Tanzania yaichapa Somalia 1-0 mechi ya kwanza kufuzu CHAN 2023

Tanzania yaichapa Somalia 1-0 mechi ya kwanza kufuzu CHAN 2023

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
FYW4LQCWYAEe_1s.jpg

Timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Somalia katika mchezo wa kuwania Kufuzu Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN 2023) kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam, leo Julai 23, 2022.

Goli limefungwa na Abdul Hamis Sopu dakika ya 47, ukiwa ni mchezo wa kwanza wa mtoano Tanzania wakitambulika kuwa wapo ugenini kwa kuwa Somalia waliomba mchezo wao uchezwe uwanjani hapo

Timu hizo zinatarajiwa kurudiana wikiendi ijayo ambapo mshindi wa hapo ataenda kucheza dhidi ya Uganda, mchezo ambao utaamua nani anafuzu kwenda CHAN 2023.
FYW6zV9XEAQ2-S9.jpg
 
Somalia Wana timu, yaani wako kitimu ila pale mbele wamekosa mtu wa kuamua matokeo.
Wakikutangulia maji utaita mma.
 
Nasikia tungeshinda nyingi tu..... Lkn Fei Alikuwa alenga mtambaa panya tu....!
Mlioshuhudia,Ni Kweli..?
 
Timu inatoka kwenye nchi ambayo inakumbwa na mapigano mara kwa mara,tunatoka nayo kwa hayo Matokeo,are we serious?
Nchi hii bhana.
 
Back
Top Bottom