezo kiafya, kiuchumi, kidiplomasia, kutangaza nchi nje, kujenga utaifa kwa kuwaunganisha vijana bila kujali itikadi, imani , rangi n.k

 
Ndoto kubwa za chama cha mpira wa wavu (volleyball) Tanzania , TAVA za zazimika ghafla kufuatia kushindwa kulipia ada na malazi.

6 Sept 2021

TIMU YA TAIFA YA WAVU KWENDA RWANDA


Wanamichezo wametakiwa wametakiwa kuitambua thamani ya uwekezaji wa serikali kwenye sekta hiyo kwa kuongeza bidii na kupata mafanikio ikiwemo ushindi kwenye matukio mbalimbali ya kimashindano ndani na nje ya nchi wanayoshiriki.

Nasaha hiyo nzito inayowahimiza wanamichezo kuitia moyo serikali ili iendelee kuwasaidia wachezaji na timu za michezo mbalimbali nchini imetolewa na Afisa Michezo Mwandimizi kutoka Baraza la Michezo la Taifa Allen Alex wakati wa hafla ya kuikabidhi bendera timu ya taifa ya mchezo wa mpira wa wavu inayotarajiwa kuondoka usiku huu kuelekea nchini Rwanda kushiriki michuano ya mataifa ya Afrika.

Mwenyekiti wa chama cha mpira wa Wavu nchini (TAVA) Meja Jenerali Mstaafu Patrick Mlowezi Ametumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa kuchangia maendeleo makubwa ya chama hicho, nukuu ambayo imeungwa mkono na katibu Mkuu wake ambaye pia ameishukuru serikali kufanikisha safari hiyo ya Rwanda.

Msafara wa Tanzania kuelekea michuano hiyo unajumuisha watu kumi na nne, ikiwemo wachezaji kumi, kocha mkuu wa Timu hiyo, Meneja wa timu, Mwamuzi mmoja na mkuu wa Msafara kutoka Baraza la michezo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…